Nina mashaka na utu wa Rais Magufuli

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,088
103,323
21752140_1616072328456755_8325708474094424723_n.jpg


Nimeanza kupata shaka na utu wa Rais Magufuli. Sijui yanakuwa matamshi ya bahati mbaya au makusudi.

Rais anazifanya fikra kwamba kina Manji wanandamwa kwa sababu wana raha zionekane sahihi. Au tuseme kina Mbowe wanahujumiwa miradi yao kwa sababu wana raha? Inaudhi sana.

Tazama watu wamefikia kumtukana Rais mitandaoni kwa sababu ya kauli kama hizi
 
View attachment 592348
Nimeanza kupata shaka na utu wa Rais Magufuli. Sijui yanakuwa matamshi ya bahati mbaya au makusudi.

Rais anazifanya fikra kwamba kina Manji wanandamwa kwa sababu wana raga,zionekane sahihi. Au tuseme kina Mbowe wanahujumiwa miradi yao kwa sababu wana raha? Inaudhi sana. Tazama watu wamefikia kumtukana Rais mitandaoni kwa sababu ya kauli kama hizi
Rais wa nchi anatakiwa afanye kila juhudi ili kila mwananchi aishi kwa raha ya ajabu anavyotaka.

Rais hatakiwi kuwaandamawale waliofanikiwa kuishi kwa raha ya ajabu.

Kuna video moja ya nyumbani kwa mtoto wa Bakhresa inasambazwa. Mzee Bakhressa alipata kufanya kazi sana na Mzee wangu,katikabiashara zao. Kuna siku Mzee wangu alikuwa ananihadithia jinsi Bakhressa alivyotakakufukuzwa benkiUswizi kwa kufikiriwa ni mtu asiyetakiwa kuwa pale katikabenki (kavaa kanzu zake simple anaonekana Muafrikamchafu tu), baada ya kujieleza na kufika kwa meneja na meneja kumtanbuakama mteja wao mwenye mamilioni ya dola hapo, ilibidi meneja aomuombe radhi sana Bakhresa.

Nilivyoona video zile nikasema kuna dhana kwamba pesa zinazovunwa na wazazi humble hutapanywa na watoto ambao hawana hiyohumility,na si ajabu mtu kama Mzee Bakhresa hakupendezewa na kujionyesha kule.Na nikasema, hii humility ya Mzee Bakhressa si tabia nzuri yake binafsi na inayotokana na Uislamu wake safi tu, ni business acumen ukiwa nchi kamaTanzania.

Ukijionyesha tu una ma Rolls Royce kesho serikali inakuona chanzo cha mapato na inakukaba kodi hata ambazo hazipo itakutungia tu.

Ndicho kinachotokea sasa.

Badala ya Rais na serikaliku support wafanyabiashara ili wakuze biashara zao,wakuze ajira na serikaliipate kodi zaidi,serikaliinataka kuandama wafanyabiashara iliiue biashara na kesho ikose kodi kabisa.

Sasa uchumi ukianguka tutashangaa vipi hapo?
 
Magufuli anafanya kazi ili aje aishi kwa raha,na kila mtu anafanya kazi kwa bidii ili baadae uishi kwa raha.
Sasa basi wanaopata raha baada ya kufanya kazi zao yeye analalanaombele kwasababu gani?.
Ok akimaliza Urais atakula kwa raha yote aliochuma leo.Je wakija kulala nae mbele baada ya hapo atasemaje?
 
View attachment 592348

Nimeanza kupata shaka na utu wa Rais Magufuli. Sijui yanakuwa matamshi ya bahati mbaya au makusudi.

Rais anazifanya fikra kwamba kina Manji wanandamwa kwa sababu wana raha zionekane sahihi. Au tuseme kina Mbowe wanahujumiwa miradi yao kwa sababu wana raha? Inaudhi sana.

Tazama watu wamefikia kumtukana Rais mitandaoni kwa sababu ya kauli kama hizi

Acha unafiki ninyi wenyewe mlisema tunataka rais mkali, mkaenda mbali na kusema anatakiwa raisi mwenye maamuzi magumu, amkuishia hapo mkasema tunataka rais ambaye hataangalia sura ya mtu.

Mmekuwa vigeugeu sana. Viva Magufuli Vivaaaaaa!!!!
Na tunamwongezea mika 7 mara 2 = 14 mtameza wembe lazima.
 
View attachment 592348

Nimeanza kupata shaka na utu wa Rais Magufuli. Sijui yanakuwa matamshi ya bahati mbaya au makusudi.

Rais anazifanya fikra kwamba kina Manji wanandamwa kwa sababu wana raha zionekane sahihi. Au tuseme kina Mbowe wanahujumiwa miradi yao kwa sababu wana raha? Inaudhi sana.

Tazama watu wamefikia kumtukana Rais mitandaoni kwa sababu ya kauli kama hizi
Mkuu mleta mada, hapo wanaongelewa wapigaji, mafisadi na wote wa aina hiyo.

Wanaongelewa watu wapenda short cut za maisha, wapenda matanuzi makubwa kwa kutegemea mgongo wa wanyonge.

Ni maneno yanayojikita kwenye vita ya mapambano dhidi ya dhuluma, JPM sio mwanasiasa japo urais ni cheo cha kisiasa.

Kwa miaka miwili aliyokaa ikulu ilitegemewa kuwa awe ameshaanza kuwa na aina ya hotuba tofauti na zile za wakati wa kampeni, lakini kwa sababu sio mwanasiasa anabakia na mtindo wake wa ufikiriaji na uongeaji ambao ni wa kwake na sio wenye kutokana na kuiga tabia za wanasiasa warasimu.
 
Hiv uyu mtu sijui mbaba ana stress gan lakini???

ataishi kambi ya jeshi siku akimaliza madaraka yake ama?

Maana kila siku naona anatukoroga, kwaiyo anataka wenye raha waishi kwa stress? Au kila mwenye hela nchi hii aliibia serikali???

ndo maana anasumbuana na akina manji eee!!

baba huyu ! Sijui ana roho ya aina gani! Ndio maana makato kayaongeza kwenye mishahara, faini hazieleweki!! Rais gani unataka watu wapate shida??

kweli ule msemo jinsi sura ilivyo ndo na roho yamtu iko ivo ivo! Ptuuuuuuu!! Na ashindwe, naomba albadir ya kila mwezi isomwe!

Msintumie nisan nyeupe
 
Back
Top Bottom