Nini Kiliikuta Jimbo Katoliki la Mbulu!

Nini Kiliikuta Jimbo Katoliki la Mbulu!

Ryzen

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2012
Posts
7,315
Reaction score
8,748
Katika pita pita zangu za JF nilikuta Comment inasema Askofu Hhando wa Jimbo la Mbulu aliwahi Kuwapinga Ma Askofu wenzake katika Kikao Kinaitwa MV Kipalapala Jambo lilipelekea kutengwa na Ma Askofu Wenzake.. Pia Hili lilipelekea Jimbo la Mbulu kutopelekewa Ma Askofu wazawa kwa Kipindi Kirefu mpaka Hapo Majuzi..

Pia katika pitapita zangu Huko Mtandaoni Nikanukuu haya maneno ambayo yana Relation na Hayo Hapo Juu..
Mwaka 1984 kulikuwa na mapendekezo ya kuligawanya jimbo la Mbulu lililokuwa likiongozwa na mhashamu Askofu Nicodemus Hhando kuwa na jimbo lingine kwa upande wa Babati na kadiri ya mapendekezo walidhani Padre Wilbroad angekuwa Askofu wa jimbo hilo lingine, Bahati mbaya au nzuri jimbo halikugawanywa hivyo Wilbroad alibakia kuwa Vicar General wa jimbo la Mbulu akitegemewa kumrithi askofu Hhando, Haikuwa hivyo kukatokea hali ambayo sitaki kuongelea lakini baada Cardinal Pengo kumrithi marehemu Cardinal Rugambwa kulitokea tatizo ambalo hadi leo lipo pale Mbulu, warithi wa Hhando wamekuwa wakitoka nje ya Jimbo la Mbulu!


Je nini Kilitokea Jimbo la Mbulu au Kilifanywa na Jimbo Hilo Mpaka Madai hapo Juu yakatokea..
Kama Kuna Mtu anafahamu vizuri Historia ya Askofu Nicodemus Hhando tafadhali atujuze..

Asanteni!
 
Japo sio mjuzi sana wa hizi nyanja ila sidhani kama kunasheria ndani ya kanisa catholic inayosema askofu wa jimbo fulani lazima awe mzawa, na ndio maana askofu Ruwaich ambaye sasa nadhani ni askofu msaidizi wa jimbo kuu la Dar yey ni mtu wa moshi lakini alishawahi kuwa jimbo la Mbulu, Dodoma, Mwanza na Sasa Dar.
 
Back
Top Bottom