Ningependa kujua tukio la kuuwawa kwa Mwangosi na Polisi na Kuuwawa kwa muumini wa Sabato kanisani yaliishia wapi? Kuna mengi zaidi.

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Watanzania mara nyingi tunakuwa wepesi sana wa kusahau. Raisi Kikwete akijua huu udhaifu wetu, pale ambapo alipata changamoto kutoka kwa wananchi aliwashauri wateule wake kutojishighulisha na mihemuko ya wananchi, akidai ni mambo ambayo yangepita tu kama upepo.

Kwa mfano, juzijuzi hapa mitandao ya jamii ilikuja juu sana kuhusu tukio la Mkurugenzi wa Halmashauri kutuhumiwa kumpiga kijana risasi ndani ya kanisa. Tukio hili lilikuwa na mhemuko mkubwa iliposemekana Mkurugenzi huyo alikuwa ni mtoto wa dada yake Raisi Magufuli. ILisemekana alikamatwa na kuwekwa ndani. Sasa kama bado yuko ndani sijui na ningependa kujua, ukizingatia kwamba hapa Tanzania kesi za mauaji hazina dhamana.

Pili ni yule askari wa FFU alipowekwa ndani kwa kosa la kumuua mwandishi wa habari, Mwangosi. Je nini ilikuwa hatima ya lile suala? Je askari alikukumiwa?

Nadhani kuna matokeo mengi makubwa ambayo wan JF mnayajua, na ni wengi wangependa kujua yalikuja kuishaje. Kuna kesi nyingi sana za Polisi kuua raia katika vituo vya polisi ambazo tumesikia, lakini hata siku moja hatujasikia mwisho wake, au wauaji kuwajibishwa. Juzi hapa IGP alisema anawajua watekaji wa MO na atawatia ndani baada ya siku tatu. Kimya, na hakuna anaejali. Kuna suala la FFU kupiga watu Ukonga, na hata askari na gari zilizotumika zilijulikana na serikali kuahidi kuchukua hatua kali. Kimya.

Je, serikali imegundua kuwa Watanzania ni wepesi kusahau hivyo hata wauaji huachiwa kwa kuwa hakuna tena anaekumbuka mambo maovu waliyofanya? Watanzania tumekuwa ndondocha kiasi hiki?

Wale ambao ndugu au rafiki zenu walikutwa na masahibu kama hayo na habari ikavuja, tuambieni kama waliohusika walichukuliwa hatua. Wengine tunaambiwa mnalipwa ili yaishe kimya.
 
Usisahau kuandika na kuacha wosia pia make umegusa kwenye uwanja wa wasiojulikana ova
 
Sisi wachangiaji wakutizama tunapenda waje wenye ujuzi wahizi kazi wakupe majibu yaakina Ben saanane maana nahisi umechoka kuishi andika vizuri wosia ukague vizuri naona kama kunamtoto ametendewa vibaya
 
Yule askari aliye muua Mwangosi alihukumiwa kifungo sikumbuki vizuri ni miaka mingapi ila nadhani ni Kama saba hivi. Alihukumiwa mwaka juzi na mahakama kuu Iringa
 
Usisahau kuandika na kuacha wosia pia make umegusa kwenye uwanja wa wasiojulikana ova
Kuna siku mtasikia watu waliotaka kumteka mtu wameuwawa! Ipo siku, wee ngoja tu. Au hao wanaowatuma Wasiojulikana. Kuna watu hapa Tanzania wana hivi vitu wamekaa navyo tu kimya. Ngoja tufikie flash point

1099379
 
FFU aliyee muua mwangosi keshaga hukumiwa muda mrefu
Shukurani kwa taarifa. Natumaini yuko ndani kikweli, maana niliambiwa Tanzania mtu anaweza kuhukumiwa kwenda jela lakini asiende jela hata siku moja.

Ningependa mwandishi mchokozi afuatilie huyu askari yuko gereza gani.
 
Na huyo Daudi Balali tuliyeaminishwa kafia Marekani kwenye utawala wa JK, mbona juzi kwenye kifo cha Mengi tuliona amejitokeza kwenye mitamdao na kuanza kutoa maoni!

Embu liongezee na hili kwenye mada yako, ili wenye uelewa wa haya mambo watuondolee vibanzi machoni.
 
Mkuu hawa watu wasiojulikana anyway tuishie hapa labda pengine unaneno lakusema nikupe wasaa wakuzungumza
Mkuu, gumzo lililopo mjini hapa ni kwamba wasiojulikana ni kikosi maalum kinaongozwa na mkuu wa kanda na ukuu wa kanda ni kivuli tu ndio maana ana bajeti kubwa kuliko wengine na haguswi. Sasa kama hiyo ndio hadithi bado tu ni Wasiojulikana? Hiyo hadithi sijaivujisha mie.
 
Watanzania mara nyingi tunakuwa wepesi sana wa kusahau. Raisi Kikwete akijua huu udhaifu wetu, pale ambapo alipata changamoto kutoka kwa wananchi aliwashauri wateule wake kutojishighulisha na mihemuko ya wananchi, akidai ni mambo ambayo yangepita tu kama upepo.

Kwa mfano, juzijuzi hapa mitandao ya jamii ilikuja juu sana kuhusu tukio la Mkurugenzi wa Halmashauri kutuhumiwa kumpiga kijana risasi ndani ya kanisa. Tukio hili lilikuwa na mhemuko mkubwa iliposemekana Mkurugenzi huyo alikuwa ni mtoto wa dada yake Raisi Magufuli. ILisemekana alikamatwa na kuwekwa ndani. Sasa kama bado yuko ndani sijui na ningependa kujua, ukizingatia kwamba hapa Tanzania kesi za mauaji hazina dhamana.

Pili ni yule askari wa FFU alipowekwa ndani kwa kosa la kumuua mwandishi wa habari, Mwangosi. Je nini ilikuwa hatima ya lile suala? Je askari alikukumiwa?

Nadhani kuna matokeo mengi makubwa ambayo wan JF mnayajua, na ni wengi wangependa kujua yalikuja kuishaje. Kuna kesi nyingi sana za Polisi kuua raia katika vituo vya polisi ambazo tumesikia, lakini hata siku moja hatujasikia mwisho wake, au wauaji kuwajibishwa. Juzi hapa IGP alisema anawajua watekaji wa MO na atawatia ndani baada ya siku tatu. Kimya, na hakuna anaejali. Kuna suala la FFU kupiga watu Ukonga, na hata askari na gari zilizotumika zilijulikana na serikali kuahidi kuchukua hatua kali. Kimya.

Je, serikali imegundua kuwa Watanzania ni wepesi kusahau hivyo hata wauaji huachiwa kwa kuwa hakuna tena anaekumbuka mambo maovu waliyofanya? Watanzania tumekuwa ndondocha kiasi hiki?
Mpaka ULE MWENGE UTAKAPOACHWA KUZUNGUSHWA KWENYE HII NCHI NDO UNDONDOCHA UTAISHA....BILA YA HIVYO....MPK YESU ARUDI....NA AKIRUDI ATABEBA WANA WA NCHI ZOTE SISI ATATUACHA..
 
Na huyo Daudi Balali tuliyeaminishwa kafia Marekani kwenye utawala wa JK, mbona juzi kwenye kifo cha Mengi tuliona amejitokeza kwenye mitamdao na kuanza kutoa maoni!

Embu liongezee na hili kwenye mada yako, ili wenye uelewa wa haya mambo watuondolee vibanzi machoni.
Hahaha! Mkuu, yaani hizo simu mlinyang'anywa kwenye huo msiba? Hata msimpige picha huyo Balali?
 
Shukurani kwa taarifa. Natumaini yuko ndani kikweli, maana niliambiwa Tanzania mtu anaweza kuhukumiwa kwenda jela lakini asiende jela hata siku moja.

Ningependa mwandishi mchokozi afuatilie huyu askari yuko gereza gani.
Kweli kabisa, kuna jamaa yupo huku mtaan kwetu, alikuwa na bonge la kesi l, tukajua jamaa hato rudi kitaan, lakini hivi sasa jamaa yupo na anafanya yke.

Ninasikia alihukumiwa lakn baada ya miezi kadhaa akaachiwa na faili lake linasema jamaa alishakufa ilhali jamaa yupo mitaa.
 
Unataka majibu gani wakati kesi zote zipo mahakamani,pia unapozungumzia suala la askari kuua raia usisahau pia matukio mbalimbali ya askari kuuawa,vituo vya polisi kuvamiwa na baadhi ya adkari kuuawa na watuhumiwa kukamatwa na kupelekwa mahakamani,inaonekana mtoa post mtazamo wako ni kwamba askari kuuawa ni haki yao.
 
Back
Top Bottom