Ninatafuta mpenzi/mume nipo serious

Ninatafuta mpenzi/mume nipo serious

Single mom kachoka kuwa single sasa anataka mwenzi wakuzeeka naye... Ujana ule na akina fulani na fulani imefika uzeeni unaweka free entry kwa yeyote
 
Single mom kachoka kuwa single sasa anataka mwenzi wakuzeeka naye... Ujana ule na akina fulani na fulani imefika uzeeni unaweka free entry kwa yeyote
Una uhakika gani kuwa ujana nilikula na akina fulani? Usike kulinganisha kila mtu. Asante.
 
Unaonekana mstaarabu sana dada. Mungu akupe hitaji la moyo wako
Amina ndugu. Mungu akubariki. Watu wajue tu kuwa si kila mtu anakuja hapa kuhadaa au kwa kuwa alishapiga uhuni mitaani akachoka. Hapana mimi si wa hivyo. Nimekuja nikiwa na akili zangu na ninamaanisha na si kwamba nimekosa wanaume wa ku pass time wapo wamejaa tele ila si lengo langu la maisha hapa duniani. Cha msingi umri ninaoutaka wengi wameoa tayari so chances ni chache kupata wasioa/wataliki/wagani hivyo nimejiongeza kupitia JF. Mungu ndiyo anaijua historia yangu basi.
 
Moja ya tangazo lililokamilika kabisa, na hii inaonyesha jinsi ulivyo serious,kila la kheri dada.
 
Bibie hapa umempata mume wala usiwe na wasiwasi vigezo vyote ninanvyo isipokuwa kimoja tu siju kama utakichulia kama kikwazo kwangu mimi naona ni changamoto za kimaisha tukishirikiana tutaweza kuvuka daraja pasipo madhara.

Nishaowa nina mke na watoto wawili nipo tayari kuongeza mke wa pili,je upo tayari kuruka hichi kikwazo kiduchu kweli kweli.
 
Bibie hapa umempata mume wala usiwe na wasiwasi vigezo vyote ninanvyo isipokuwa kimoja tu siju kama utakichulia kama kikwazo kwangu mimi naona ni changamoto za kimaisha tukishirikiana tutaweza kuvuka daraja pasipo madhara.

Nishaowa nina mke na watoto wawili nipo tayari kuongeza mke wa pili,je upo tayari kuruka hichi kikwazo kiduchu kweli kweli.
Asante sana. Siko tayari kuwa mke wa Pili au kuwa na mume wa MTU. Ni hivi hata kama dini yako inaruhusu lakini wake zenu inawauma sana. Mpende mkeo usimletee pressure.
 
Nip mim ila sina kila kitu ulicho kisema, wala kazi .
Asante. Kama huna Kazi mwanaume unategemea kuwa kichwa cha Nyumba? Jitahidi uwe na Kazi. Ni fedheha kulelewa na mwanamke kama huna sababu ya ugonjwa au vinginevyo. Epuka umarios.
 
Back
Top Bottom