Nini kifanyike ili kuiokoa CHADEMA?

Nini kifanyike ili kuiokoa CHADEMA?

Ccm sio imara bali ina uimara fake ulio chini ya madaraka ya urais. Kwakuwa ccm imepata mwenyekiti kwa kupitia kofia yake ya urais, anaweza kufanya lolote na asikutane na kikwazo chochote cha ndani. Rais huyu ana chuki na nongwa ya wazi dhidi ya upinzani hasa cdm, hivyo anatumia madaraka yake vibaya kuagiza taasisi zote za kimamlaka kuua upinzani hasa cdm.

Rais huyu anaingilia box la kura, na kuagiza bila hofu kuwa matokeo yawe yale anayoyataka. Hakuna mwananchi mwenye uwezo wa kuhoji, kwani anashurutisha ionekane demokrasia ndio kikwazo cha maendeleo. Wale wote wasiomsujudia wanatekwa, wanabambikiwa kesi, vyombo vya habari vinavyomkosoa vinavyofungiwa. Huo ndio uimara wa ccm. Mtu mjinga tu ndio anaweza kusema ccm ni imara, eti kisa kuna kundi kubwa linajitokeza kugombea uwakilishi. Hilo kundi linajitokeza kama sehemu ya hizi siasa za kishenzi zinazoendelea humu nchini.
Bw. Tindo, Vp shughuli za maendeleo zilizofanyika ambazo ni utekelezaji wa ilani ya CCM. Nazo ni fake? Rais huyu kwa kipindi cha miaka 5 amesimamia tu chuki dhidi ya CDM hakufanya lolote? Nahisi labda wewe ndo utakua na chuki dhidi yake na Serikali anayoiongoza.
 
Mambo yatakuwa mazuri CDM sio chama cha kufa kirahisi, ni chama chenye wapenzi wengi kuliko CCM na kimeenea sana mashinani. Kwa vyovyote kama ccm hawatamzuia Lissu, basi tegemea mtananga wa kufurahisha na kama ACT na vyama vingine vikiungana basi ccm hawana lao.

Haipaswi kuwa ni uamuzi wa CCM Lissu kurejea na kupambana au la.

Hilo linapaswa kuwa ni moja katika hadidu za rejea za mwungano.

Inawezekana kuweka maazimio ya vyama vinavyo matter kumrejesha Lissu salama na kupambana. Hii ni whether CCM wanataka au hawataki.

Mbona Mali wanaelekea kusalimu amri.

Saa ya ukombozi ni sasa nasema rev. Mtikila (rip).
 
CHADEMA wakijifanya wabishi kila chama kitasimamisha mgombea wake na CCM itacheza hii game vizuri kwa kuwapa ACT viti vingi vya ubunge na CHADEMA itapewa viti 3 mpaka 5. Baada ya hapo ACT kinakuwa chama kikuu cha upinzani. Baada ya hapo CCM itaiundia ACT mizengwe ili kizoofike na kukipa ngivu chama kingine.

Wanyinga ndiyo wali wao 😂 😂😂
 
Mambo yatakuwa mazuri CDM sio chama cha kufa kirahisi, ni chama chenye wapenzi wengi kuliko CCM na kimeenea sana mashinani. Kwa vyovyote kama ccm hawatamzuia Lissu, basi tegemea mtananga wa kufurahisha na kama ACT na vyama vingine vikiungana basi ccm hawana lao.


Wakati utaamua! Tuvute subira.
 
CHADEMA wakijifanya wabishi kila chama kitasimamisha mgombea wake na CCM itacheza hii game vizuri kwa kuwapa ACT viti vingi vya ubunge na CHADEMA itapewa viti 3 mpaka 5. Baada ya hapo ACT kinakuwa chama kikuu cha upinzani. Baada ya hapo CCM itaiundia ACT mizengwe ili kizoofike na kukipa ngivu chama kingine.

Wanyinga ndiyo wali wao 😂 😂😂
Ahsante kwa kutushilikisha katika njozi zako bila kukuomba.
 
ACT ni Chama kilichojipanga.angalau kinaweza pata hata wabunge kumi.kuliko nyinyi ufipa na chama chenu mtaambulia wabunge watatu tu.
Wenye mbwa wanajua nguvu ya CDM, wenye mbwa walijiapiza kuwa CDM haitakuwepo kufikia leo..wewe endelea kuota!
 
Hivi mnavyosema CCM inatafuta wa kumfia, unakua upo serious au unafanya utani au akili zinakua zimeruka. Yaani vyama vinavyokufa hamvioni?

Hivi kuna kipindi ambacho CCM imeimarika kuliko sasa? Hivi kuna kipindi ambacho wananchi wamekua na imani na hiki chama kuliko sasa? Hivi hamuoni hatua za maendeleo zilizopigwa mpaka kufikia uchumi wa kati katika awamu hii? Hivi hamuoni lundo la wanachama na viongozi wanaotoka upinzani kuhami CCM? Hivi hamuoni muamko wa watu wa kaliba mbalimbali wanojitokeza kugombea kupitia CCM? Mpaka sasa CDM imefanikiwa kuweka wagombea kwa 5% katika majimbo yote, na wengi wao wamegombea wenyewe hawakua na upinzani. Hakuna waliojitokeza kugombea huko. Mgombea urais wenyewe mwenye ushawishi wa kushindana na JPM hajulikani. Halafu unadiriki kusema CCM inataka kufa. Seriously????!!!
Chama imara ubebwa na sera na sio polisi, maendeleo yeyeto Kama hayabadilishi maisha ya watu huwezi yaita maendeleo,hizo ni propaganda
 
Bw. Tindo, Vp shughuli za maendeleo zilizofanyika ambazo ni utekelezaji wa ilani ya CCM. Nazo ni fake? Rais huyu kwa kipindi cha miaka 5 amesimamia tu chuki dhidi ya CDM hakufanya lolote? Nahisi labda wewe ndo utakua na chuki dhidi yake na Serikali anayoiongoza.

Kwanza ujue shughuli zote za maendeleo hazifanyiki kwa hisani bali ni wajibu. Hata weupe wa Afrika kusini walisimamia maendeleo tena makubwa kuliko ya hapa kwetu, lakini waliendesha chuki kubwa sana ndani ya nchi hiyo. Usitake kujificha kwenye maendeleo yoyote maana maendeleo sio hisani ni wajibu. Ndio maana nasema, serikali hii inashurutisha ionekane demokrasia ni kikwazo cha maendeleo, jambo ambalo sio kweli.
 
Mie i think wacheni kife naturally..wanasiasa wengine wa emerge na vyama vingine vya upinzani viwe strengthern...
 
Salaam Wakuu!!
Kuna maneno wengi yanaongelewa kwamba ACT ilianzishwa ili kuua upinzani ,na kwamba Membe ametumwa na CCM ili kugawanya kira za wapinzani kupitia ACT.

Inawekana kabisa tuhuma hizi zikawa na ukweli ndani yakr,lskini tunkumbuke ya kwamba CCM inatafuta mtu wa kumfia na kuna uwezekano mkubwa ikamfia Magufuli, Kikwete ilinusurika kidogo tu.

ACT ina balance power bara na visiwani yaani inajengeka kwa muonekano wa kitaifa zaidi ni hybrid ya CUF,CHADEMA na CCM. Sass kama CCM muliitengeza ACT ili kuidhofisha CHADEMA basi inaweza kuja kuimeza CCM baada ya hapo ACT na CHADEMA ndiyo watakuwa Democratic and Republican wa Tanzania.

CHADEMA chezeni hii game kwa akili,asimamishwe Membe kupitia ACT kisha achianeni ubunge na udiwani. Ili joka la Kishetani(CCM) tunaliua kidogo kidogo kwa kutumia akili nyingi. Vinginevyo hicho kinachodhsniwa kitatokea kweli,kura zitagawanywa na joka la kijani litaendelea kuwa.

Huu ni mwaka kitia pilipili kwenye kidonda cha Joka la Kijani cha 2015. CCM haiwezi kutawala milele idondoke,na itamfia Magufuli maana ana kibri na hashauriki anajiona ana akili nyingi kuliko CCM wote.
Ccm haijawahi kuimarika kiasi hiki tangu chama kimoja! Hizo zako ni ndoto za alinacha!
 
Kwanza ujue shughuli zote za maendeleo hazifanyiki kwa hisani bali ni wajibu. Hata weupe wa Afrika kusini walisimamia maendeleo tena makubwa kuliko ya hapa kwetu, lakini waliendesha chuki kubwa sana ndani ya nchi hiyo. Usitake kujificha kwenye maendeleo yoyote maana maendeleo sio hisani ni wajibu. Ndio maana nasema, serikali hii inashurutisha ionekane demokrasia ni kikwazo cha maendeleo, jambo ambalo sio kweli.
Hivi unatumi Nini kufikiri? Akili zingine zinakatisha tamaa kabisa hata kuzitekeleza! Eti siyo hisani...kina membe walipokuwa madarakani walishindwaje kuyafanya aliyoweza Magufuli? Mijitu mwingine inachosha mmfyuuuuu!
 
Weka nakala ya utafiti wenu
haaaa,,,we jamaa umenifurahisha sana.eti"weka nakala ya utafiti wenu".
yani unataka niweke ili ujue ni wabunge wepi wa upinzani watajitoa dk za majerui kabla ya tarehe ya uchaguzi?
 
haaaa,,,we jamaa umenifurahisha sana.eti"weka nakala ya utafiti wenu".
yani unataka niweke ili ujue ni wabunge wepi wa upinzani watajitoa dk za majerui kabla ya tarehe ya uchaguzi?
Kumbe hauna kitu, pole kwa kutegemea policcm na ghiliba. Mwaka huu kichwa kitakuuma bure. Mmechokwa.
 
Hivi unatumi Nini kufikiri? Akili zingine zinakatisha tamaa kabisa hata kuzitekeleza! Eti siyo hisani...kina membe walipokuwa madarakani walishindwaje kuyafanya aliyoweza Magufuli? Mijitu mwingine inachosha mmfyuuuuu!

Narudia tena, kutekeleza miradi ya maendeleo ni wajibu wa serikali yoyote maana ndio inayokusanya kodi. Hata serikali ya mkoloni ilitekeleza miradi ya maendeleo. Kina Membe walitekeleza yao, na pale walipochemsha tuliwapa ukweli wao. Magufuli kafanya muujiza gani mpaka apate uhalali wa kutumia madaraka yake kunajisi uchaguzi, au kuua vyama vingine vya siasa asivyovipenda?
 
Kwanza ujue shughuli zote za maendeleo hazifanyiki kwa hisani bali ni wajibu. Hata weupe wa Afrika kusini walisimamia maendeleo tena makubwa kuliko ya hapa kwetu, lakini waliendesha chuki kubwa sana ndani ya nchi hiyo. Usitake kujificha kwenye maendeleo yoyote maana maendeleo sio hisani ni wajibu. Ndio maana nasema, serikali hii inashurutisha ionekane demokrasia ni kikwazo cha maendeleo, jambo ambalo sio kweli.
Ahsante sana. Umeiweka vizuri safi kabisa. Itabidi niwe naku quote ili kuwasaidia waimba mapambio.
 
Naunga mkono hoja 👊🏽👊🏽👊🏽. Isomwe na Zitto kama kusimamisha mgombea mmoja wa upinzani kwenye Urais basi ni Lissu na siyo Membe.

CHADEMA imsimamishe Lisu. ACT kama hawataki kumsapoti Lisu CHADEMA iachane nao. CHADEMA ifocuss kujijenga kwa sasa. Isimamishe wagombea kwa ngazi zote wazawa wa chama, iachane na shortcuts za kusimamisha watu kutoka ccm kisa umaarufu wao. CHADEMA ijiruhusu kukua kwa kutumia wanachama wake wazelendo. Iwe na malengo ya muda mrefu na sio kufocuss kwenye uchaguzi wa mwaka huu tu. Iwe na mikakati ya hata miaka 10 mbele. Nina imani CHADEMA ikiwa na msimamo itakuja kuchukua nchi.
 
Kumbe hauna kitu, pole kwa kutegemea policcm na ghiliba. Mwaka huu kichwa kitakuuma bure. Mmechokwa.
Sawa ila nyinyi komaeni kwenye mitandao.
sisi tunazama kwenye kina cha mkondo wa nungwi mpaka chini kabisa ya bahari ambapo nyinyi hata kwa dawa hamuwezi fika.
 
Back
Top Bottom