Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,620
- 46,259
Mara kadhaa ajali nilizowahi kushuhudia madereva wa vyombo husika vilivyohusika na ajali walikuwa ni watu walio katika hali ya taharuki, hamaki, wanafoka, wanatukana, wanapayuka na mambo mengine ya hovyo kama hiyo.
Hali hii ya taharuki hutokea hata pale dereva husika ndio chanzo dhahiri cha ajali yenyewe, hali hii pia hutokea hata kama ajali yenyewe ni ndogo sana na watu wangeweza kuzungumza kwa uungwana wakaelewana.
Hii hali ya kukosa uungwana kwa madereva wanapokuwa barabarani huchangiwa na nini?
Hali hii ya taharuki hutokea hata pale dereva husika ndio chanzo dhahiri cha ajali yenyewe, hali hii pia hutokea hata kama ajali yenyewe ni ndogo sana na watu wangeweza kuzungumza kwa uungwana wakaelewana.
Hii hali ya kukosa uungwana kwa madereva wanapokuwa barabarani huchangiwa na nini?