Nini kifanyike ili kuongeza ufanisi wa biashara Tanzania

Mama Joe

JF-Expert Member
Mar 30, 2009
1,504
828
Jamani wajasiriamali wenzangu leo nimeona tujadili hili; Tanzania tuna rasilimali nyingi tu lakini tatizo bado tunaagiza vitu nje hata ambavyo tunazalisha hapa mfano nianzie na wakulima supermarket na hoteli nyingi kubwa unakuta vitu kama nyama, maziwa, mayai, nafaka kama mchele wanaagiza nje. Niliwahi kuuliza hili nikaambiwa watanzania hatuwezi kufanya biashara nao kwani tukiambiwa tenda ya kuku 1000 wenye kg 1.3+ kwa siku tunashindwa mara leo wakubwa sana keshokutwa wadogo, kesho kuku 800 au huna kabisa. Wanasema vivyo kwa nafaka mchele mzuri ila mchafu, packing nk.
Mbaya zaidi hata kwa matumizi ya maduka na manyumbani bado kuna vitu toka nje ambavyo mtu wa Tanzania angeweza kabisa kuzalisha au anazalisha isipokuwa tu packing. Jamani hebu tusaidiane hapa nadhani sio lazima mtu mmoja azalishe kuku 1000 kwa siku, lita 1000 za maziwa au kg 1000 za mchele isipokuwa hakuna network kati ya hawa wafanyabiashara, Naweza kutoa mfano wa nchi jirani Kenya wananunua maziwa yetu fresh wanachanganya na wanayozalisha wao wanafanya packing nzuri wanaleta kuuza Tanzania, wananunua handicrafts kama vinyago, sandals na pochi, vikapu wanaviboresha na kwenda kuuza Ulaya kwa bei juu.
je nini kifanyike ili soko la bidhaa Tanzania likue sio hapa bali nje pia. Kwa walio nje hebu tunaomba tofauti kati ya bidhaa zetu na hizo za wenzetu zikoje mbona kila leo vitu vya nje tu sie tunashindwa wapi? Je bidhaa gani ambayo hapa nyumbani tunaweza kuiza nje hata kwa hawa jirani zetu wa East Africa?
 
Tatizo kubwa la baadhi ya wafanyabiasha (tena walio wengi) katika nchi yetu hii ni kukosa elimu ya ujasiriamali na kufanya biashara in isolation, bila mkakati madhubuti wa kuelimishana kuhusu elimu ya ujasiriamali na kuanzisha networks kamwe hatutofika mbali.,kingine ni udogo wa mitaji yetu, hii inawafanya wafanyabiashara wengi washindwe kuchangamkia opportunities nyingi zilizopo hivyo kuachia wenzetu kutoka nje kuzichukua, hili la mitaji nadhani inabidi mfumo wa utoaji mikopo wa mabenki yetu uangaliwe upya, riba ipunguzwe kuendana na hali halisi na masharti ya mikopo pia yawe nafuu zaidi kuwawezesha hawa wafanyabiashara kupata mikopo.
 
Tatizo kubwa la baadhi ya wafanyabiasha (tena walio wengi) katika nchi yetu hii ni kukosa elimu ya ujasiriamali na kufanya biashara in isolation, bila mkakati madhubuti wa kuelimishana kuhusu elimu ya ujasiriamali na kuanzisha networks kamwe hatutofika mbali.,kingine ni udogo wa mitaji yetu, hii inawafanya wafanyabiashara wengi washindwe kuchangamkia opportunities nyingi zilizopo hivyo kuachia wenzetu kutoka nje kuzichukua, hili la mitaji nadhani inabidi mfumo wa utoaji mikopo wa mabenki yetu uangaliwe upya, riba ipunguzwe kuendana na hali halisi na masharti ya mikopo pia yawe nafuu zaidi kuwawezesha hawa wafanyabiashara kupata mikopo.

Ni kweli hapa na mie naona tatizo ni elimu ndogo bado wafanyabiashara wanonekana ni watu waliokosa ajira au elimu, vijana waliosoma wengi wanataka waajiriwe tu, pili kukosa umoja au mfumo mzuri wa mawasialiano lakini hii pia inachngiwa na ufinyu wa elimu, mitaji midogo pia naona ni tatizo. Wengi tunazalisha ili mradi tu kuganga njaa na sio zaidi ya mahitaji yetu. Ubora wa bidhaa pia ni muhimu.
 
Pia kuna ubinafsi kati ya mkulima na mkulima, au mzalishaji na mwenzie..Kila mmoja anataka atengeneze faida, aile yeye peke yake bila kugawana na mwingine!
Ishu ya kuchanganya teknolojia (merging), ili kupata brands za kisasa zaidi za products na zinazoendana na soko zaidi hapa ni hadithi!
Kwa mtindo huu bado tutaendelea sana kunyanyaswa na wajanja!
 
Kwanza ni kuwahamasisha Watanzania kupenda bidhaa zinazozalishwa kutoka katika viwanda na mashamba yetu na kuachana na bidhaa kutoka Ulaya na Amerika

Pili ambalo ni muhimu ni kwa wazalishaji wa nchini kwetu kuzalisha kwa viwango vya juu na kuuza kwa bei ambayo Watanzania wa madaraja yote wataweza kununua

Tatu ni kwa serikali kuwa makini katika kulinda wazalishaji na walaji wa ndani

Asante Mama Joe kwa mada nzuri na MUNGU akulinde. Amen
 
Pia kuna ubinafsi kati ya mkulima na mkulima, au mzalishaji na mwenzie..Kila mmoja anataka atengeneze faida, aile yeye peke yake bila kugawana na mwingine!
Ishu ya kuchanganya teknolojia (merging), ili kupata brands za kisasa zaidi za products na zinazoendana na soko zaidi hapa ni hadithi!
Kwa mtindo huu bado tutaendelea sana kunyanyaswa na wajanja!
You have said it, kukosa umoja, lakini hii inatokana na hofu ya ushindani ambayo pia ni kukosa elimu, mi nadhani wasomi mnapaswa kuingia katika biashara ili kuipa ufanisi zaidi. Mfano mmoja wa direct graduate wa SUA waliopata award ya Business Plan competition, hawa vijana wameanzisha biashara yao from the scratch na kuingia kwenye mashindano haya wameshinda ni mfano bora wa kujiajiri, umoja na biashara zilizoenda shule. (check BiD network)
 
Kwanza ni kuwahamasisha Watanzania kupenda bidhaa zinazozalishwa kutoka katika viwanda na mashamba yetu na kuachana na bidhaa kutoka Ulaya na Amerika

Pili ambalo ni muhimu ni kwa wazalishaji wa nchini kwetu kuzalisha kwa viwango vya juu na kuuza kwa bei ambayo Watanzania wa madaraja yote wataweza kununua

Tatu ni kwa serikali kuwa makini katika kulinda wazalishaji na walaji wa ndani

Asante Mama Joe kwa mada nzuri na MUNGU akulinde. Amen

Naomba hapo juu kwenye red tutofautiane, sasa hivi kuna utandawazi, huwezi kumlazimisha mtu atumie bidhaa duni iliyozalishwa Tanzania wakati anaweza kupata nyingine nzuri zaidi kutoka Kenya, Uganda au SA acha nchi za ng'ambo.

Hiyo ya viwango hapo sawa kabisa, tunahitaji kuwa wabunifu, tuzalishe sio mradi tu bali tujali ubora, pia uhakika wa bidhaa zetu, sio tukizalisha kidogo tu, tunatanua na kusheherekea tunafunga biashara kwa muda, vitu hivi ndio vinatugharimu kwa kukosa masoko ya uhakika hata hapa nchini ambayo yangepelekea kutangaza bidhaa zetu nje pia.

Kuhusu serikali kwakweli naona kama haina nia kabisa ya kumsaidia mwananchi wa kawaida, kwani Tanzania ndio imejaa kila bidhaa fake, hakuna hata kukagua kama sheria zinafuatwa katika kuagiza. Pili kuna ukandamizaji wa wakulima na wafanyabiashara mfano wakulima huko Rukwa wanaozewa na chakula kisa wamekatazwa kuuza nje na barabara za kupeleka mikoa mingine hazipitiki! Pili wafanyabiashara wa magogo wanasumbuliwa sana na TRA, serikali kiasi kwamba inakatisha tamaa hii pia inawakuta wachimabji wadogo wa madini.
Sasa hawa watu wanaishia kuuza magendo kwa bei duni kwa watu mara nyingi wa nje ambao wanaenda kuuza nje kwa bei kubwa zaidi
Lakini yote haya nadhani kungekuwa na umoja kati yao, na wana elimu ya kujua haki zao na hela ya kuzidai hizo haki basi manyanyaso yangeisha. Its a vicious circle to me........
 
Naomba hapo juu kwenye red tutofautiane, sasa hivi kuna utandawazi, huwezi kumlazimisha mtu atumie bidhaa duni iliyozalishwa Tanzania wakati anaweza kupata nyingine nzuri zaidi kutoka Kenya, Uganda au SA acha nchi za ng'ambo.

Hiyo ya viwango hapo sawa kabisa, tunahitaji kuwa wabunifu, tuzalishe sio mradi tu bali tujali ubora, pia uhakika wa bidhaa zetu, sio tukizalisha kidogo tu, tunatanua na kusheherekea tunafunga biashara kwa muda, vitu hivi ndio vinatugharimu kwa kukosa masoko ya uhakika hata hapa nchini ambayo yangepelekea kutangaza bidhaa zetu nje pia.

Kuhusu serikali kwakweli naona kama haina nia kabisa ya kumsaidia mwananchi wa kawaida, kwani Tanzania ndio imejaa kila bidhaa fake, hakuna hata kukagua kama sheria zinafuatwa katika kuagiza. Pili kuna ukandamizaji wa wakulima na wafanyabiashara mfano wakulima huko Rukwa wanaozewa na chakula kisa wamekatazwa kuuza nje na barabara za kupeleka mikoa mingine hazipitiki! Pili wafanyabiashara wa magogo wanasumbuliwa sana na TRA, serikali kiasi kwamba inakatisha tamaa hii pia inawakuta wachimabji wadogo wa madini.
Sasa hawa watu wanaishia kuuza magendo kwa bei duni kwa watu mara nyingi wa nje ambao wanaenda kuuza nje kwa bei kubwa zaidi
Lakini yote haya nadhani kungekuwa na umoja kati yao, na wana elimu ya kujua haki zao na hela ya kuzidai hizo haki basi manyanyaso yangeisha. Its a vicious circle to me........
Asante kwa changamoto za majibu yako Mama Joe
 
Watanzania wana bidhaa nzuri sana ila tatizo ni packaging na consistency in delivering. Tumeshazoea ubabaishaji, kwahiyo leo unaweza kupata mzigo wa kupeleka kwa mteja kesho ukakosa au ukapata nusu ya mahitaji ya mteja wako.

We should start focusing on long term investment, huo ndio utakuwa mwanzo mzuri wa kuondoa huu ubabaishaji. Ukiwa na matazamio ya biashara yako kukua ni lazima utawork out factors zinazoweza kusababisha biashara yako kufa ambazo kubwa ni consistency in delivering good quality product, with the best packaging! Tukiweza hapo, biashara zetu zita-take off vizuri sana! Angalia juice tunazo nunua, kama Ceres, hebu jaribu kuijaza kwenye mifuko ya plastic ya plastic uone inavyofanana...

Haya majadiliano kila mmoja wetu akayafanyie kazi mahala pake pa biashara yasiishie hapa!
 
Watanzania wana bidhaa nzuri sana ila tatizo ni packaging na consistency in delivering. Tumeshazoea ubabaishaji, kwahiyo leo unaweza kupata mzigo wa kupeleka kwa mteja kesho ukakosa au ukapata nusu ya mahitaji ya mteja wako.

We should start focusing on long term investment, huo ndio utakuwa mwanzo mzuri wa kuondoa huu ubabaishaji. Ukiwa na matazamio ya biashara yako kukua ni lazima utawork out factors zinazoweza kusababisha biashara yako kufa ambazo kubwa ni consistency in delivering good quality product, with the best packaging! Tukiweza hapo, biashara zetu zita-take off vizuri sana! Angalia juice tunazo nunua, kama Ceres, hebu jaribu kuijaza kwenye mifuko ya plastic ya plastic uone inavyofanana...

Haya majadiliano kila mmoja wetu akayafanyie kazi mahala pake pa biashara yasiishie hapa!

Asante sana Kabengwe kwa mchango wako, kwakweli michango hii itatusaidia sana kama tutaiweka kivitendo katika biashara zetu.
 
Kukosa umoja inachangiwa sana na tabia ya wengi wa watu kutokuwa waaminifu!!!!!
 
Mfano nitauliza swali.

Kwa nn vazi rasmi la bunge ni suti? kwa nini vazi lisiwe zisiwe batiki.kama ni lazima vazi la bunge kuwa kuwa suti kwa nn wasiweke kipengele kuwa ziwe zimeshonwa humu nchini. Hii itaongeza ajira kwa mafundi na wabunifu wa nyumbani.

na kwakuona viongozi wetu wankubali nguo za nyumbani naamini na sisi tuwafuata.

serikali iwe mfano kwa kuagiza na kutumia samani (furniture) zilizotengenezwa nchini.

Kwa mawaziri na viongozi kuendelea kutibiwa na madaktari wale wale kabla hawajapata nafasi za juu. Kabla ya kuwa waziri alikuwa anatibiwa na Dr lema baada ya kuwa waziri anatibia na dr patel.

Kuna vitu vingi vya kufanyika lakini serikali iwe driving force sio kwenye sera tu bali hata kuzitekeleza na kuziishi sera wanazotunga.
 
Mfano nitauliza swali.

Kwa nn vazi rasmi la bunge ni suti? kwa nini vazi lisiwe zisiwe batiki.kama ni lazima vazi la bunge kuwa kuwa suti kwa nn wasiweke kipengele kuwa ziwe zimeshonwa humu nchini. Hii itaongeza ajira kwa mafundi na wabunifu wa nyumbani.

na kwakuona viongozi wetu wankubali nguo za nyumbani naamini na sisi tuwafuata.

serikali iwe mfano kwa kuagiza na kutumia samani (furniture) zilizotengenezwa nchini.

Kwa mawaziri na viongozi kuendelea kutibiwa na madaktari wale wale kabla hawajapata nafasi za juu. Kabla ya kuwa waziri alikuwa anatibiwa na Dr lema baada ya kuwa waziri anatibia na dr patel.

Kuna vitu vingi vya kufanyika lakini serikali iwe driving force sio kwenye sera tu bali hata kuzitekeleza na kuziishi sera wanazotunga.
Ni kweli serikali haiko serious katika kutusaidia wananchi lakini juhudi zetu ndizo zitazotufanya tujikomboe, sio kweli kuwa wabunge wote wanavaa nguo za nje, nenda Dodoma wakati wa vikao vya bunge, nakumbuka hawa kina mama wenye majina katika batiki na vitenge fashion nimewakuta kwenye mahoteli mengi tu wanakofikia viongozi wa kitaifa na nguo zao kwa vile ni quality zinauzwa bei tena juu kuliko hata suti za China na zinanunuliwa sana.
Kwanza tuanze wenyewe kwa kutengeneza vitu vyenye ubora, kisha mitaji ili biashara isiwe ya ubabaishaji, tatu umoja ili kukuza na kutafuta soko zuri zaidi.
Nafikiri kiongozi nae ni binadamu kama sie huwezi kumlazimisha anunue kitu chako ili tu kukusaidia aishie kumpa house girl akifika nyumbani!
 
Nafikiri tatizo tulilonalo watanzania kwanza ni ulipuaji, hatuko makini kwa vitu tunavyovifanya, tatizo lingine tunafikiria tunataka faida kubwa, bila kujiuliza au kufikiria namna ya kuzalisha kitu chenye ubora,

mfn wafugaji wa kuku wa nyama kuna baadhi wanawapata kuku wao vindonge vya majira ili wakue haraka na wawe wanono hapa tunaona mtu hazalishi kitu chenye ubora, tena anazalisha kitu kinachaweza kumhadhiri mtumiaji kwa kupenda faida kubwa, hivyo hivyo kwa wafungaji wa kuku wa mayai, siku hizi kiini cha yai ni cheupe, (kwa Mwz mikoa mingine sijui)wakati tunajua kabisa kama kuku akilishwa inavyotakiwa basi kiini cha yai inatakiwa kiwe cha njano.

Kwa wafugaji wa Ng'ombe wa maziwa, wao (baadhi) wanatia maji mengi tu kwenye maziwa, halafu wanaweka mafuta ya Blue band wanajua mtumiaji akiona mafuta yanaelea kwenye maziwa basi anajua ni mazuri! na mifano ni mengi tu, na hii yote inaua soko kwani usipojenga uaminifu kwa mteja wako hasara yake ni kubwa na uwezekano wa kutoaminiwa katika product unazoproduce inaweza kuendelea kizazi mpaka kizazi na mpaka uje urudisha uaminifu wa wateja/watumiaji inaweza kuchukua muda mrefu, matokeo yake tunayaona leo unakuta tunamasupermarket lkn vitu wanaorder kutoka Southafrika, au kwenye Migodi vyakula vyao hutoka southafrika au Europe, na si ajabu hata kwenye mahotel makubwa wanaorder huko huko, na kwa bahati mbaya hakuna nayeliona si viongozi si wafanyabiashara tunaendelea kuzalisha vitu visivyo na viwango, na wakati huu ambapo ulimwengu ni kama nchi moja tutajikuta watoto na wajukuu wetu wanatumia product kutoka nje ya nchi, kwasababu soko letu tunaliua mwenyewe kwa kuzalisha vitu visivyo na ubora.

Nafikiri wakati umefika wafanyabiashara kuwa na umoja, hii itasaidia kubadilishana tipps mbalimbali, kuelimishana namna ya kuzalisha vitu yenye ubora na hapohapo kupata faida, na pia kupanga bei zisisomuumiza mlaji/mtumiji na pia na wao kutengeneza faida, sio kama ilivyo sasa kila mtu ana bei yake na pia .itakuwa rahisi kupata tenders katika sehemu mbalimbali.


Alinda
 
Back
Top Bottom