warthog gun
JF-Expert Member
- Aug 9, 2018
- 1,466
- 1,256
Nathubutu kusema hivyo kwakua huna ubinadam tumekukosea nini watanzania? Umefanya mambo mengi ambayo wala hujatuuliza sisi watanzania kama tunayahitaji.
Mosi, uko bize kununua hiyo mi mwewe yako kwa kodi zetu tumekwambia tunayahitaji?
Nina mpwa wangu alisoma shule ya msingi yetu yaani ya serikali, secondary amesoma private school, advanced level amesoma shule yetu/serikali, sasa yupo chuo kikuu Dsm mkopo kanyimwa sababu eti ordinary level hakusoma ya serikali, sasa nina maswali ya kukuuliza kama ifuatavyo :-
Mosi, hizo pesa za mikopo kwa ajiri ya wanachuo unatoa mfukoni mwako au ni zetu wananchi?
Mimi nilipomsomesha mpwa wangu private school ina maana nilikupunguzia mzigo kidogo lakini wajibu wako bado upo pale pale wa kusomesha hawa watoto wetu Kwa sababu pesa zinazotumika ni kodi zetu sisi watanzania wala si zako sasa kwanini unakuwa na roho mbaya iliyojaa ukatili namna hiyo? Wewe umetoka kuzimu hakika na kama hujatoka kuzimu basi utakua si mtanzania.
Sasa kulingana na jinsi vyuma vilivyokaza nimekwama kuendelea kulipa Ada ndani ya wiki hii mpwa wangu anarudi nyumbani nina hasira isiyovumilika kodi nalipa kama mtanzania kamili lakini kodi yangu inanunua mitaka taka ambayo wala si kipao mbele chetu.
Mambo ni mengi ya hovyo yanayofanyika katika awamu hii ya tano yaani hasira tu hili limenivuruga na nimevurugwa kweli kweli.
Mosi, uko bize kununua hiyo mi mwewe yako kwa kodi zetu tumekwambia tunayahitaji?
Nina mpwa wangu alisoma shule ya msingi yetu yaani ya serikali, secondary amesoma private school, advanced level amesoma shule yetu/serikali, sasa yupo chuo kikuu Dsm mkopo kanyimwa sababu eti ordinary level hakusoma ya serikali, sasa nina maswali ya kukuuliza kama ifuatavyo :-
Mosi, hizo pesa za mikopo kwa ajiri ya wanachuo unatoa mfukoni mwako au ni zetu wananchi?
Mimi nilipomsomesha mpwa wangu private school ina maana nilikupunguzia mzigo kidogo lakini wajibu wako bado upo pale pale wa kusomesha hawa watoto wetu Kwa sababu pesa zinazotumika ni kodi zetu sisi watanzania wala si zako sasa kwanini unakuwa na roho mbaya iliyojaa ukatili namna hiyo? Wewe umetoka kuzimu hakika na kama hujatoka kuzimu basi utakua si mtanzania.
Sasa kulingana na jinsi vyuma vilivyokaza nimekwama kuendelea kulipa Ada ndani ya wiki hii mpwa wangu anarudi nyumbani nina hasira isiyovumilika kodi nalipa kama mtanzania kamili lakini kodi yangu inanunua mitaka taka ambayo wala si kipao mbele chetu.
Mambo ni mengi ya hovyo yanayofanyika katika awamu hii ya tano yaani hasira tu hili limenivuruga na nimevurugwa kweli kweli.