MamaBeata
JF-Expert Member
- Apr 15, 2013
- 325
- 112
Mimi ni mwanamke mwenye familia. Ndoa yetu ni changa bado. Hivi karibuni nilipata simu kutoka kwa mfanyakazi mwenzangu alieniomba nimsaidie kukaa na mdogo wake kwa siku tatu ili atafute chumba baada ya hapo angeondoka. Cha ajabu yule mtoto alikaa kwa wiki tatu akidai chumba hajapata ingawa haikua kweli vyumba vilikuepo ila yeye alitaka aendelee kukaa hapa kwangu. Nikamvumilia hadi alipoamua kuondoka na hajaenda kukaa mbali na hapa kwangu. Kilichonikera ni jinsi anavyokuja nyumbani kila mara hasa mida ya menu. Najua dada yake anampa hela ila yeye ananunulia viwalo kama mjuavyo wanachuo akitegemea kuangushia kwa mama Beata. Isitoshe mimi nina bajeti zangu nyumbani kwangu akishakuja yeye kila kitu kinaharibika. Mboga niliopanga iwe ya mchana na jioni itaishia mchana. Kingine akitaka kufua nguo, kuoga anakuja hapa kwangu kitu ambacho naona atanivunjia hata ndoa yangu maana huyu sio ndugu na hashindwi kufanya lolote na mume wangu. Hivi kweli kanikera. Naomba mnipe jibu zuri la kumwambia huyu mtoto asiizoee nyumba yangu mimi nilimkaribisha kwa heshima ya dada yake ila naona mazoea yamezidi wema wangu utaniponza. Mnisaidie wadau. Wasalaam, mama Beata