Ningemshangaa sana Mungu

Ningemshangaa sana Mungu

Ndugu zangu kwa muda nimekuwa nikijiuliza hivi kweli Mungu yupo? Ni kwa sababu naona muda unavyokwenda binadamu wanaigeuza dunia watakavyo, wanaenda tofauti na kusudi lake mwenyezi.

Mfano wako wanaooana wanaume kwa wanaume, wanawake kwa wanawake, wapo wanaonyanyasa wenzao, wapo wanaoua wenzao kwa namna mbalimbali, wapo wasioheshimu utu wa mwanadamu wengine wanatukana watu wazima hadharani tena bila kujali kuwa hawa watu wazima wana wake watoto, wajukuu wanaowaheshimu sana, kuvunjiana heshima, sasa tunabaguana wenyewe kwa wenyewe mfano ikitokea raisi akawa msukuma basi viongozi wote wa serikali.

Vitengo na seksheni mbalimbali watakuwa wasukuma. Watu wanajijengea mahekalu, ranchi za kustarehe kana kwamba hicho ndicho watanzania wamewatuma kuwafanyia. Hakuna namna mungu angetuacha tuendelee hivi, lazima angeshusha gharika. Nina wasiwasi corona inaweza kuwa ishara ya gharika lijalo siku si nyingi tusipojirekebisha
Imefikia hatua hadi binadamu wanaoana na wanyama na cheti wanapewa na Serikali!

Acha atushughulikie kidogo kidogo tutaelewa tu uwepo wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom