GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Kwa Sheria za Tanzania, unaweza kumiliki ardhi lakini sio kilichopo chini ya ardhi kama madini. Ndivyo nijuavyo, labda kama utaratibu umeshabadilika. Inamaanisha kuwa hata ukigundua dhahabu kwenye shamba lako au kiwanja chako, hutaruhusiwa kuchimba mpaka uwe na leseni.
Sasa chukulia ulikuwa unachimba shimo la choo, na ghafla ukakutana na bonge la dhahabu (nugget) kubwa kama kichwa cha ng'ombe, nini utakachopaswa kufanya Kisheria?
1. Kwenda kuripoti Polisi?
2. Kwenda kutoa taarifa wizarani?
3. Kuujulisha uongozi wa Serikali ya Mtaa?
4. Kwenda kuiuza na kisha kuwasilisha TRA stahiki za Serikali?
Ni hatua gani sahihi utakayopsawa kuchukua?
Nani atakuwa mmiliki halali wa hiyo dhahabu?
Ukijimilikisha bila kutoa taarifa Serikalini utakuwa umetenda kosa, hasa ikizingatiwa kuwa umeichimbua bila kutarajia?
Sasa chukulia ulikuwa unachimba shimo la choo, na ghafla ukakutana na bonge la dhahabu (nugget) kubwa kama kichwa cha ng'ombe, nini utakachopaswa kufanya Kisheria?
1. Kwenda kuripoti Polisi?
2. Kwenda kutoa taarifa wizarani?
3. Kuujulisha uongozi wa Serikali ya Mtaa?
4. Kwenda kuiuza na kisha kuwasilisha TRA stahiki za Serikali?
Ni hatua gani sahihi utakayopsawa kuchukua?
Nani atakuwa mmiliki halali wa hiyo dhahabu?
Ukijimilikisha bila kutoa taarifa Serikalini utakuwa umetenda kosa, hasa ikizingatiwa kuwa umeichimbua bila kutarajia?