Nimwambie Ukweli?

Nimwambie Ukweli?

Pole na matatizo yaliyokukuta. Binafsi naona kuwa mtu huyo unamfahamu vizuri tabia yake maana alishaionyesha toka mara ya kwanza mlipokutana lakini ulimpenda na mkaenda mbele zaidi mpaka ukahamia kwake, amekuwa akikukosea kwa kukupiga na kukunyanyasa mara kwa mara kutokana na wivu wa kimapenzi.

Hivyo unatakiwa ujuwe kuwa hiyo ndiyo tabia yake halisi na tabia ni kama ngozi ya mwili huwezi kuibadili (hata kwa mkorogo). Sasa pamoja na yote hayo bado unakili kuwa UNAMPENDA na hujui la kufanya mpaka unatuomba ushauri. mimi nakushauri USIKILIZE MOYO WAKO MAANA UNACHOMPENDEA UNAKIJUA MWENYEWE ila ningekuwa mimi ningeachana naye bila kugeuka nyuma.

HUU NI USHAURI TU. MAAMUZI UNAYO MWENYEWE
 
Kosa kubwa ulilolifanya mara ya kwanza ni kukubali kurudiana nae baada ya kuwatumia ndugu zako kukushawishi.

Utabiri wangu: Kosa kubwa unakaribia kulifanya baada ya kusikiliza moyo wako unataka nini bila kujali kwamba mwili utaumia (mateke na magumi)

Ushauri wangu: Usirudie lile kosa la mwanzo.
 
Achana naye mana mwisho wa siku anaweza kukata shingo alafu ikawa ndo mwisho wako, mbona wanaume tupo wengi mkuu ,ila amini ukipata mwanaume mwingine pia unaweza kuta ana mapungufu fulani aidha ni makubwa au madogo kuliko huyo kurya boy
 
Nahisi ni hadithi ameikopi sehemu akapesti huku!

Upigwe ufungiwe ndani bado upo tu, dada wa mjini tena dsm sijui kama hatakuitia polisi

brain is the beautiful part of the body.
Wewe usiombe kukutana na watu wenye upendo, kuna watu wanaupendo hautafakariki yawezekana ni kweli, ila upendo ni kitu cha ajabu sana
 
Wewe usiombe kukutana na watu wenye upendo, kuna watu wanaupendo hautafakariki yawezekana ni kweli, ila upendo ni kitu cha ajabu sana
Labda, ila mimi nimeshindwa kuunganisha dot pale aliposema alipendwa sana lakini ghafla alivohama akapigwa na kufungiwa ndani!

brain is the beautiful part of the body.
 
Bora hayo... hachelewi kumkeketa kwa kisu...

Mkurya si mtu wa kispotispoti...

Ila kuna watu wengine wanafikiri vichaa ni lazima wawe wanaokota makopo barabarani... Afu wakija kuuliwa watu wanasingizia mapenzi ya Mungu. Mungu kashakupa akili unataka akufundishe namna ya kuitumia?
Na hata kama unapenda mtu hadi unakua huoni unaangalia na hapo unapopenda

Alipaswa ajifunze kumuacha aende

Madame S
 

yaa..nafikiri hii ndo njia sahihi kwani anaonekana anampenda licha ya uwepo wa masumbwi, akija tolewa macho ama kuvunjika mgongo ndipo atajua umuhimu wa kujihami, vile vile vyombo vya sheria vipo stalking ni harassment hyo, kwanini asiende kumshitaki ?
 
yaa..nafikiri hii ndo njia sahihi kwani anaonekana anampenda licha ya uwepo wa masumbwi, akija tolewa macho ama kuvunjika mgongo ndipo atajua umuhimu wa kujihami, vile vile vyombo vya sheria vipo stalking ni harassment hyo, kwanini asiende kumshitaki ?
Anampenda jamani ndio maana amekua mgumu kuchukua maamuzi hayo

Madame S
 
WEWE MWANAMKE NAKUSHAURI USIACHANE NAYE MPAKA AKUTOE JICHO.

HIVI, HUJUI KUWA HAKUNA MKURYA ASIYEPIGA? WAKURYA KUMPIGA MKEWE NDYO MAHABA YAO HAYO.

WEWE UMEVAMIA MTU BILA KUJUA HSTORIA YA KABILA.

JIONGEZE.. SIWEZ KUKUSHAURI UMRUDIE AU KUACHANA KWA 7BU WAKATI MNAANZA MI SKUWEPO.. ILA NDIYO HVYO YANI, WAKURYA NA VIPGO NI KAMA KUNYWA MAJI.. MKUMBUKE binti miss wakati anaweka vgezo vya mume anayemtaka alisema asiwe mtu wa mara.
Mbona Mkurya wangu hapigi?
 
Huyo kaka mpe masharti 1.atafute msaada wa ushauri wa kisaikolojia

2.Abadilike na kuwa mcha Mungu mbali na hapo hatakufaa
 
Back
Top Bottom