Ningemshangaa sana Mungu

Ningemshangaa sana Mungu

MANILABHONA

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2015
Posts
462
Reaction score
351
Ndugu zangu kwa muda nimekuwa nikijiuliza hivi kweli Mungu yupo? Ni kwa sababu naona muda unavyokwenda binadamu wanaigeuza dunia watakavyo, wanaenda tofauti na kusudi lake mwenyezi.

Mfano wako wanaooana wanaume kwa wanaume, wanawake kwa wanawake, wapo wanaonyanyasa wenzao, wapo wanaoua wenzao kwa namna mbalimbali, wapo wasioheshimu utu wa mwanadamu wengine wanatukana watu wazima hadharani tena bila kujali kuwa hawa watu wazima wana wake watoto, wajukuu wanaowaheshimu sana, kuvunjiana heshima, sasa tunabaguana wenyewe kwa wenyewe mfano ikitokea raisi akawa msukuma basi viongozi wote wa serikali.

Vitengo na seksheni mbalimbali watakuwa wasukuma. Watu wanajijengea mahekalu, ranchi za kustarehe kana kwamba hicho ndicho watanzania wamewatuma kuwafanyia. Hakuna namna mungu angetuacha tuendelee hivi, lazima angeshusha gharika. Nina wasiwasi corona inaweza kuwa ishara ya gharika lijalo siku si nyingi tusipojirekebisha
 
Kuna wakati Mungu alijilaumu kwa nini alimuumba mwanadamu na kukiri kuwa hataweza kushindana nae na kuamua kumfutilia mbali juu ya uso wa dunia. Kaleta garika.

Kumbuka mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu, na hapo ndio tatizo linapokuja. Kumbe mwanadamu ni photo copy ya Mungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu ambaye yuko tayari kumuua mtoto wako wa miaka minne asiye na hatia ili akupime imani yako ajue jinsi gani unampenda, Mungu huyo hapaswi kutolewa hata sadaka
 
Daaaa pumzi inakisumbua ndugu yangu,anyway endelea hivyo kumzihaki Mungu ipo siku utakuatana nae

Sent using Jamii Forums mobile app
Elements za uoga hizo

Mungu ndio anakudhihaki wewe, hivi inamake-sense kweli Mungu mwenye sifa ya ujuzi wote na upendo wote ateketeze watoto wasio na hatia kwenye ukoo wa farao ili tu amuoneshe farao kua yeye ni ana nguvu?

Haya baada ha huyo farao kusanda kwanini hakuwarudishia uhainwale watoto aliowaua katika mapigo yale kumi na wakati uwezo wote alikua nao?

Vitabu vyenu ndio vimemdhihaki Mungu

Ila kumbuka Mungu hayupo wala usidate ukadhani namdhalilisha
 
Hakuna jipya chini ya jua.. huwa tunayafanyia maboresho tu kutokana na teknolojia inavyokua ila dhambi ni zile zile tu mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom