Ninaomba wana jf tuijadili picha hii.

Ninaomba wana jf tuijadili picha hii.

Mh! Kitendo cha kushi nje ya nchi na kuona wenzetu walivyo makini kwenye kazi zao bado ukaendelea kuwa CCM .......................!!!:angry::frown:
Nakwambia ni kukosa matumaini.Kitabu chako hakikupi matumaini yoyote.Matokeo ovyo,au kozi haina mshiko.Mtu unayejiamini unaweza kufanya mambo yako ya maana na elimu yako bila kumtegemea mtu yeyote au una-credentials za kuajirika huwezi kufanya huu upuzi.
Ni aibu kwa elimu yao.Huko Urusi nako bwana wanajiabisha sana.Huu umasikini wote ambao CCM imeturithisha bado huku nje ya nchi tunashindwa hata kuja na mawazo mbadala bado tunaukumbatia uccm na ufisadi(ccm=ufisaidi).Shame on them!..sore loosers!
 
kumbe pesa za walipa kodi zinatumika kukusanya mateja wa pombe na kuwanunulia vodka, na kuparty usiku kucha? kudadeki!
 
Dah! Natamani kweli kuwatukana hawa Manyang'au
Mod's kama vipi anzisheni jukwaa la matusi ili mtu akikereka na jambo akamalizie hasira zake humo...

Anyway, nina imani matusi yangu wameyapata hawa Vibaraka wa CCM wasiojua hata wenyewe wanataka nini.......
 
Anayeweza kuwa na fair comment ni yule aliyekwenda Urusi kwa pesa zake siyo uongee wakati umeenda kwa scholarship za chama. Acheni ukenge na ujuha:bump:
 
wanasherehekea nini na wakati m/kiti wao (t) hana raha na ushindi aliopata?
 
MINALIA NA PICHA YA RAISI TUU! :whoo::crazy:
 
Sijui waligawana vipi hao wanawake manake midume ni mingi na mavodka walokunywa mmmh....au kuna mabwabwa?
 
Waagize nyumbani hata picha mpya ya rais basi! aah!
 
Hawana akili hao watu wa kusamehewa yaani wapo tu hawajui nini cha kufanya hapa duniani.
 
Msihangaike na hao walevi mashabiki wa simba na yanga! Inasikitisha mno kuona wasomi wanaotegemewa kuwa chachu na chimbumko la mabadiliko ya kisiasa Tanzania wanakuwa mashabiki wa vyama! Mtanzania mwenye akili timilifu anajua fika ya kwamba CCM sio chama cha kuleta maendeleo nchi! Kimeingiliwa na majizi na mafisadi papa! Fikiria Jitu kama Mrema la TANROAD liko pale miaka 5 limeliingizia taifa hasara kiasi gani! God knows! Rais mkuu wa nchi yupo anakenua meno tu! Mnasubiri Magufuli aje amuadabishe! Ki barabara cha mandela for almost 5 years kinageuzwa geuzwa tu Rais anakenua meno tu! mpaka aje magufuli?
Halafu nyie na mivodika yenu mnauza sura na kujipendekeza kumpongeza kwa jema lipi?
 
Jamani huu ni upuuzi ambao tumekua tukiipinga ofisi za ubalozi kugeuzwa matawi ya CCM.Mh. Balozi ni kiasi gani cha pesa kilitumika katika sherehe hiyo?Hapo naona sherehe hiyo ilifanyika katika ubalozi wa Tanzania Moscow kwa misingi hipi!!!!?Naona hata ubalozi unashindwa kuelewa mipaka ya kazi ya ubalozi na CCM.Sasa sisi CHADEMA ,CUF,NCCR MAGEUZI N.k tunaweza kufanya hilo katika ofisi ya ubalozi?Hao wana CCM walimpigia kura JK?Ningeliwaelewa kama wangekutana au kuandamana kudai uhuru wa kupiga kura katika ofisi ya ubalozi.Huu ni zaidi ya upuuzi hapa kuna ufisadi,unafiki na kujipendekeza.Wengi walioshiri tafsiri ni kilichopo mezani,sitashangaa hata wengi waliohudhulia hawamfahamu hata Rais.KWAO CHA MUHIMU NI MNUSO.IMEFIKIA WAKATI WA SERIKALI KUPIGA MARUFUKU SHUGHULI ZA VYAMA VYA KISIASA UBALOZINI KAMA WANATAKA WAKODI KUMBI"UBALOZI NI WA WATANZANIA NA SIO WA CCM"MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
IMG_0196.JPG


Na Mwandishi wetu Happy
Katika hali iliyoonekana kuwavutia watanzania wengi waishio nchini Urusi, Tawi la CCM Moscow limefanya sherehe ya kumpongeza Mwenyekiti wa CCM na Raisiwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete kwa ushindi mkubwa alioupata katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni. Sherehe hiyo iliyoanza majira ya saa kumi na moja jioni ya tarehe 27/11 na kumalizika majira ya saa kumi na mbili na nusu asubuhi ya tarehe 28/11 iliwavutia sii tuu watanzania waishio nchini Urusi na Maeneo ya jirani, bali pia natu wengine wasio watanzania.

Miongoni mwa wageni muhimu waalikwa na Capt. Mstaafu Jaka Mwambi ambaye pia aliwahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi Tanzania ikiwemo ukatibu mkuu msaidizi wa CCM Taifa. Mh. Mwambi katika htuba yake kwa wapenzi, wanachama na wakereketwa wa CCM waliohudhuria amesisitiza kuwa vijana sio tuu taifa la kesho, ila pia ni Taifa la Leo na la Keshokutwa. Mh. Mwambi amesema kuwa vijana wasifikirie kuwa kujiunga na chama ni kujinufaisha kifedha, bali ni kukomaa kimawazo na kisiasa na lengo kubwa ni baadae kuwatumikia wananchi na sio wananchi kuwatumikia.

Mwenyekiti wa Tawi la CCM Urusi Dk. Alifred Kamuzora katika hotuba yake alihoji kuwa katika uchaguzi wa hivi karibuni, ambapo wapinzani wanadai matokeo yalichakachuliwa, isije kuwa wenyewe wanaotoa madai hayo ndio waliojichakachua wenyewe. Akisisitiza jambo, Dk. Kamuzora alisema Matokeo ya Uchaguzi kuanzia ya uraisi hadi wabunge na madiwani yalikuwa sio ya ubabaishaji na uchaguzi ulikuwa huru na, salama na Haki, hata taarifa ya waangalizi wa Umoja wa Ulaya, Umoja wa Africana SADC walithibitisha hilo. Aither Dr. Kamuzora alisisitiza kuwa katika kipindi cha mwanzo cha uongozi wa Raisi Kiwete CCM imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutimiza ilani yake ya uchaguzi. Katika kauli mbiu ya CCM ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania, CCM imeweza kuboresha huduma za hospitali, kuongeza shule za msingi, shule za sekondari kwa kila Kata na hata vyuo vikuu nchini vimeongezeka kutokana na sera na Ilani ya CCM.
Mengine ni uboreshaji wa mahakama huru, ambapo watanzania wameshuhudia hata watu waliowahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini wakisimama kizimbani, uboreshwaji wa chombo imara cha dola, jeshi la Polisi, Jeshi la Wananchi, na Jeshi la kujenga Taifa.
Aidha, CCM imeweza kuboresha elimu, maji, umeme, barabara nk. hayo ndio maisha bora yanayozungumzwa.


source: Chama Cha Mapinduzi Tawi la Moscow: Tawi la CCM Moscow Lafanya Sherehe Kumpongeza JK

wanafiki. Hawajui wanachosherehekea. hayo ndiyo matatizo ya wazamiaji, wanatafuta favour ya gov. Iwape posho na sponsorship.
 
isiyokuwasha hujailamba.
kwanza kura tu hamkupiga, sasa sijui hayo mashauo mnayatoa wapi?
Nyie kaeni huko mnywe mipombe mikali kisha muendelee kukuza uchumi wa wenzenu...
 
SOMETIMES YOU WONDER WHERE DID PEOPLE LIKE KAMUZORA GET THEIR PhD FROM
WITH THIS KIND OF THINKING??. HOW DO YOU KNOW THE ELECTION WAS FREE AND FAIR
WITHOUT EVEN TALKING TO VOTERS ??. A PERSON WITH PhD, SHOULDN'T YOU DO A LITTLE RESEARCH INSTEAD OF READING IT ON NEWSPAPERS AND BELEIVE IT AS TRUTH. PLEASE TELL US WHERE DID YOU GET YOUR PhD FROM SO I DON'T SEND MY CHILD TO SUCH SCHOOL. DR. KAMUZORA CAN YOU AT LEAST EXPLAIN HOW DID SLAA GET 40
VOTES FROM KARATU AND AT THE SAME HIS CANDIDATE FOR MP GOT 25,000 VOTES ??.
 
waache kuchonga huko kwenye maabunge yanayofanya kazi. Waje apa bongo kukesha asubuni masaa matatu na jioni matatu kwenye foleni.
 
Back
Top Bottom