Nini maoni yako kuhusu kauli ya RC Dodoma kuwa Mwanafunzi akichelewa kuripoti shule atalimishwa matuta kumi?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
877
4,105
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amesema mwanafunzi akichelewa kuripoti shule atalimishwa matuta kumi, kauli hii ni amri kwa wakuu wakuu wa shule lakini tujiulize ni amri halali?

Kwanini mwanafunzi anachelewa shule? Ni mwanafunzi wa umri gani atalimishwa matuta kumi? Je hata wanafunzi wa private school ambao wengi ni watoto wa viongozi na wanasiasa wakichelewa watalimishwa matatu kumi au ni agizo kwa watoto wa wakulima pekee?

Ni kwa namna gani kauli hii inamshinikiza mzazi kutimiza wajibu wake? Kama mtoto hajanukuliwa uniform akichelewa shule anastahili adhabu pia?

Kwanini tunaamini watoto ndio wanapaswa kupewa adhabu badala ya wazazi?
 
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amesema mwanafunzi akichelewa kuripoti shule atalimishwa matuta kumi, kauli hii ni amri kwa wakuu wakuu wa shule lakini tujiulize ni amri halali?

Kwanini mwanafunzi anachelewa shule? Ni mwanafunzi wa umri gani atalimishwa matuta kumi? Je hata wanafunzi wa private school ambao wengi ni watoto wa viongozi na wanasiasa wakichelewa watalimishwa matatu kumi au ni agizo kwa watoto wa wakulima pekee?

Ni kwa namna gani kauli hii inamshinikiza mzazi kutimiza wajibu wake? Kama mtoto hajanukuliwa uniform akichelewa shule anastahili adhabu pia?

Kwanini tunaamini watoto ndio wanapaswa kupewa adhabu badala ya wazazi?
Mkuu wa Mkoa Bi Sinyamule amejisahau kwenye madaraka.

Waziri Hussein Bashe alikwisha kemea sana suala la kulima kuwa adhabu kwa wanafunzi. Kwa kuwa inaleta NEGATIVITY sana.

Kama RC Dodoma hatabadili kauli yake basi juhudi za Rais Samia kupitia Waziri Hussein Bashe za kuwafanya vijana ma graduate wapende kilimo zitakwama.
 
Kama Elimu ni bure, kwanini wachelewe? Hata hivyo mbona adhabu ya kawaida sana, kwasababu wengi wao baada ya kuwa wamehitimu elimu yao ya msingi ni wakulima tarajiwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom