Nini Kilimkuta Dr Ferdinand Masako?

Nini Kilimkuta Dr Ferdinand Masako?

Ciprofloxacin.

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2015
Posts
1,583
Reaction score
2,702
Alikuwa ni mtanzania mzalendo na mwenye uchungu na taifa lake,hakutaka kwenda Namibia au Botswana ili kupata mshahara mkubwa,badala yake akaanzisha hosp kurasini ya kutibu magonjwa ya moyo (THI)Tanzania Heart Institute akijua kuwa ingewasaidia watanzania wenzake maana hapakuwa na matibabu hayo Tanzania nzima,enzi zile umri wangu ulikuwa mdogo nikasikia fununu tu kuwa alikuwa anafanyiwa mizengwe sana na watu waliojua kuwa anaenda kufanikiwa kupitia taasisi yake hiyo,baadae alifariki,jamani kwa mnaojua A to Z na mkanda mzima wa Dr Masako,nini hasa kilijiri na ilikuwaje?
 
Dr masako na THI sijui hebu uliza na peruzi vizuri naona umerudia masako na jina lako ni dawa utakuwa unasomea udaktari au daktari naomba udadisi jina kwanza usije pata maelezo tofauti
 
Kuna uzi upo humu JF kuhusu huyo Dr...akiitwa Masau not Masako!
 
UFAFANUZI.
1/Nadhani unamaanisha Dr.Ferdinand Masao ambaye kwa sasa ni marehemu.

2/Fitna, Chuki, Mizengwe dhidi yake kutoka kwa Baadhi ya Watanzania wakiwemo Madaktari, Maafisa wa wizara ya Afya, viongozi kadhaa kutoka serikali ndiyo vilichangia sana Dr.Masao kufariki. Stress za maisha akipambana kutaka kufanikisha ndoto zake zilipelekea kuugua na kufariki. Alikuwa na ndoto njema sana na pana sana kwa Tanzania, hakuwahi kukata tamaa kabisa.

3/Hakuwahi kuwatendea ubaya wowote watanzania, alitumia Muda wake, Utaalamu wake, Kipaji chake na Juhudi zake binafsi katika kuanzisha Hospitali ya kutibu na upasuaji wa moyo ili huduma hiyo iwepo nchini na watu wasiendelee kupelekwa nje, Lakini alichokumbana nacho, kinatia huzuni sana. Alifanyiwa kila aina ya Fitna, alikosa watu wakumtetea, alisakamwa mpaka basi.

4/Kiukweli kabisa, Tanzania tumeitupa Lulu ya thamani sana, Dr.Masao alikuwa ni lulu tena lulu ya thamani sana. Katika hili laana iko juu ya nchi yetu. Mbegu ya Fitna tuliyoipandikiza itatutafuna mpaka basi. Kila mtaalamu atakayeibuka hapa Tanzania atapigwa vita vibaya sana. Usishangae ya Dr.Mwaka kupigwa vita badala ya kusaidiwa kusonga mbele. Ni mwendelezo ule ule.
 
Dr. Ferdinand Masau ninampa heshima ya pekee. Alihusika kumtibu ndugu yangu wa karibu ugonjwa wa moyo kwa gharama nafuu kabisa na amepona hata kidonge hatumii. Hakuwa na tamaaa kabisa. Ilifika mahali akaruhusu tena kwa kutukimbiza kuwa tusiende tena check up akawa alitoa consultation za after every year. Ingekuwa walafi ungeambiwa kila mwezi rudi ili tu akukamue hela. Rest in Peace mtaalam uliyepigwa vita hata na serikali yako. Inakatisha tamaa sana. Ninaamini ingekuwa ni serikali ya Magufuli wala asingepigwa vita kwa kuwa mchango wake ulikuwa wazi.
 
Nakumbuka sakata lilianza katika jengo alilopanga mara linadaiwa..ikaonekana kuna wafadhili wanataka kulipa ili aendelee kufanya kazi wizara ikamaliza kwa kusema ana vyeti vya Marekani haruhusiwi kufanya kazi hapa..wakiugua wanaenda Marekani kutibiwa,,harafu vyeti vyao hamvitambui akili za wapi izo..nilichogundua ni kuwa kuna watu wanapata Faida kwa kuwa na hizi huduma mbovu katika Afya.maana ma Dr hawa ndio wanathaminiwa sana Nchi za kusini huko..
 
Alitaka kuharibu dili za wakubwa kutibiwa Apollo India, ndio hivyo serikali ikiamua kukumaliza haishindwi, itatafuta loop hole yoyote ya udhaifu wako, basi wanapitia hapo hapo. Alikuwa na deni nssf la pango la nyumba, basi alishughulikiwa kwa nguvu za ajabu utadhani ni yeye pekee anadaiwa na nssf, na waziri alikuwa mkali.kweli hata maana alisema hela lazima ilipwe haraka. Basi mwisho wa siku wakakamata vifaa vyake vyote vya hospitali na kiviuza. Nadhani ilimuumuza sana, muda mfupi baadaye akafariki.
 
Dr masako na THI sijui hebu uliza na peruzi vizuri naona umerudia masako na jina lako ni dawa utakuwa unasomea udaktari au daktari naomba udadisi jina kwanza usije pata maelezo tofauti

Hiyo ni ID tu mkuu niliwahi kuugua UTI hiyo dawa ndo ikaniponya, ndo maana nikalipenda hilo jina.
 
Serikali ya CCM chini ya Benjamin Mkapa haichomoki hapa
 
Dr. Ferdinand Masau ninampa heshima ya pekee. Alihusika kumtibu ndugu yangu wa karibu ugonjwa wa moyo kwa gharama nafuu kabisa na amepona hata kidonge hatumii. Hakuwa na tamaaa kabisa. Ilifika mahali akaruhusu tena kwa kutukimbiza kuwa tusiende tena check up akawa alitoa consultation za after every year. Ingekuwa walafi ungeambiwa kila mwezi rudi ili tu akukamue hela. Rest in Peace mtaalam uliyepigwa vita hata na serikali yako. Inakatisha tamaa sana. Ninaamini ingekuwa ni serikali ya Magufuli wala asingepigwa vita kwa kuwa mchango wake ulikuwa wazi.

"wema hawana MAISHA"
 
Kwenda kutibiwa India ni dili kubwa sana kwa katibu mkuu wizara ya afya na vigogo wengine. Mwaka 2013 Apollo Hospital Ilikua inaidai serikali ya TZ billion 56. Hio hela hulipwa kwa awamu huku zaidi ya 10% kuliwa na vigogo.
Kuna haja sana sana, uchunguzi ufanyike kwa wahujumu uchumi wote na majambazi haya yalioua watu wengi wasio na hatia.
 
UFAFANUZI.
1/Nadhani unamaanisha Dr.Ferdinand Masao ambaye kwa sasa ni marehemu.

2/Fitna, Chuki, Mizengwe dhidi yake kutoka kwa Baadhi ya Watanzania wakiwemo Madaktari, Maafisa wa wizara ya Afya, viongozi kadhaa kutoka serikali ndiyo vilichangia sana Dr.Masao kufariki. Stress za maisha akipambana kutaka kufanikisha ndoto zake zilipelekea kuugua na kufariki. Alikuwa na ndoto njema sana na pana sana kwa Tanzania, hakuwahi kukata tamaa kabisa.

3/Hakuwahi kuwatendea ubaya wowote watanzania, alitumia Muda wake, Utaalamu wake, Kipaji chake na Juhudi zake binafsi katika kuanzisha Hospitali ya kutibu na upasuaji wa moyo ili huduma hiyo iwepo nchini na watu wasiendelee kupelekwa nje, Lakini alichokumbana nacho, kinatia huzuni sana. Alifanyiwa kila aina ya Fitna, alikosa watu wakumtetea, alisakamwa mpaka basi.

4/Kiukweli kabisa, Tanzania tumeitupa Lulu ya thamani sana, Dr.Masao alikuwa ni lulu tena lulu ya thamani sana. Katika hili laana iko juu ya nchi yetu. Mbegu ya Fitna tuliyoipandikiza itatutafuna mpaka basi. Kila mtaalamu atakayeibuka hapa Tanzania atapigwa vita vibaya sana. Usishangae ya Dr.Mwaka kupigwa vita badala ya kusaidiwa kusonga mbele. Ni mwendelezo ule ule.

Aisee jana kwenye uzi wangu wa 'mimi na ka passo hadi Kigali '.kuna sehemu nilisema Tanzania ni taifa lisilo na mbele wala nyuma. duuh watu ikawauma sana, acha waniandame jana, ukweli utabaki Kuwa ukweli tu kuwa Tanzania ni taifa la ajabu sana, ukiinuka na kuonyesha uzalendo unapigwa vita ikibidi hata kuuawa, sasa hapo kuna mbele na nyuma?
 
Mzungu aliletwa aongoze managemen ya muhimbili wachaga wa muhimbili.muhas na walioko wizara ya afya walimfukuza kama mbwa ona sasa hospitali inavyokufa
 
Aisee jana kwenye uzi wangu wa 'mimi na ka passo hadi Kigali '.kuna sehemu nilisema Tanzania ni taifa lisilo na mbele wala nyuma. duuh watu ikawauma sana, acha waniandame jana, ukweli utabaki Kuwa ukweli tu kuwa Tanzania ni taifa la ajabu sana, ukiinuka na kuonyesha uzalendo unapigwa vita ikibidi hata kuuawa, sasa hapo kuna mbele na nyuma?

mkuu tatzo le2 cc watz ni WANAFIKI XANA yaan unapotaka kufanya k2 cha maendeleo watajfanya kukuunga mkono na kuwa pamoja na ww, subr ukishapata mafanikio ndo utaanza kuziona rangi zao halsi, yaan watz tumejaa unafki kuanzia utosini hadi nyayoni, all in all R.I.P dr. Masau
 
Nimejikuta machozi yananitoka, niliwahi kumpeleka mama yangu pale hospitalini kwake, ndio maana napata shida kuona wapuuzi fulani wakijiita wazalendo!!
UFAFANUZI.
1/Nadhani unamaanisha Dr.Ferdinand Masao ambaye kwa sasa ni marehemu.

2/Fitna, Chuki, Mizengwe dhidi yake kutoka kwa Baadhi ya Watanzania wakiwemo Madaktari, Maafisa wa wizara ya Afya, viongozi kadhaa kutoka serikali ndiyo vilichangia sana Dr.Masao kufariki. Stress za maisha akipambana kutaka kufanikisha ndoto zake zilipelekea kuugua na kufariki. Alikuwa na ndoto njema sana na pana sana kwa Tanzania, hakuwahi kukata tamaa kabisa.

3/Hakuwahi kuwatendea ubaya wowote watanzania, alitumia Muda wake, Utaalamu wake, Kipaji chake na Juhudi zake binafsi katika kuanzisha Hospitali ya kutibu na upasuaji wa moyo ili huduma hiyo iwepo nchini na watu wasiendelee kupelekwa nje, Lakini alichokumbana nacho, kinatia huzuni sana. Alifanyiwa kila aina ya Fitna, alikosa watu wakumtetea, alisakamwa mpaka basi.

4/Kiukweli kabisa, Tanzania tumeitupa Lulu ya thamani sana, Dr.Masao alikuwa ni lulu tena lulu ya thamani sana. Katika hili laana iko juu ya nchi yetu. Mbegu ya Fitna tuliyoipandikiza itatutafuna mpaka basi. Kila mtaalamu atakayeibuka hapa Tanzania atapigwa vita vibaya sana. Usishangae ya Dr.Mwaka kupigwa vita badala ya kusaidiwa kusonga mbele. Ni mwendelezo ule ule.
 
cc mh rais Dkt. magufuli, fuatilia hii issue ya dokta masau
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom