Nina maumivu makali mno ya jino

Nina maumivu makali mno ya jino

Ungesema pia upo wapi/mji, ili mtu akiwa na ushauri ajue pa kuanzia.
Huku Usukumani nawasikia wakisema wanazo dawa za mitishamba ila sijui kama ni za uhakika........
 
Jino linaniuma mno
Sitaki kung'oa maana nishangoa Moja naogopa mapendo.

Mwenye dawa ya dharula ya jino bila kung'oa aniekezee

Nahitaji uamuzi wa kung'oa kuziba au kung'oa uwe wa mwisho baada ya kila njia kushindikanq
Pole sana.

Kuna kiwango cha jino kuharibika ambapo maumivu yanakuwa makali sana ambapo matibabu yake ni kuling'oa tu.

Ili kuepuka kung'oa jino ni muhimu kufanya uchunguzi wa meno kila baada ya miezi sita ili kuziba au kuchukua hatua mapema kabla ya kufikia hatua ya kung'oa.

Kung'oa jino huacha pengo, hata hivyo bado kuna uwezekano wa kuwekewa jino la bandia ili kuziba pengo la jino lililong'olewa.

Ili kuepuka meno kuharibika ni muhimu kupiga mswaki walau mara mbili kwa siku (asubuhi na jioni) hasa baada ya kupata kifungua kinywa na mara baada ya kula usiku.

Tumia dawa sahihi ya meno unapopiga mswaki, ukinunua dawa ya meno angalia sehemu ya ingredients ambapo kwa mtu mzima dawa sahihi huwa na fluoride 1450ppm na kwa watoto ni 1000ppm.

Pia punguza ulaji au matumizi ya sukari au vyakula/vinywaji vyenye sukari. Epuka kula vyakula au vitu vyenye sukari hasa katikati ya milo.

Kila kheri.
 
Mkuu,naomba fungua thread yako,shuka chini kama unasoma coments,shuka tu mpaka reply thread, shuka chini mpaka kwenye related threads kisha kagua mmoja baada ya mwingine kuna ushauri mzuri mno kwenye threads hizo. Pole na jioni njema.
 
Mkuu,naomba fungua thread yako,shuka chini kama unasoma coments,shuka tu mpaka reply thread, shuka chini mpaka kwenye related threads kisha kagua mmoja baada ya mwingine kuna ushauri mzuri mno kwenye threads hizo. Pole na jioni njema.
 
TIBA YA JINO

1.Ampiclox (Nunua hata za Buku)
2.Prednisolone/Predilone (Nunua hata za buku)
3.Dawa Tatu ( Nunua hata za buku)
4.Hydrogen Peroxide (Mouth Wash) - Hii huuzwa kuanzia Tsh 2500 - 4000


MATUMIZI

1.Kwanza kabla ya kumeza hizo dawa hapo hakikisha unasukutua hiyo dawa ya Hydrogen Peroxide (Mouth wash- Pima vifuniko viwili vya hiyo dawa ya mouth wash halafu iweke mdomoni walau dakika 15 huku ukiwa unasukutua kwa kuzungusha mdomoni,Baada ya hapo iteme usije ukaimeza,Ukishaitema chukua maji masafi sukutua tena hadi mdomo ubaki msafi)

2.Baada ya hilo zoezi la kwanza kufanyika,Anza kutumia hizo dawa nilizokuandkia hapo,Utameza kulingana na ushauri wa daktari

Hizi dawa hapo nimekuandikia ni kiboko ya Jino au meno yanayouma!,Hutuliza na kumaliza kabisa maumivu ndani ya muda mfupi na inabaki historia!
 
TIBA YA JINO

1.Ampiclox (Nunua hata za Buku)
2.Prednisolone/Predilone (Nunua hata za buku)
3.Dawa Tatu ( Nunua hata za buku)
4.Hydrogen Peroxide (Mouth Wash) - Hii huuzwa kuanzia Tsh 2500 - 4000


MATUMIZI

1.Kwanza kabla ya kumeza hizo dawa hapo hakikisha unasukutua hiyo dawa ya Hydrogen Peroxide (Iweke mdomoni walau dakika 15 huku ukiwa unasukutua kwa kuzungusha mdomoni,Baada ya hapo iteme usije ukaimeza,Ukishaitema chukua maji masafi sukutua tena hadi mdomo ubaki msafi)

2.Baada ya hilo zoezi la kwanza kufanyika,Anza kutumia hizo dawa nilizokuandkia hapo,Utameza kulingana na ushauri wa daktari

Hizi dawa hapo nimekuandikia ni kiboko ya Jino au meno yanayouma!,Hutuliza na kumaliza kabisa maumivu ndani ya muda mfupi na inabaki historia!
Asante sana Mkuu
Budget yake ni sh ngap jumla?
 
Watu wamekushauri dawa nyingi mkuu.ila mm nikushauri dawa ya jino ni KUNG'OA tu..mm nshatumiaga dawa zt za kienyeji na za hospital mpk za kichina lkn sikufua dafu kutibu zaidi yakuliondoa.
 
Nenda hospital kama vipi watasafisha na kuliziba au la watauwa mizizi ubaki na jino lako
 
UGORO tu kazi kwishaa hakuna cha jino kuuma tena, mimi mwenyew ndo shuhuda.

nilitumiaga UGORO na tangu mwaka 2018 mpaka leo, sijawahi kuhis maumivu ya jino tena mim yalikua mawili kushoto na kulia.

dawa nilitumia kila aina sijui karafuu, chumvi, majivu, ampricoxy na nyingne za shamba za kusukutua ila zilipoza tu.

nikaja kupona kwa ugoro wa jero tu.

FANYA HIVI
Kama kuna kishimo tafuta pamba au chana kidaso unachoona kinaweza kujaa kweny hicho kishmo cha jino lilipo toboka.

Tandaza pamba/kidaso katikat weka ugoro kidogo na kisha kikunje kidaso ugoro ufunikwe uwe katikati(kifundo).

Hicho kifundo ndan yake ulimo ugoro kipachike kweny shimo la jino.

Fanya hvo ahsubh baada ya kupga mswak unaweka.
Usiku tena unatoa unapga mswak unaweka ugoro mwingne na kidaso/pamba unabadiri kingne.

Siku ya pili tu utaona badiliko, fanya siku 7.

Utasahau hayo maumivu.
Mim vimeshabak vishmo tu. Na nyama natafuniapo
 
Back
Top Bottom