Ninaanza rasmi mgomo wa kulipa kodi

Ninaanza rasmi mgomo wa kulipa kodi

Kuna siku nilinunua mabati ya mil 4 nikapewa risiti ya 1.5m....zamani nilikua nachukia. Ila kwa haya yanayoendelea namimi silipi. Na siku hizi sina PAYE hata hawanipati shenzi kabisa mapanya buku yamekula 1.5T kimya kimya. Halafu yanaimba ngonjera za uzalendo. To hell.

Sent using my Nokia Torch
Wao wanataka sisi tuwe wazalendo ila wao hawana huo uzalendo. Basi twende hivyo hivyo.
 
... NILISHAACHA KULIPA KODI TANGU ENZI ZA KIKWETE
... KULIPA KODI KWA NCHI KAMA TANZANA NI KUJIDHIHIRISHA KUWA WEWE NI MWEHU.
 
Uzuri ni kwamba wote tunaisoma namba, haina CCM wala upinzani. So tuendelee kupiga makofi
 
Umenikumbusha machungu, leo kuna dogo wamemkamata wameenda nae mnaz mmoja kosa halipi kodi ofis yenyewe hata laki mbili za mtaji haifiki ni saloon kiti elf40 vile vya kuunga, mashine ya kunyolea elf30, kioo 40elf na benchi la kukalia wateja wamemwambia kila mwenye frem lazima alipe kodi na kaambiwa alipe 155400,sasa sijui watampeleka polisi manake wameenda nae,swali langu lipo hapa kama wanaotakiwa kulipa kodi wanatakiwa wawe na mitaji ya ml4 hawa wasiofikisha mitaji hiyo hela zao zinaenda wapi?na kwanini wasifanye hivyo kama sheria yao inavyosema? manake pale hivyo vitu vinahesabika hata kwa kukisia tu unajua hapa hakuna hata laki 3 mbona tunaoneana hivyo?mkuu tuko pamoja sitolipa kodi ya aina yoyote na mengine ntakayofanya najua mwenyewe .

tatizo lugha
Aiseeeees
 
Aisee mtoa mada km una point ktk bandiko lako,nakuunga mkojo mkuu haiwezekana tukawa tunahangaika kulipa kodi halafu kilaza huyu na wenzie wa design yake wanazichezea watakavyo.
tapatalk_1549615604087.jpeg


"Proudly, brought to u by Bachelor Sugu"
 
Asante sana mtoa post wewe ni mimi kabisa................ kodi watakayopata ni ile ya kukatwa kwa lazima PAYE 506,000 kila mwezi.... Inaniuma sana na ndio maana nikiona inachezewa hovyo nakasirika.. MUNGU TUPE UJASIRI
Unalipa Payee shs.506,000/= kwa mwezi! Mara kumi na mbili 506,000×12= !!?????!!!! Wewe si mwenzetu Mungu akulani.
 
Hakuna nchi ya mabeberu inayofanya hivyo,ni stori tu.
Ulipaji wa kodi TZ haupo vizuri,nchi za mabeberu kuna kiwango cha kulipa kodi,ukishavuka hicho kiwango fedha inayozidi unarudishiwa,cha kushangaza TZ,viongozi wenye nyadhifa/vyeo vikubwa ndani ya nchi hawalipi kodi kabisa,mie ngumbaru mchoma mkaa nalipa kodi kubwa kumzidi hata waziri wa serikalini.
 
Ukilipa kodi yote utakufa masikini.😂😂ila wakikudaka jiandae kwenda kula soya..
 
Back
Top Bottom