Halafu wewe bado unajiita Mama mwenye nyumba?. Ukicheka na nyani utaishia kuvuna mabua!.huyo mtu mmoja kila siku Sista? Tena anataka kulala tu asimsaidie msichana wangu wa kazi? Yani humu ndani tumekua wenye nyumba wawili. Kinachonikera hataki mapishi nayoagiza mimi. Mfano chai huwa napenda iweke tea masala anamwambia dada usiweke bwana mi sipendi. Wali tumezoea kuweka iliki ye anasema ya nn usiweke. Mi mtu wa kunipangia maisha yangu kwenye nyumba yangu simtaki hata ukisema mi mchoyo.
Hebu nipm namba yake,mimi nitampa pa kukaa na atakula na kusaza.
Kaizer hilo la mume pia linanipa hofu na wakati mwingine huwa nahisi mume wangu anakosa freedom nyumbani na anakerwa na hali hii. Kwanza hata uvaaji wa huyu mtoto ni wa kimitego anapenda vigaun vifupi na vikaptura. Kumbuka pia yeye sio ndugu. Sina imani kabisa na huyu msichana sijui kwann kaizoea nyumba yangu hivi.
Tatizo wabongo ni kutojiamini. Yaani hapo unajiuliza hivi nikimsema watu (au labda dada yake) watanifiriaje?!! Yaani unawaza watu watakuonaje kama vile huwa mnasaidiana kutafuta hela. Mimi ukinizingua nakupa live na wala sijali watu wanafikiria nini. Wafikirie vyovyote vile wala hainiumizi kichwa.mjasiria nimeomba ushauri nahofu nisije nikawa mbinafsi kupitiliza. Kama binadam nimejiuliza tatizo ni mimi au yeye? Penye wengi hapaharibiki jambo, na nisingependa kuja kujutia uamuzi wangu au niseme kitu ambacho baadae nikaja kujiona mbaya. Si unajua dhamira huwa inasuta wakati mwingine!
Ya Annastacia yepi? Mamndenyi. Kiukweli nahitaji ushauri mi mazoea siyapendi. Kwa nini hela yake atengenezee kucha akitegemea kuja kula kwangu? Hivi hajui maisha magumu au anajitoa ufahamu?
Mimi ni mwanamke mwenye familia. Ndoa yetu ni changa bado. Hivi karibuni nilipata simu kutoka kwa mfanyakazi mwenzangu alieniomba nimsaidie kukaa na mdogo wake kwa siku tatu ili atafute chumba baada ya hapo angeondoka. Cha ajabu yule mtoto alikaa kwa wiki tatu akidai chumba hajapata ingawa haikua kweli vyumba vilikuepo ila yeye alitaka aendelee kukaa hapa kwangu. Nikamvumilia hadi alipoamua kuondoka na hajaenda kukaa mbali na hapa kwangu. Kilichonikera ni jinsi anavyokuja nyumbani kila mara hasa mida ya menu. Najua dada yake anampa hela ila yeye ananunulia viwalo kama mjuavyo wanachuo akitegemea kuangushia kwa mama Beata. Isitoshe mimi nina bajeti zangu nyumbani kwangu akishakuja yeye kila kitu kinaharibika. Mboga niliopanga iwe ya mchana na jioni itaishia mchana. Kingine akitaka kufua nguo, kuoga anakuja hapa kwangu kitu ambacho naona atanivunjia hata ndoa yangu maana huyu sio ndugu na hashindwi kufanya lolote na mume wangu. Hivi kweli kanikera. Naomba mnipe jibu zuri la kumwambia huyu mtoto asiizoee nyumba yangu mimi nilimkaribisha kwa heshima ya dada yake ila naona mazoea yamezidi wema wangu utaniponza. Mnisaidie wadau. Wasalaam, mama Beata
binafsi sijakupenda kivileeee, sijakataa ndoa ni changa ila una katabia kauchoyo kishkaji. usimind mambo ya misosi tunakula na kunyw*. lalamika huna amani atakuibia mume lakini sio msosi. share ya mtu mmoja haiwezi kukuharibia bajet kihivyoooo
Ngoja waje mie naogopa ya anastazia.[/QUOTE]
Yupi huyo? na ndo nani?? dada funguka