Nini maana ya kulipia bima ya papo kwa papo?

Koryo2

JF-Expert Member
Nov 28, 2016
2,056
2,515
Leo kwa kweli nimeichukia sana Wizara ya Afya. Leo asubuhi nilimpeleka mgonjwa wangu ambaye alikuwa amevimba mguu ili apate matibabu katika KITUO CHA AFYA CHA UTEGI -WILAYA YA RORYA, Mkoa wa Mara.

Kwanza tuliambiwa kulipa Bima ya Afya ya papo kwa papo ya Tshs.5,000(elfu tano). Alipomaliza kuchunguzwa tukaambiwa twende tununue dawa. Nimeenda kununua kwenye maduka ya binafsi ya Tshs.15,000(Elfu kumi na tano). Ninauliza maswali yafuatayo:-

(1) Nini maana ya kulipia bima ya papo kwa papo?
(2) Kwa nini kila siku Waziri wa Afya anasimama Bungeni na kutuaminisha kuwa dawa zipo na Serikali imetenga fedha nyingi kwa ajili ya madawa?
(3) Kwa nini dawa zinakosekana kwenye hospitali, Vituo vya afya na dispensari hapa nchini?

Kwa kweli leo nimewachukia sana. Msiwe mnatudanganya.
 
Ulichajiwa hela ya ziada baada ya kutoa hiyo elfu 5? Ulilipia gharama ya kumuona daktari? Ulilipia vipimo vya maabara?
 
Mkuu kawaida sana hiyooo

Nenda MUHIMBILI matibabu unapata dawa utayopangiwa ni bei kubwa kuzidi gharama ya matibabu au nusu yake ajabu ukienda duka lso hamna utasikia toka getini pale kuna duka wanauza ambapo ukienda kweli ipo na,ni bei hutaki kafie mbeke.

Ukichunguza wenye hizo famasi nje ya hospital ni madkt wakubwa au vigogo wakubwa sana ndani ya hospital yasni ni untouchable.
 
Back
Top Bottom