Mimi ni mwanamke mwenye familia. Ndoa yetu ni changa bado. Hivi karibuni nilipata simu kutoka kwa mfanyakazi mwenzangu alieniomba nimsaidie kukaa na mdogo wake kwa siku tatu ili atafute chumba baada ya hapo angeondoka. Cha ajabu yule mtoto alikaa kwa wiki tatu akidai chumba hajapata ingawa haikua kweli vyumba vilikuepo ila yeye alitaka aendelee kukaa hapa kwangu. Nikamvumilia hadi alipoamua kuondoka na hajaenda kukaa mbali na hapa kwangu. Kilichonikera ni jinsi anavyokuja nyumbani kila mara hasa mida ya menu. Najua dada yake anampa hela ila yeye ananunulia viwalo kama mjuavyo wanachuo akitegemea kuangushia kwa mama Beata. Isitoshe mimi nina bajeti zangu nyumbani kwangu akishakuja yeye kila kitu kinaharibika. Mboga niliopanga iwe ya mchana na jioni itaishia mchana. Kingine akitaka kufua nguo, kuoga anakuja hapa kwangu kitu ambacho naona atanivunjia hata ndoa yangu maana huyu sio ndugu na hashindwi kufanya lolote na mume wangu. Hivi kweli kanikera. Naomba mnipe jibu zuri la kumwambia huyu mtoto asiizoee nyumba yangu mimi nilimkaribisha kwa heshima ya dada yake ila naona mazoea yamezidi wema wangu utaniponza. Mnisaidie wadau. Wasalaam, mama Beata
mmmh maman beata hata sijui nianzie wapi,
wengi tunakutana na hayo mambo, sio kwa watu baki tu lakini hata kwa ndugu,
ushauri wangu mimi muangalie na tabia yake kwanza kama ni nzuri, halafu mchukulie kama ndugu japo si ndugu
kama ana tabia nzuri sio mbaya akija mara moja moja, atakusaidia espcially kukupatia habari za wadad wa kazi ambao kwa kweli ni majanga
pia anaweza kukusaidia kazi mabali mabli za nyumbani...anapokula mpangi nza kazi kadhaa za kufanya, mfano akija kufua mpe na nguo zenu afue, aoshe vyombo, apike n.k ilimradi mshughulishe...akiona mwenyewe kazi zimemzonga atakata miguu kuja hapo..
siamini kama kweli chakula cha mtu mmoja ni bg issue sana, naaamini chakula cha watu 3 kinatosha wanne...n.k..
mimi kwangu chakula sio issue kama huyo mtu hana tabia mbaya...tatizo ni tabia, wengine utakuta anakukosanisha na wadada wa kazi au anakusema vibaya, au hasaidii kazi yoyote hapo nyumbani..hapo sawa unamuondoa..
nafikiri ungelichukulia in postive way kuliko negative..halafu huyo ni km mdogo wako unatakiwa umkalishe chini umfundishe hasa kama anachzea hela,
sio mbaya kumsaidia mwanafunzi, mdog wa rafiki yako esp kitu km chakula mi naona very minor issue..
kiukweli mi yaani uchoyo uchoyo wa ugali sinaga kabisaaa....tutakula hicho hicho kilichopo hata km ni dagaa...ila akiniboa kwa matabia yake hapo namuondoa ila chakula tu aleeeeee mpk ashibe