Mkami Lum
JF-Expert Member
- Feb 23, 2013
- 414
- 95
Mwajionaje hali ndugu zangu,
Kuna dada mmoja nilitokea kumpenda sana, na nampenda sana mpaka sasa.Mahusiano yetu yalianza kibahati mara baada ya kumsaidia mambo fulani.Nikiwa Tanga yeye akiwa Iringa, aliniambia yeye kapata kazi wilaya moja wapo ya mkoa wa Tanga na akaniambia anapokuja kuripoti ataomba nikampokee na awe mgeni wangu na hapo ndipo nitaanza kulifaidi tunda kwani toka tuanze sijamla nikafurahi kusikia hivyo.
Cha ajabu alipokuja Tanga akaesema kasindikizwa na dada yake hivyo kuonana ni ngumu, akaniomba msamaha kwa kutofanikisha mpango wetu, nami nikamsamehe.Baada ya yeye kuja kuanza kazi rasmi huko wilayani, mimi nikapata kazi Kahama na ikanibidi niondoje tena bila kuonana nae.
Nikiwa kahama amekua akiniomba niende kwake, nikamwambia nasubiria off ndio nitakwenda.Siku zikasogea nikapata off yangu ya wiki mbili, nikamwambia nakuja, akasema wewe njoo mme wangu nipo kwa ajili yako.
Nikiwa safarini (Singida) huku tukiwa tunawasiliana akaniambia ratiba ya kazini kwao imebadilika kwa hiyo wiki hii atakua busy anaona sitafaidi sana...
Ghafla nikaona safari yangu imekua chungu, nikaamua niteremkie hapa dodoma ili nisalimie ndugu.
Usiku wa leo sijalala kwa raha kila nikishtuka namuwaza yeye tu.Kwa hasira nikampigia simu nikamwambia sitaenda tena kwake ila akiwa likizo yeye ndio aje kwangu. Akasema likizo ni mbali, anahamu na mimi sana huku akiwa analia akanisihi niende wiki ijayo.
Kiukweli nimekua simuelewi, ananipenda au ananizuga?
Naombeni mnishauri
Kuna dada mmoja nilitokea kumpenda sana, na nampenda sana mpaka sasa.Mahusiano yetu yalianza kibahati mara baada ya kumsaidia mambo fulani.Nikiwa Tanga yeye akiwa Iringa, aliniambia yeye kapata kazi wilaya moja wapo ya mkoa wa Tanga na akaniambia anapokuja kuripoti ataomba nikampokee na awe mgeni wangu na hapo ndipo nitaanza kulifaidi tunda kwani toka tuanze sijamla nikafurahi kusikia hivyo.
Cha ajabu alipokuja Tanga akaesema kasindikizwa na dada yake hivyo kuonana ni ngumu, akaniomba msamaha kwa kutofanikisha mpango wetu, nami nikamsamehe.Baada ya yeye kuja kuanza kazi rasmi huko wilayani, mimi nikapata kazi Kahama na ikanibidi niondoje tena bila kuonana nae.
Nikiwa kahama amekua akiniomba niende kwake, nikamwambia nasubiria off ndio nitakwenda.Siku zikasogea nikapata off yangu ya wiki mbili, nikamwambia nakuja, akasema wewe njoo mme wangu nipo kwa ajili yako.
Nikiwa safarini (Singida) huku tukiwa tunawasiliana akaniambia ratiba ya kazini kwao imebadilika kwa hiyo wiki hii atakua busy anaona sitafaidi sana...
Ghafla nikaona safari yangu imekua chungu, nikaamua niteremkie hapa dodoma ili nisalimie ndugu.
Usiku wa leo sijalala kwa raha kila nikishtuka namuwaza yeye tu.Kwa hasira nikampigia simu nikamwambia sitaenda tena kwake ila akiwa likizo yeye ndio aje kwangu. Akasema likizo ni mbali, anahamu na mimi sana huku akiwa analia akanisihi niende wiki ijayo.
Kiukweli nimekua simuelewi, ananipenda au ananizuga?
Naombeni mnishauri