Nini Kitaamua Mshindi wa Kura ya Urais na Kwanini?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
Matokeo ya Uchaguzi wa Urais mwaka huu yataamuliwa na vitu vingi au mambo mengi. NInaamini mambo makubwa kadhaa yataamua kama ni John Magufuli au Edward Lowassa anaibuka kidedea. Hili lote linahusiana na nani atapata kura nyingi na kwa nini.

Binafsi naamini yafuatayo yataamua:

1. Watakaojitokeza kupiga kura (voters turnout). Hili ndilo jambo kubwa zaidi litakaloamua nani anashindwa au kushindwa. Ikumbukwe kuwa kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2010 Watanzania waliweza kujitokeza kupika kura kwa wingi mno kiasi kwamba hakuna Uchaguzi wowote Mkuu tangu uhuru hadi ule wa 2010 ambapo idadi ya wapiga kura ilikuwa chini ya asilimia kama 70 hivi ya watu waliojiandikisha.

Hata hivyo mwaka 2010 kwa mara ya kwanza- pamoja na hamasa yote ya kampeni ? ni kama asilimia 42 tu hivi ya Watanzania waliojiandikisha kupiga kura ndio walipiga kura. Na hapo ndipo CCM na mgombea wake Rais Jakaya Kikwete waliweza kuibuka na ushindi wa kama asilimia 62 hivi.

Katika Uchaguzi Huu inaweza ikatokea hivyo hivyo tena; endapo wapiga kura hawatafikia ile asilimia kama 70 ya waliojiandikisha kupiga kura ni wazi CCM itashinda. Kama wapiga kura wengi watajitokeza kupiga kura na hapa nafikiria iwe karibu ya asilimia 80 hivi ndio CHADEMA inaweza kushinda. Ikumbukwe kuwa kinachopiganiwa ni kufikia asilimia 50 tu hivi ya wapiga kura kuweza kumpata mshindi.

Kama wapiga kura wengi zaidi watajitokeza maeneo ya mijini (kwa asilimia kubwa karibu ya 70-80 basi Lowassa ni rahisi zaidi kushinda.

2. Kutokana na hilo hapo juu jambo jingine liko wazi; endapo wana CCM wengi (wale wenye kadi) wataamua kuvuka (crossover) na kumpigia mgombea wa CHADEMA basi watasaidia sana kuifikisha hiyo asilimia 50 ambayo Lowassa anaitafuta. Hata hivyo, kama wana CCM wengi hawa wataamua kusimama na chama chao na kupiga kura basi hilo litampendelea Magufuli zaidi kwani Magufuli anategemea kwanza kabisa kura za wana CCM halafu za wengine.

Upande mwingine pia ni kweli; endapo wapo wana CDM au watu wa upinzani ambao wataamua kwenda kinyume na mgombea wa CHADEMA na kuamua kumpigia kura Magufuli wakati Magufuli hajapoteza wana CCM kwenda kwa Lowassa ni wazi kuwa Magufuli atashinda. Hivyo hapa kuna swali la crossover ya wanachama.

3. Mojawapo ya kundi ambalo halijaeleweka sana na labda halijajionesha sana ni wale ambao hawana vyama na hawakuwa wamefanya uamuzi hadi dakika hizi za mwisho (independents). Sijui kundi hili ni kubwa kiasi gani kwani uchaguzi wa mwaka huu unaonekana umegawa watu sehemu mbili kubwa na si tatu hivyo linaweza kuwa kundi dogo lakini lenye nguvu. Fikiria tu kama kura zinakaribiana sana halafu kuna
 
Mshindi Ni Lowassa, CCM Haikubariki na Vijana Ndio Wamejaa Vituoni. Ni Mabadiriko Hakuna Namna.Je Umemkaribisha Dr.

Slaa Huko Uliko.Ni Lowassa Ni Mabadiriko Wala Hakuna Namna Nyingine.Lowassa Atashinda Kwa zaidi ya 70% Sisi ndio Tupo Site Tunaona

Sio wewe Unaecheza na keyboard...Na Kubeba Mabox USA.
 
Subiria Huku Huko Matokeo, Pamoja Na Kufanya Kazi Yako Ya UKIBARAKA, LOWASSA Ndiye RAIS.
 
1. Wapiga kura wengi ni vijana ambao kwa asilimia kubwa siyo wanachama wa CCM

2. Ccm haina mtaji huo unaousema, wengi wamejitoa kwa kutoridhishwa na utendaji wa chama

3. Upepo, unavumia upinzani

4. Uchaguzi huu ni tofauti sana na wa 2010, interms of candidates, inflence, na voters
 
Utabiri wa nini wakati sie tushaanza kupiga kura asubuhi hii.
Subiri matokeo hakuna haja ya kufanya utabiri hapa...

Kazi yako ya kupigia debe ccm umefanya kwa miezi miwili bado hujaridhika? ?
 
Sitaki kumbuka zamani............................. ndugu MM umepuuzwa kama kinyesi cha mgonjwa wa EBOLA
 
1. Wapiga kura wengi ni vijana ambao kwa asilimia kubwa siyo wanachama wa CCM

2. Ccm haina mtaji huo unaousema, wengi wamejitoa kwa kutoridhishwa na utendaji wa chama

3. Upepo, unavumia upinzani

4. Uchaguzi huu ni tofauti sana na wa 2010, interms of candidates, inflence, na voters

kitu mnachosahau kwenye hao vijana wengi ni wasichana/wanawake na hawapendi upinzani kwa sababu ya woga na kutokuelewa mambo! wale bodaboda ni wachache sana sema vurugu nyingi
 
Mzee mwenzangu mwanakijiji asie ishi kijijini pole huku nyumbani sio wanawake wanaume wote mabadiliko huyo swahiba yako Dr Thaa hakuwa na umaarufu wa mrema na pia mrema hana umaarufu wa Edward lowasa ndio maana unao waandikia wanategemea sympathy toka kwako na watu wengine ambao hawapo nyumbani, kama kina chahali rudi nyumbani tulijenge Taifa watanzania wana amua leo
NUKUU YA LEO>
Kuhubiri democrasia ni kitu kingine na kusimamia democrasia ni jambo lingine!! kama nchi mwanachama wa jumuia ya AFRIKA MASHARIKI tunafuatilia yale yanayoendelea katika TANZANIA wakati ikielekea uchaguzi wao mkuu,hivyo tunahamu ya kuona rafiki yetu mwenyekiti wetu anayesimamia jumuiya yetu akithibitisha kwetu namna ya democrasia inavyotakiwa kusimamiwa kwa vitendo nchini Tanzania ili ajitofautishe nami ama na "NKURUNZIZA" {PAUL KAGAME}
 
mbwa akikutangazia kuna msiba!; ukidharau utakuta wamemaliza kuzika...
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji, nakushukuru sana kwa hii Mada. Kumbe na wewe kichaa chako kile kilikuwa ni kichaa cha msimu tuu kama ulivyo wazimu wa msimu, nimekunote katika bandiko hili your are now back to your senses with your usual objectivity!.

Welcome back to your real self, na tusubiri kupokea reality ndipo tukumbushane, wa kupongezana kupongezana, na wakupeana pole, tupeane pole!.

Pasco
 
Huyu jamaa ni House Boy huko majuu lakini yuko bise kuripoti ishu za Uchaguzi wakati hata kura hapigi, ni wajinga pekee ndo watako msapoti that is why amekimbilia jukwaa hili make kule watu walisha mchoka
 
kitu mnachosahau kwenye hao vijana wengi ni wasichana/wanawake na hawapendi upinzani kwa sababu ya woga na kutokuelewa mambo! wale bodaboda ni wachache sana sema vurugu nyingi

Hebu ongea kwa Nguvu Niffah akusikie
Kwa hiyo waliokua wanaenda kwenye kampeni walikua wanaume eeh ??
 
Back
Top Bottom