Nimemsoma Rostam vizuri sana ktk waraka wake wa kujiuzuru na hakika mwandishi wa hotuba yake ni mzuri na anaijua kazi yake. Pamoja na mapambo mengi jambo moja ambalo lenye ukweli na Rostam kashindwa kuliweka wazi ni pale aliposema kwamba mpango wa Kujivua magamba ulikuwa viongozi wa kamati kuu na sekretariet kujizuru na kumpa nafasi rais kuchagua viongozi wapya...
Lakini ukweli tunaoufahamu ni kwamba Makamu mwenyekiti wa CCM aliwatumia RACHEL barua za kujiuzuru. Haikuwa uvumi wala maneno ya Chiligati na Nnauye bali kamati iliamua na majina haya halitolewa kwenye mkutano wa NEC uliopita ambapo nakumbuka vizuri sana Sophia Simba alijaribu sana kuwatetea. Rostam amefukuzwa na kujiuzuru ilikuwa kufunika kombe mwanafaramu apite lakini Rostam kalifunua..
Sasa napomsoma Rostam kwa madai yake ambayo yanaonyesha wazi kwamba kuna mgawanyiko ndani ya chama na hakika mapokezi ya Rostam yameweka doa kubwa kwa chama tawala sii tu kwa jimbo la Igunga bali mkoa mzima wa Tabora ambao ulituma wajumbe wake toka kila jimbo kumpa mkono wa kwa heri na kionyesha masikitiko yao kwa kuondokewa na Robin hood..
Katika majumuiko ya maswala yote haya najaribu kufikiria hatma ya chama hiki hasa pale watakapo jiuzuru Lowassa na Chenge ambao kati yao nina mashaka makubwa na Lowassa kwa sababu huyu baba kesha jifunza angamizo lake alipojiuzuru kama waziri mkuu na shidhani kama safari hii atakubali kuondoka biila kufukuzwa kama chama kilivyoatoa maagizo..
Na iwapo hawa wote wataondoka, nashindwa kuelewa nguvu ya Jk itatoka wapi ikiwa The brain, financer na wakili wake watajiondoa na kumwacha yeye pekee kama Alpacino ktk mchezo wa Scarface, au Robert DeNero ktk Al Capone! huku akibakiwa na mtu mmoja tu ktk kundi lake la kwanza - mzee Sitta!
Kweli ameweza kuwacheza akili wengi waliotangulia toka baraza lake la kwanza la mawaziri kina Msabah, na watu wake wa karibu sana kama marehemu mzee Ditopile wote wameondoka kwa huzuni achilia mbali wale walioshughulika sana ktk kampeni za kumweka Ikulu na akawaacha solemba kama kina mzee Janguo.
JK atabakia Mpweke huku wimbi kubwa la Upinzani ukidai mambo magumu sana ambayo yalishindikana toka enzi za mwalimu...Miaka minne mizima imebakia kabla ya uchaguzi ujao na JK yuko kiti kikubwa, Sijui ya kesho, Mungu pekee ndiye anajua lakini Uhai wa CCM upo ICU wataweza vipi kupita mtihani huu...
Lakini ukweli tunaoufahamu ni kwamba Makamu mwenyekiti wa CCM aliwatumia RACHEL barua za kujiuzuru. Haikuwa uvumi wala maneno ya Chiligati na Nnauye bali kamati iliamua na majina haya halitolewa kwenye mkutano wa NEC uliopita ambapo nakumbuka vizuri sana Sophia Simba alijaribu sana kuwatetea. Rostam amefukuzwa na kujiuzuru ilikuwa kufunika kombe mwanafaramu apite lakini Rostam kalifunua..
Sasa napomsoma Rostam kwa madai yake ambayo yanaonyesha wazi kwamba kuna mgawanyiko ndani ya chama na hakika mapokezi ya Rostam yameweka doa kubwa kwa chama tawala sii tu kwa jimbo la Igunga bali mkoa mzima wa Tabora ambao ulituma wajumbe wake toka kila jimbo kumpa mkono wa kwa heri na kionyesha masikitiko yao kwa kuondokewa na Robin hood..
Katika majumuiko ya maswala yote haya najaribu kufikiria hatma ya chama hiki hasa pale watakapo jiuzuru Lowassa na Chenge ambao kati yao nina mashaka makubwa na Lowassa kwa sababu huyu baba kesha jifunza angamizo lake alipojiuzuru kama waziri mkuu na shidhani kama safari hii atakubali kuondoka biila kufukuzwa kama chama kilivyoatoa maagizo..
Na iwapo hawa wote wataondoka, nashindwa kuelewa nguvu ya Jk itatoka wapi ikiwa The brain, financer na wakili wake watajiondoa na kumwacha yeye pekee kama Alpacino ktk mchezo wa Scarface, au Robert DeNero ktk Al Capone! huku akibakiwa na mtu mmoja tu ktk kundi lake la kwanza - mzee Sitta!
Kweli ameweza kuwacheza akili wengi waliotangulia toka baraza lake la kwanza la mawaziri kina Msabah, na watu wake wa karibu sana kama marehemu mzee Ditopile wote wameondoka kwa huzuni achilia mbali wale walioshughulika sana ktk kampeni za kumweka Ikulu na akawaacha solemba kama kina mzee Janguo.
JK atabakia Mpweke huku wimbi kubwa la Upinzani ukidai mambo magumu sana ambayo yalishindikana toka enzi za mwalimu...Miaka minne mizima imebakia kabla ya uchaguzi ujao na JK yuko kiti kikubwa, Sijui ya kesho, Mungu pekee ndiye anajua lakini Uhai wa CCM upo ICU wataweza vipi kupita mtihani huu...