Ninaomba msaada katika hili tatizo

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Babu yangu alikuwa Muislamu, alibahatika kupata elimu enzi za Mjerumani,akiwa shule abadili dini na kubatizwa. Alifanya kazi kwenyel serikali ya Wajerumani pia Waingereza.

Alipopata mchumba ilibidi mchumba abadili dini na walifunga ndoa kanisani. Ingawa alikuwa Mkristu, bibi alitufundisha Juzuu tukiwa wadogo. Alifariki akiwa na 100+, kabla mauti kumfika aliomba sana aitiwe Imamu lakini watoto wake Wakristu walimpuuza.

Sasa hivi familia ni kama imegawanyika, binamu zangu wanabadili dini kwa kasi ya umeme. Wengi wanapata wachumba Waislamu. Si wanaume si wanawake.

Sasa hivi hata kwenye misiba hatuli tena kiti moto hata misa ikifanyika wengi wanabaki pembeni.

Ndoa inaweza kufungwa kicserikali ina maana haina dini, sasa msiba usio na dini tutaufanya vipi?
 
Mambo ya dini haya watu wanahitaji kupata utambuzi sana, suala la imani ni kama safari ya kiroho ambayo twaweza kuwa sote twaelekea destiny moja lakini njia za kufikia zinatofautiana simply because we are all unique with difference attitudes, purpose, etc.
Kitendo au matendo ya kulazimisha mfanano katika njia ya kuufikia umilele sio kitu chepesi na hivyo kuleta mikanganyiko.katika jamii
 
Mnahitaji kujitambua na kutambua kuwa kila mmoja wenu anayo haki ya kuchagua imani ipi inamfit kwa mazingira yake na namna yake hivyo mvumiliane na kuheshimiana na kusapotiana katika safari yenu, tunapojaribu kutetea dini ndipo tunakoseana kama ndugu,upendo Wa kindugu na uhalisia Wa kushare damu hauna mbadala bila kujali nani ana amini nini....chukulianeni kama ndugu achaneni na tofauti za kidini mkishirikiana katika yote.
 
Mnahitaji kujitambua na kutambua kuwa kila mmoja wenu anayo haki ya kuchagua imani ipi inamfit kwa mazingira yake na namna yake hivyo mvumiliane na kuheshimiana na kusapotiana katika safari yenu, tunapojaribu kutetea dini ndipo tunakoseana kama ndugu,upendo Wa kindugu na uhalisia Wa kushare damu hauna mbadala bila kujali nani ana amini nini....chukulianeni kama ndugu achaneni na tofauti za kidini mkishirikiana katika yote.
Hili ndiyo lengo letu, ili wote tushiriki ni kheri kuendeleza mila kwenye misiba yetu, akija Imam au padre iwe ni mazishi tu.
 
ohoooo.... jitahidini kujua hizo dini ni ustaarabu na tamaduni za wazungu na waarabu... sisi utamaduni wetu ni kuishi kwa kupendana na siyo dini.... JITAHIDINI MSIJEANZA KUCHINJANA. bibi anastahili sana kulaumiwa kwa kushindwa kujitambua mapema.
 
nyinyi hamna miongoni mwenu mkristo,mkristo anayeasi dini hakuwa mkristo,alikuwa akijiendea tu.

cha msingi kila mmoja aachwe afanye aonavyo inafaa.kama amefariki akiwa anaenda kanisani na akadai azikwe kikristo iwe hivyo,sio mambo ya kukabana marehemu azikwe na imamu ama padri.
 
nyinyi hamna miongoni mwenu mkristo,mkristo anayeasi dini hakuwa mkristo,alikuwa akijiendea tu.

cha msingi kila mmoja aachwe afanye aonavyo inafaa.kama amefariki akiwa anaenda kanisani na akadai azikwe kikristo iwe hivyo,sio mambo ya kukabana marehemu azikwe na imamu ama padri.
 
Babu yangu alikuwa Muislamu, alibahatika kupata elimu enzi za Mjerumani,akiwa shule abadili dini na kubatizwa. Alifanya kazi kwenyel serikali ya Wajerumani pia Waingereza.

Alipopata mchumba ilibidi mchumba abadili dini na walifunga ndoa kanisani. Ingawa alikuwa Mkristu, bibi alitufundisha Juzuu tukiwa wadogo. Alifariki akiwa na 100+, kabla mauti kumfika aliomba sana aitiwe Imamu lakini watoto wake Wakristu wakimpuuza.

Sasa hivi familia ni kama imegawanyika, binamu zangu wanabadili dini kwa kasi ya umeme. Wengi wanapata wachumba Waislamu. Si wanaume si wanawake.

Sasa hivi hata kwenye misiba hatuli tena kiti moto hata misa ikifanyika wengi wanabaki pembeni.

Ndoa inaweza kufungwa kicserikali ina maana haina dini, sasa msiba usio na dini tutaufanya vipi?
Nakumbusha tu. Kwenye hukumu kila binadamu atasimama peke yake na siyo kundi kama familia au ukoo
 
Back
Top Bottom