Nini kimeyakumba mabasi ya mwendokasi

FB_IMG_1554838936531.jpg
 
Halafu eti kiongozi yupo hapo anaangaika na akina liquid, mara tezi dume, ujinga mtupu!
 
Hiyo route wapewe wamiliki kadhaa wa daladala zile kubwakubwa wasaidiane na hao UDART ni suala la kupaka rangi ya UDART tu hii habari ya mabasi machache au mabovu itajisolve kwasababu kila basi litahudumiwa na mmiliki wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Imerip kama UDA,heri angepewa aliyeshinda tenda
Mradi huu ilibidi waachie wale waholanzi kwa mwaka mzima. Then waachie wabongo kwa miezi kadhaa kwa majaribio.BRT ni mradi serious kabisa, hauhitaji siasa.
 
Badala ya kua suluhisho la tatizo la Usafiri hapa Jijini .Mwendokasi imekuwa Ni MwendoShida kwa kweli.Ni iombe mamlaka inayo Shughurikia Usafiri huu hapa jijini Wajipange upya kwani kumekua na matatizo makubwa sana kwenye Usafiri huu.Kwanza ni mabasi kujaza abiria kupita kiasi .(2) Ni waombe waondoe utaratibu wa Express.kwani huu utaratibu huu umekuwa Ni mwanya kwa madereva wa mabasi haya kupita vituo vidogo hata kama yapo tupu na wakati kwenye vituo hivyo wapo abiria .(3),Kwenye mabasi haya pale malangoni kuna eneo limeandikwa si ruhusa kusimama hapa.lakini eneo hilo utakuta wame simama Watu zaidi ya Kumi.kwa maana hiyo kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria kwenye mabasi haya(4)Vifaa Vingi katika mabasi haya kwa sasa havitumiki ipasavyo kama Vipaza sauti madereva awavitumii kabisa na hata yule dada anesema kituo kinachofata siku hizi asikiki zaidi ya Siku kama Simba Sc inacheza ndio utawasikia washabiki wa timu hiyo wakisema huko mitaani .(5)Vituoni kumekuwa na uvujaji mkubwa wa mapato .na haswa huu mtindo wa ukinunua tiketi na kuchanwa pale na wale wahudumu pale kwenye kigeti cha mwisho .sasa awa Wahudumu sio malaika tiketi zingine azichanwi matokeo yake zinarudi dirishani kuuzwa tena .(6) ni dhuruma tuliyo fanyiwa sisi tuliouziwa kadi .sasa kadi hizi aziwezi kununua huduma matokeo yake zimekuwa ni mapambo kwenye Waleti zetu na kwenye mikoba .tuwaombe wafanye mpango wachukue kadi zao wazipeleke jumba la makumbusho.Na Mwisho kabisa ni lugha mbaya kwa wahudumu wa Vituoni unapotoa Noti ya shilingi Elfu kumi au tano.Utazania Umetoa pesa ya kuzimu kwa maneno utakayotolewa na muhudumu .matokeo yake utangandishwa pale mpaka chenji ipatikane .Kusema kweli kuna mambo mengi sana kwenye Usafiri huu wa Mwendo Shida mwendo tabu .niwaombe askari wa Usalama barabarani waanze kukagua haya mabasi waone uvunjifu wa sheria kwenye mabasi haya .ni vizuri kuzuia kuliko kutibu.Asante naomba kuwakilisha

Sent using Jamii Forums mobile app
Hilo la chenji ya 10000 lilinikuta pale Morocco

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpaka leo nna mwezi mmoja sasa naugulia maumivu ya kutegua bega. Nilikuwa napanda haya magari kitemi. Wakizuia mlangoni mimi kazi yangu ilikuwa ni kuvishika vile vidude vya kukamatia juu...basi nawaminya mpaka naingia. Siku moja looooooooo....niliking'ang'ania mpaka nikahisi kuna kasindano kamepenya kwenye bega langu....nikashuka salama. Ile kufika nyumbani maumivu niliyoyapata ni balaa. Kukakucha hivyohivyo na maumivu yake. Nikajipeleka hospital nilichoambiwa duuuu...ndo naendelea na tiba ya mwendo Kasi hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom