Nini tatizo la RC Mrisho Gambo na wasaidizi wake?

Nini tatizo la RC Mrisho Gambo na wasaidizi wake?

Nimeona wanachama wenzangu wa Chama Cha Mapinduzi wakiongelea kwa hisia tukio la Mkuu wa Mkoa Arusha ndugu yangu Mrisho Mashaka Gambo na Mkuu wa Wilaya ya Arusha ndugu yangu Gabriel Daqaro.

Bahati nzuri hawa wote ni marafiki zangu tofauti ni kuwa Dc wa Arusha siyo mwanasiasa kabisa lakini wote wawili wanafanana kuwa ni watu Wapole machoni pa watu.

Nakumbuka mwaka 2016 Mh Rc Arusha aliwahi kupatikana na tukio kama ili dhidi ya aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Arumeru ambaye kwa sasa ni mkuu wa Mkoa Manyara Mdogo wangu Alexander Pastory Mnyeti ambapo Mheshimiwa Gambo aliamua kumtimua kwenye kikao.

Sijajua nini kinampata Mheshimiwa Mrisho Gambo sijui ule mwili wake Mdogo watendaji wa chini yake wanamdharau au sijui tatizo ni nini?

Matukio kama Haya inaonyesha jinsi ambavyo watendaji wa serikali hawaelewani na kama hawaelewani maana yake achievement inakuwa ndogo.

Hivi karibuni tulimsikia Waziri Mkuu akiwaagiza mawaziri kwenda mkoa wa Kilimanjaro kusuluhisha mgogoro kati ya Mkuu wa Mkoa na madc wake.

Kwa mantiki hii inayoonyesha kuwa kuna shida kubwa ya mahusiano ya kikazi kati ya hawa makamisaa.

Ningewaomba wanaccm tufanye utafiti sana kabla ya kuongea na kushutumu upande wowote.

Katibu mkuu wa ccm Dr Bashiru Ally aliwahi kutamka mikoa ambayo hakuna mahusiano mazuri ya kiutendaji kati ya chama na Serikali.

Mkoa wa kwanza ilikuwa Mara, Arusha, Dar es salaam na Mbeya lakini kiujumla mahusiano ya Viongozi hayako sawa sehemu nyingi.

Utakuta Madc hawaelewani na maded Marc na makatibu Tawala mikoa Marc na ofisi za chama hawaelewani mbaya zaidi siku hizi wanachama wengi wa ccm ni wafuasi wa Viongozi.

Wanachama wengi wa ccm siku hizi wanashabikia Viongozi kuliko chama.

Kwahiyo kila kiongozi kwa nafasi yake ametengeneza wafuasi wake.

Leo ukitaka kukosoa utendaji wa Viongozi ndani ya chama na serikali utaambiwa una wivu na matusi ya wafuasi utayaoga.

Na hata ili la Arusha wafuasi wa Viongozi wako busy kutetea wapambe wao suala maadili ya Viongozi wa chama hakuna anayejali.

Na hii tabia ya wafuasi wa Viongozi imetamalaki mpk kwenye ngazi ya maamuzi kila kiongozi ana Godfather wake Ndiyo maana hukawii sasa hivi ndani ya chama matamko ya wanachama hayaishi hata kama hayana tija kwa chama au taifa ili mradi aonekane.

Kusema ukweli mahusiano ya kikazi kati ya Mkuu wa Mkoa Arusha na wasaidizi ina shida siyo mazuri sana.

Na Frey Cosseny

Sent using Jamii Forums mobile app
Utawala uliofitinika, mlitarget kuua upinzani, kwa kuteua makada nafasi za utendaji, mungu hadhiakiwi tatizo mlilolitengeza litabackfire kwenye uchaguzi 2020
 
Nimeona wanachama wenzangu wa Chama Cha Mapinduzi wakiongelea kwa hisia tukio la Mkuu wa Mkoa Arusha ndugu yangu Mrisho Mashaka Gambo na Mkuu wa Wilaya ya Arusha ndugu yangu Gabriel Daqaro.

Bahati nzuri hawa wote ni marafiki zangu tofauti ni kuwa Dc wa Arusha siyo mwanasiasa kabisa lakini wote wawili wanafanana kuwa ni watu Wapole machoni pa watu.

Nakumbuka mwaka 2016 Mh Rc Arusha aliwahi kupatikana na tukio kama ili dhidi ya aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Arumeru ambaye kwa sasa ni mkuu wa Mkoa Manyara Mdogo wangu Alexander Pastory Mnyeti ambapo Mheshimiwa Gambo aliamua kumtimua kwenye kikao.

Sijajua nini kinampata Mheshimiwa Mrisho Gambo sijui ule mwili wake Mdogo watendaji wa chini yake wanamdharau au sijui tatizo ni nini?

Matukio kama Haya inaonyesha jinsi ambavyo watendaji wa serikali hawaelewani na kama hawaelewani maana yake achievement inakuwa ndogo.

Hivi karibuni tulimsikia Waziri Mkuu akiwaagiza mawaziri kwenda mkoa wa Kilimanjaro kusuluhisha mgogoro kati ya Mkuu wa Mkoa na madc wake.

Kwa mantiki hii inayoonyesha kuwa kuna shida kubwa ya mahusiano ya kikazi kati ya hawa makamisaa.

Ningewaomba wanaccm tufanye utafiti sana kabla ya kuongea na kushutumu upande wowote.

Katibu mkuu wa ccm Dr Bashiru Ally aliwahi kutamka mikoa ambayo hakuna mahusiano mazuri ya kiutendaji kati ya chama na Serikali.

Mkoa wa kwanza ilikuwa Mara, Arusha, Dar es salaam na Mbeya lakini kiujumla mahusiano ya Viongozi hayako sawa sehemu nyingi.

Utakuta Madc hawaelewani na maded Marc na makatibu Tawala mikoa Marc na ofisi za chama hawaelewani mbaya zaidi siku hizi wanachama wengi wa ccm ni wafuasi wa Viongozi.

Wanachama wengi wa ccm siku hizi wanashabikia Viongozi kuliko chama.

Kwahiyo kila kiongozi kwa nafasi yake ametengeneza wafuasi wake.

Leo ukitaka kukosoa utendaji wa Viongozi ndani ya chama na serikali utaambiwa una wivu na matusi ya wafuasi utayaoga.

Na hata ili la Arusha wafuasi wa Viongozi wako busy kutetea wapambe wao suala maadili ya Viongozi wa chama hakuna anayejali.

Na hii tabia ya wafuasi wa Viongozi imetamalaki mpk kwenye ngazi ya maamuzi kila kiongozi ana Godfather wake Ndiyo maana hukawii sasa hivi ndani ya chama matamko ya wanachama hayaishi hata kama hayana tija kwa chama au taifa ili mradi aonekane.

Kusema ukweli mahusiano ya kikazi kati ya Mkuu wa Mkoa Arusha na wasaidizi ina shida siyo mazuri sana.

Na Frey Cosseny

Sent using Jamii Forums mobile app
UTEUZI WA RC ARUSHA NA DC ARUSHA WATENGULIA

Rais Magufuli, leo ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na nafasi yake imechukuliwa na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Idd Kimanta

Pia ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqarro na nafasi yake imechukuliwa na Kenan Kihongosi wa UVCCM Iringa

Aidha, ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Dkt. Maulid Madeni na kumteua Dkt. John Pima kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri

#JFLeo #Magufuli
View attachment 1483586

Soma pia:

1) Arusha: RC Gambo aibua sintofahamu Soko la Samunge, abeza taarifa ya DC na Mkurugenzi

2) Nini tatizo la RC Mrisho Gambo na wasaidizi wake?

3) Ugomvi baina ya RC Gambo na Mkurugenzi wa Jiji Arusha lashika kasi

4) RC Gambo aumbuka vijana wa CCM Arusha wamshambulia mitandaoni, aamua “ku left “

5) Ntibenda: Kama kuondolewa kwangu kama RC Arusha kuna mkono wa mtu; Mungu atalipa
Duh...!.
Kuna kitu niliwahi kushauri kumhusu Mrisho Gambo.
Rais Magufuli, somo la managing diversity kwa Serikali yako linahitajika
P
 
Back
Top Bottom