Nini kinaendelea Malawi?

Mazungumzo yamekwisha kwa bila bila

Waziri wa mambo ya nje Malawi apendekeza suala lipelekwe International Court of Justice

Mambe ashauri watoe fursa nyingine ya mazungumzo

Watakutana tena Septemba 10 hadi 14 Dar es Salaam

Katibu mkuu Wizara ya Mambo Ya Nje Malawi asema baraza la mawaziri litakutana kujadili uwezekano wa kusimamisha utafiti huo wa mafuta kama ambavyo Tanzania imependekeza ili kutafuta suluhisho kwanza. Hata hivyo Malawi wanaona kwa kufanya hivyo watakuwa wamekiuka masharti ya mkataba wao na kampuni inayoendesha utafiti
 

Kama kweli usemayo ni kweli nimesikitika sana..nalia uchungu juu ya ziwa hilo limeshatutoka....na haya ndio matatizo ya kuleta ngonjera kwenye v2 serious...jibu la swala hili lilikuwa moja tuu nalo ni NO...mpaka ni katikati ya ziwa lkn sijui diplomasia sijui nini ni kuonesha ulegelege hata wamalawi ma mataifa makubwa yameona sie ni waoga...byee ziwa nyasa
 
Wamalawi walishasema ziwa ni lao. Sidhani kama wanaweza kubadili msimamo kwenye mjadala.
 

Unapopeleka kesi mahakamani maana yake uko tayari kukubali hukumu ya mwisho. Sisi hatuko tayari kukubali hukumu ya mwisho iwapo haisemi ziwa pasu kwa pasu. Kwa hiyo swala la mahakama ni kupoteza muda na pesa. Mazungumzo yakishindikana, tuendelee tu kulinda mpaka wetu kama tunavyolinda mipaka mingine.
 

Kitendo cha Membe kushawishi Malawi kwamba zitumike njia nyingine badala ya kukimbilia IJC napata picha Tanzania hatujatoa hoja convincing. Ndo maana tunaogopa kwenda kwenye vyombo vya sheria
 
Kitendo cha Membe kushawishi Malawi kwamba zitumike njia nyingine badala ya kukimbilia IJC napata picha Tanzania hatujatoa hoza convincing. Ndo maana tunaogopa kwenda kwenye vyombo vya sheria

It is true...kabisa..yani inaonesha kila dalili ya kushindwa maana kama watu wankuita kwenye mazungumzo unahsindwa kubadilisha kitu hata uite mazungumzo mara ngapi haisadii wakati mweingine ni misimamo ndio inasaidia mfano wenyewe wamalali wanameshaweka msimamo hata ujija kwenye mazungumzo wanakupa msimamo wao ndio maana unaona hakuna mafanikio sasa sie hatuna msimamo tuna amini kwenye kuwashawishi wao wabadili msimamo wao...too late hata huku ICC tunashindwa nakwambia dalili zipo wazi kbs...hatujaonesha ukakamavu wetu ktk hili adui wameshatujua tunaogopa kwisha kazi ngoja tuone.
 
km kweli waandishi wetu wamekamatwa huko kwa kutoa taarifa za Kikao kilipokuwa kikiendelea ni haki kabisa maana baada ya Balozi kutufahamisha tungekaa kimya na sisi lakini tuligoma hata ushauri tuliopeana kuwa si busara kuendelea au kuanika anayotutumia Balozi wetu watu waliendelea humu JF mpaka ikaonekana hata waliotumwa hawafai na hawaujui mpaka ulipopita, Jamani Malawi itatufikisha pabaya hasa sisi waandishi makanjanja humu JF watu wanachukulia data kwa uhakika km vile ugomvi wa TBC na waislamu kuhusu SENSA
 

Ningeona ajabu kusiwe na pendekezo kwamba kama imeshindikana tukutane kwenye corridor za Mahakama ya Kimataifa.
Aliedhani kwamba mazungumzo yasingeisha kwa pendekezo hilo basi ni kati ya wale waropokaji wengi humu JF.
 

Upende usipende huwezi kumzuia mtu duniani asikupeleke mahakamani. Kama wamalawi wakitupeleka mahakamani na hukumu ya mwisho ikawa nzuri kwao, wewe jiandae na statement kama ya Museveni kukiachia Kisiwa cha Mingingo kwenda Kenya na uwe mpole.

HUna ubavu wa kuzuia dunia nzima iache kuwasaidia Malawi kijeshi kulinda haki yao watakayopewa na Mahakama ya Kimataifa.

Na hilo litakuwa fundisho kubwa la adabu na kama ni virungu vyako nenda kawasubiri CHADEMA na maandamano yao lakini si wanaume waliokubwaga mahakama ya kimataifa kwa hoja thabiti.
 
Kitendo cha Membe kushawishi Malawi kwamba zitumike njia nyingine badala ya kukimbilia IJC napata picha Tanzania hatujatoa hoja convincing. Ndo maana tunaogopa kwenda kwenye vyombo vya sheria

Mnadhani hata huko mkutanoni ni kasi cha kwenda na kumba wimbo usemao MIMI NI MZALENDO, MIMI NI MZALENDO, MIMI NI MZALENDO.

Shusha data wausikilize na si kupiga domo kama wakurupukaji wa humu eti MIMI NI MZALENDO, wakati hujasoma hata page moja ya history ya mpaka huu.

Ziko wapi porojo za Balozi kwamba presentation yao ilikuwa kama Phd thesis na yao ilikuwa pass grade. Kuumbuka tupu.

BInafsi niliuosma vilivyo mgogoro wa mpaka huu. NImesoma post na kuandika nyingi sana humu. Yote ni kutaka walau kujua kama kuna post itakayonishawishi tupate ziwa hili.

Kwa ujumla asilimia zangu za kutopata hata tone moja la ziwa zilikuwa ni zaidi ya 96 na zilizidi kupanda kila nikisoma post za watu wa humu.

Kwa ujumla Balozi alishusha kabisa matumaini yangu kupata ziwa hili.

Fundisho.
 

Mkuu Ukwaju walokamatwa walikuwa ni waandishi wawili wa Malawi
 

Haya sasa. Anzeni kumwita Membe naye ni mmalawi. Kushindwa kuhusu hili mimi sina wasiwasi nako.

Nilisema jana kwamba nina hamu mazungumzoa yaishe ili tufundishane adabu.

Huwezi kudai ziwa kama ni lako kwa kigezo cha kushabikiwa na watanzani awote huku wanaokuonya kwamba utaumbuka unawaona kama wamalawi.

Furahieni matokeo msisikitike. Mimi sisikitiki hata tone. Mliyataka wenyewe mlipokuwa mnaukimbia ukweli.
 
Ni vita tu ndo itatoa solution..hakuna cha mahakama wala vikao vya nini sijuhi
 

Mimi matumaini yangu ndo ICJ. Kule lazima pasu kwa pasu
 

Ndugu,

Usisingizie watu kwamba wameanika aliyoandika Balozi. Mwambie balozi wako hili ni fundisho aache ushamba kwani facebook inasomwa duniani kote na wamalawi hawahitaji kuja JF kusoma alichoandika Balozi huko kwenye facebook yake.

BInafsi nimeandika sana ukweli ninaoujuakhusu mpaka huu, sasa unaposema tuliandika hadi waliotumwa wakaonekana hawajui basi udhaifu ni wao. Si mlituambia kwamba walipeka Phd Thesis. Sasa kama sasa ndiyo mnaona tuliyoleta sisi humu yalifanya hadi waonekane vilaza basi maana yake tuliyoandika humu tunapaswa kupata award zaidi ya Phd!

Na kama sasa mnaona tumepresent sdata nzuri humu JF basi idumu JF kuanika uozo ikiwemo hata uozo wa wanaoenda kutuwakilisha nje yaani uozo wa ukilaza na kudesa.
 
Ni vita tu ndo itatoa solution..hakuna cha mahakama wala vikao vya nini sijuhi

Kasome historia uone jinsi Saddam alivyoidharau Kuwait na udogo wake na kweli aliikavamia na kuikamata ndani ya masaa kadhaa.
 

Nafikiri wewe ndo mshamba wa haki, haya mashambulio yako juu yake ungeyaandika namna hii kama ungejiridhisha kwamba unayemwita mshamba ni member humu, naye kupata nafasi kwa kurudisha makombora if any.

Mambo ya kutuaminisha kwamba yeye ni mshamba wakati huna hakika yeye ni mwanachama hapa, huo ni utoto kwa kuifinyanga haki yakuji-defend. Elezea alipokosea na wewe ungekuwa kama wewe ungefanya vipi, na usiende kuanza kumshambulia wakati yeye hayupo-ushauri tu.
 
Inaelekea matokeo siyo mazuri, maana siku ya kwanza mbwembwe zilikuwa nyingi. Baada ya hapo media za Tanzania na Malawi ziko kimya, walioenda kujadili nao wako kimya! Hata balozi wetu aliyenza kwa majigambo sasa yuko kimya!!!
Ni lazima yawe magumu!... Tulikuwa tunamiliki sehemu ya ziwa hilo hata kabla ya makubaliano ya mwaka 1890 kati ya mjerumani na mwingereza. Kando ya ziwa kulikuwa na wanyasa upande wa malawi na wamanda, wanyakyusa, wakisi, n.k. kando ya ziwa. Makubaliano ya wageni yananyang'ana haki za wenyeji!!!!!!............. NINAWATAKIA KILA LA KHERI WATANZANIA WANAOSHIRIKI VIKAO HIVI WATETEE HAKI YA WATANZANIA!.. ...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…