Nimezipenda solution za January Makamba kiukweli

Huyu Januari Makamba si mtu wa kuaminika. Uzalendo wake na credibility yake inatia mashaka kwani ni puppet wa Rostam Aziz na Edward Lowassa (DOWANS syndicate). Ni mtu hovyo huyu.
 
Inaonyesha kweli nyie wachache humu JF na nchini kwetu hamjui "uchumi" wala kitu kinaitwa "solution" kamati wanakaa siku 12 kuzungumzia jinsi ya kupunguza megawatts za migodini na kuongeza uzalishaji IPTL kama solutions kwa depth ya tatizo la umeme nchini Tanzania. Kwani Tanesco hawajagundua migodi haiitaji hizo megawatts au kuongeza fedha za mafuta? Kazi ya mkurugenzi wa Tanesco ni nini? au Hii kazi kapewa January pia. Mpaka sasa tunaona wananchi wanaoipenda Tanzania wanapinga Dawans ndani ya Tanesco, they don't want to hear this word anymore. Ufahamu wako wa jambo la umeme katika nchi linaonekana ni finyu sana na mnadanganywa au hamjui la kufanya au ni just political claps. Unajua Tanzania tunahitaji megawatts ngapi kuendesha viwanda mkoa wa Moshi peke yake? Unafahamu megawatts ngapi zinahitajika kuendesha hospitali za mkoa wa Dar? Itakuwa vizuri sana kama hiyo kamati fake ya January wangekuwa wanakutana public ili dialog na wananchi wanaojua in deep solutions za umeme.

Tanzania mpaka leo hii inahitaji at least 800megawatts kucover mahitaji ya wananchi na Taifa zima. Tangu hiki chama kinachojiita ccm waingie madarakani uzalishaji wa umeme umepungua kutoka karibu 300megawatt mpaka kiasi cha kusikitisha maybe 150megawatts. Ufisadi na wizi Tanesco ambako kulitakiwa kusimamia utunzaji wa mabwawa (dams) na kufanya estimates ya uzalishaji wa umeme kupitia mito. Badala yake tangu Nyerere alipojiuzuru na kumwachia Mwinyi, ufisadi ukaingia na Shirika la Umeme Tanzania, Tanesco likageuka kuwa mradi wa ccm na mafisadi wakati wa Mkapa na sasa msanii. Hakuna Mtanzania leo hii hajui haya. Tanesco pamoja na makumpuni mengi ya serikali yakafanyiwa miradi na kukaingizwa something called "contracts", "joint ventures" and "privatization" Huu ndio usingizi Watanzania wamekuwa wamelala na sasa wengi wameamka na taking responsibility kulinda raslimali za Taifa.

Baada ya baba yake kumtafutia mtoto wake January kazi ili waendelee kuwatawala Watanzania, tunamwona mpotofu mwingine January akijifanya anafanya kazi wakati malengo ni kulinda deals za Rostam na mafisadi wengine ndani ya raslimali za Watanzania. Tangu January aingizwa na Makinda kwenye kamati ya nishati na madini tunaona wazi lengo kubwa ni kumlinda Rostam na deals zake na kuhakikisha kwamba Dowans inalipwa na zaidi kuendeleza kulinda siri za vyanzo vya kuharibika kwa Tanesco. Kwanini January asishirikiane na Chadema kuanzisha mjadala Richmond na Dowans ziliingiaje Tanesco na Tanzania? Kwanini January asichunguze hadharani nani mmiliki wa migodi ya Tanzania? This will be a good direction.

Solutions za janga la Umeme Tanzania ni kama ifuatavyo. Kama kweli tunataka kutatua hili swala ni kuleta kwanza "Transparency" na kuvunja kabisa Tanesco na kuunda chombo chenye mwelekeo wa kutatua Matatizo ya umeme. Wananchi wenye professional za engeering na economy waangalie estimates and conducting researches on the real energy capabilities of our country. Vitu vingine ni jinsi ya kufanya energy investments kwa ajili ya long-term solution. Hizi solutions za January, Rostam na Kikwete ni majanga makubwa sio solutions, wanachokifanya ni kufungua milango ya kuibia Taifa letu hakuna jipya hapa.


Sisi kama Watanzania tuangalie pembeni na kusonga mbele kubadilisha hii serikali ya Kikwete na ccm. Mapinduzi yameshaanza na tunamaliza kazi siku chache zimebaki kwa hiyo January na Kikwete jiandeani kuishi kwa mlo mmoja kama Watanzania mnao watesa.​
Well said. Inaonekana huyu jamaa kapelekwa pale kwa kazi moja tuu, kulinda maslahi ya RA kwenye umeme na madini. Toka achaguliwe yeye na DOWANS! DOWANS mpaka amejisahau anaongea kama vile ndio serikali.

Tumemshtukia.
 
Hmmmmmm! solution indeed?

Kuamuru kuwashwa mitambo ya dowans. Hivi hikamati ina maslahi yanani
Wamesahau swala la dowams lipo mahakamani? Na chaajabu Raisi aliwaamuru tanesco watafute mitambo
Ya kukodi . Sas tufutelipi lamakamba ama laraisi na je makamba hajui swala
Lakuingia mkataba na dowans nikinyume na sheria? Minafikiri kamati inge shauri na si
Kuamuru , kama wana amuru kuna maslai binafsi
 
Jamani.. hakuna mtu au chombo kinachoweza kutangaza "dharura" nchini isipokuwa Rais. Kamati ya Bunge haina madaraka hayo na hili tulimkatalia Waziri Mkuu Lowassa alipoingilia kati suala hili hili kwa kudai "dharura". Mengine wanaweza kuyatoa mapendekezo lakini la kutuambia hatua ichukuliwe kwa sababu ni 'dharura' haina hoja. Haijawahi kutangazwa wakati wowote na Rais kuwa Tanzania iko katika dharura kiasi cha kulazimisha kupindisha sheria au kuchukua "extra ordinary" measures.
Kama ni rais wa kutangaza sijui,kama ni makamba mi sijui.
(shairi lako nimelikubali)
 
Hivi kamati za bunge zina mamlaka makubwa namna hiyo....mbona kamati nyingine hatuzisikii au hazijapewa meno kama hii ambayo mwenyekiti wake anaonekana kuwa na sauti hata ya kumzidi waziri wa wizara husika. Au mwenyekiti wa kamati ya bunge yuko juu kimaamuzi zaidi ya waziri? Confusing!

Mkeshaji, swali lako murua sana sina uhakika kama limejibiwa kama bado angalia kanuni za kudumu za bunge 2007 zinavyosema:

9.-(1) Majukumu ya Kamati ya Kudumu ya sekta yatakuwa
yafuatayo:
-
(a) kushughulikia bajeti ya Wizara inazozisimamia;

(b) kushughulikia Miswada ya Sheria na Mikataba inayopendekezwa kuridhiwa na Bunge iliyo chini ya Wizara inazozisimamia;

(c) kushughulikia Taarifa za kila mwaka za utendaji za Wizara hizo;

(d) kufuatilia utekelezaji unaofanywa na Wizara hizo kwa mujibu wa Ibara ya 65(3) (b) (sic)ya Katiba.

Ibara ya 63 (3) (b) ya katiba inasema:

(3) Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge laweza–

(a) kumuuliza Waziri yeyote swali lolote kuhusu mambo ya umma katika Jamhuri ya Muungano ambayo yako katika wajibu wake;

(b) kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa bajeti;

Kwa kweli Januari inaelekea hajui mipaka ya kamati yake kisheria na kikatiba, Bodi ya Tanesco ni legelege na usiyojua madaraka yake kama sheria ya kuanzisha tanesco inavyosema na menejimenti ni dhaifu mnio kwa kuburuzwa hovyohovyo tu. Si ajabu wanaogopa kuwa wakikataa watafukuzwa kazi.

Mimi naona huu ndio wakati muafaka wa kufukuza bodi na menejimenti ya Tanesco kwa kushindwa kufanya kazi na badala yake kazi zao kufanywa na mamluki Januari.
 
Matatizo yote yanaikumba TANESCO yanasababsishwa na shirika hilo kuingiliwa kiutendaji. Sasa Management inaona ni vyema kiuzia migodi umeme kwa sababu inapata pesa kamili za 125 MW tofauti na huku viwandani ambako mita zote zimechezewa ili kuonyesha umeme unaotumika ni kidogo kuliko unoingia, hivyo shirika kupata mapato kiduchu.

Mtakumbuka ile issue ya TANESCO na kiwanda cha Cement Tanga ambapo Dr Rashid alitaka kujiuzulu kama kiwanda hicho kitarejeshewa umeme kwa maagizo kutoka ngazi za juu baada ya kukamatwa wakiiba umeme.

Hivyo kitendo cha Kamati ya Januari Makamba kuifundisha management na apte umeme na nani aispate hakikubaliki hata kidogo na kitadhooifisha mapato ya shirika hilo. Naomba management ya TANESCO iachiwe iuze umeme wake kule wanapopaata mapato.
 
Migodi ndo wanaingizia TANESCO mapato makubwa kuliko makampuni mengine na sitashangaa kusikia kwamba wana mikataba inayowalinda wasikatiwe umeme.

Fumbo mfumbi mjinga mwelevu ataling'amua
 
Mimi huwa najiuliza sana kuhusu Tanesco. Kwa uelewa wangu, tanesco inapaswa kujiendesha (self sustainable) kama mradi kwa sababu huo umeme wanaozalisha tunaulipia. Pamoja na madeni wanayodai kwa wateja lakini bado wana nafasi ya kujiendesha kabisa. Iwapo wanhitaji kujipanua nadhani wanatakiwa kutafuta vyanzo vya finances kama miradi mingine inavyofanya. Kwa hali ninavyoiona ni kwamba huu mradi haulipi na ndiyo maana hauishi migogoro na matatizo tunayoyaona. Hivi inawezekana vipi tangu enzi hizo wameshindwa kutosheleza mahitaji ya umeme kwa walau 50%? Yaani haiingii akilini kabisa. Pamoja na kwamba hii ni "public good" lakini haikupaswa kuwa kama ilivyo sasa.
Mie wanachonishangaza hawa watu wa tanesco ni kuendelea kutumia "traditional and conversional" sources ya nishati ya umeme (maji na mafuta). Matumizi ya gesi bado hayaonyeshi tija japo kuna njia zingine kama zile za kutumia upepo. Nashindwa kabisa kuelewa hivi huyo CEO na mainjinia kibao huwa wanafanya nini huko tanesco?
Kwa kweli inachosha na kukera sana
 
sadly jamaa ana brag mtaani kwamba mitambo ya dowans inawashwa j3 na hamna kitu cha kufanya, anasema umeme utawaka siku nzima. hii inanishangaza kwa ajili dowans ni 100mw na wakati upungufu ni more than 500mw
 
KAMATI ya Nishati na Madini imeamuru kuwashwa mara moja kwa mitambo ya kuzalisha umeme ya Kampuni ya Dowans ili kupunguza tatizo la mgawo wa umeme.
Hatua hiyo ni kati ya maazimio na mapendekezo 30 yaliyofikiwa na kamati hiyo na huku ikisisitiza kuwa iwapo serikali itayatekeleza kwa haraka itasaidia kuiondoa nchi katika athari za kiuchumi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa kikao cha kamati hiyo kilichofanyika kwa muda wa siku 12, Mwenyekiti wa kamati hiyo na Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba (CCM), alisema kutokana na mitambo hiyo kuwepo nchini ni muhimu serikali iiwashe mara moja ili kuepukana na matatizo ya kiuchumi.
Alisema mapendekezo yaliyotolewa ni yale ya dharura, ya kati na ya muda mrefu ambapo katika moja ya mapendekezo ya dharura, kamati hiyo inataka kupunguzwe megawati 125 zinazotumika katika migodi 4 ya madini ili umeme huo uelekezwe kwa matumizi ya wananchi.
Makamba alisema migodi hiyo haijawahi kuathiriwa na tatizo la umeme hivyo kwa sasa inatakiwa ipunguziwe megawatts 50 na kusisitiza kuwa hatua hiyo inaweza kufanyika hata sasa.
“Katika migodi hiyo hawajawahi kujua wala kuonja makali ya mgawo hivyo serikali ikiamua kulitekeleza hilo linawezekana hata leo hili megawat hizo zikafidie maeneo yenye mapungufu,” alisema.
Alisema mbali na hiyo pia serikali inatakiwa kuhakikisha inatoa mafuta ya kutosha katika mitambo ya kuzalisha umeme ya IPTL ambapo hadi sasa inazalisha kati ya megawat 10 hadi 50 huku ikiwa na uwezo wa kuzalisha megawat zaidi ya 80 hadi 90.
Alieleza kuwa iwapo serikali itashindwa kutekeleza mapendekezo hayo kuna uwezekano wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kupoteza kiasi cha sh bilioni 840 iwapo mgawo huo utaendelea katika kipindi cha mwaka huu.
Alisema mapato ya taifa yamepungua kwa asilimia tano ya pato la taifa ambayo ni sawa na dola bilioni 1.1.
“Mapendekezo na maazimio tuliyotoa ni yale ya kati, dharura na ya muda mrefu na iwapo serikali itatekeleza mapendekezo hayo basi tatizo la umeme litaisha katika kipindi cha wiki moja,” alieleza.
SOURCE:TANZANIA DAIMA

Another bogus politicians at work, hawa wanatuletea upupu tu hapa, tumechoshwa na hawa vilaza wa kufikiri.
 
Inaonyesha kweli nyie wachache humu JF na nchini kwetu hamjui "uchumi" wala kitu kinaitwa "solution" kamati wanakaa siku 12 kuzungumzia jinsi ya kupunguza megawatts za migodini na kuongeza uzalishaji IPTL kama solutions kwa depth ya tatizo la umeme nchini Tanzania. Kwani Tanesco hawajagundua migodi haiitaji hizo megawatts au kuongeza fedha za mafuta? Kazi ya mkurugenzi wa Tanesco ni nini? au Hii kazi kapewa January pia. Mpaka sasa tunaona wananchi wanaoipenda Tanzania wanapinga Dawans ndani ya Tanesco, they don't want to hear this word anymore. Ufahamu wako wa jambo la umeme katika nchi linaonekana ni finyu sana na mnadanganywa au hamjui la kufanya au ni just political claps. Unajua Tanzania tunahitaji megawatts ngapi kuendesha viwanda mkoa wa Moshi peke yake? Unafahamu megawatts ngapi zinahitajika kuendesha hospitali za mkoa wa Dar? Itakuwa vizuri sana kama hiyo kamati fake ya January wangekuwa wanakutana public ili dialog na wananchi wanaojua in deep solutions za umeme.

Tanzania mpaka leo hii inahitaji at least 800megawatts kucover mahitaji ya wananchi na Taifa zima. Tangu hiki chama kinachojiita ccm waingie madarakani uzalishaji wa umeme umepungua kutoka karibu 300megawatt mpaka kiasi cha kusikitisha maybe 150megawatts. Ufisadi na wizi Tanesco ambako kulitakiwa kusimamia utunzaji wa mabwawa (dams) na kufanya estimates ya uzalishaji wa umeme kupitia mito. Badala yake tangu Nyerere alipojiuzuru na kumwachia Mwinyi, ufisadi ukaingia na Shirika la Umeme Tanzania, Tanesco likageuka kuwa mradi wa ccm na mafisadi wakati wa Mkapa na sasa msanii. Hakuna Mtanzania leo hii hajui haya. Tanesco pamoja na makumpuni mengi ya serikali yakafanyiwa miradi na kukaingizwa something called "contracts", "joint ventures" and "privatization" Huu ndio usingizi Watanzania wamekuwa wamelala na sasa wengi wameamka na taking responsibility kulinda raslimali za Taifa.

Baada ya baba yake kumtafutia mtoto wake January kazi ili waendelee kuwatawala Watanzania, tunamwona mpotofu mwingine January akijifanya anafanya kazi wakati malengo ni kulinda deals za Rostam na mafisadi wengine ndani ya raslimali za Watanzania. Tangu January aingizwa na Makinda kwenye kamati ya nishati na madini tunaona wazi lengo kubwa ni kumlinda Rostam na deals zake na kuhakikisha kwamba Dowans inalipwa na zaidi kuendeleza kulinda siri za vyanzo vya kuharibika kwa Tanesco. Kwanini January asishirikiane na Chadema kuanzisha mjadala Richmond na Dowans ziliingiaje Tanesco na Tanzania? Kwanini January asichunguze hadharani nani mmiliki wa migodi ya Tanzania? This will be a good direction.

Solutions za janga la Umeme Tanzania ni kama ifuatavyo. Kama kweli tunataka kutatua hili swala ni kuleta kwanza "Transparency" na kuvunja kabisa Tanesco na kuunda chombo chenye mwelekeo wa kutatua Matatizo ya umeme. Wananchi wenye professional za engeering na economy waangalie estimates and conducting researches on the real energy capabilities of our country. Vitu vingine ni jinsi ya kufanya energy investments kwa ajili ya long-term solution. Hizi solutions za January, Rostam na Kikwete ni majanga makubwa sio solutions, wanachokifanya ni kufungua milango ya kuibia Taifa letu hakuna jipya hapa.

Sisi kama Watanzania tuangalie pembeni na kusonga mbele kubadilisha hii serikali ya Kikwete na ccm. Mapinduzi yameshaanza na tunamaliza kazi siku chache zimebaki kwa hiyo January na Kikwete jiandeani kuishi kwa mlo mmoja kama Watanzania mnao watesa.​

Nimeikubali analysis yako. I like thinkers like you!
 
Matatizo yote yanaikumba TANESCO yanasababsishwa na shirika hilo kuingiliwa kiutendaji. Sasa Management inaona ni vyema kiuzia migodi umeme kwa sababu inapata pesa kamili za 125 MW tofauti na huku viwandani ambako mita zote zimechezewa ili kuonyesha umeme unaotumika ni kidogo kuliko unoingia, hivyo shirika kupata mapato kiduchu.

Mtakumbuka ile issue ya TANESCO na kiwanda cha Cement Tanga ambapo Dr Rashid alitaka kujiuzulu kama kiwanda hicho kitarejeshewa umeme kwa maagizo kutoka ngazi za juu baada ya kukamatwa wakiiba umeme.

Hivyo kitendo cha Kamati ya Januari Makamba kuifundisha management na apte umeme na nani aispate hakikubaliki hata kidogo na kitadhooifisha mapato ya shirika hilo. Naomba management ya TANESCO iachiwe iuze umeme wake kule wanapopaata mapato.
kuna watu kibao wana iba umeme na wafanya kazi wanajua lakini kwa kuwa hii nchi imekaa kifisadi fisadi tu ndiyo maana wasoma mita hupewa 2000 kwa mwezi wana kaa kimya, nijukumu lao Management ya Tanesco kujipanga na kuzibiti hali hiyo na wakiamua hawashindwi....kwenye nyekundu sikubaliani na wewe kabisa hawawezi kuashiwa wafanye watakalo wakati wananchi wanaumia, kamaleo TANESCO ukiwaruhusu wafanye huu ujinga kesho kuna shirika lingine litafanyi hivyo hivyi kama tunavyoona kwenye bidhaa kila mfanya biashara akijisikia kupandisha beianafanya hivyo matokeo yake tuna yao...gas, mafuta nk
 
namkubali january makamba, I wish yeye ndiyo angekuwa waziri na ngeleja angebaki mbunge.

Makamba Januari hana lolote analojua KUHUSU UMEME. He is just a politician. Huyu amekuwa planted na JK,RA na EL.
Anachoongea hapa ni siasa tu,hakutakuwa na solution yoyote hapo. Hivi you people mnafikiri Tanesco Engineers wanaweza kuwa hawajui kuwa kwenye hiyo migodi unaenda umeme Megawati ngapi na wazigawanye vipi???Mpaka Januari Makamba ndo aje kuwafundisha kazi TANESCO wakati hajui hata Calculation moja ya namna ya kupata hiyo MW 1?????

Inachekesha kweli kweli. Mimi nilishasema several times kwenye JF kuwa TATIZO KUBWA TULILO NALO WATANZANIA HIZI NYAZIFA ZA UWAZIRI HAWAPEWI PROFESSIONALS! Ilitakiwa Waziri wa NIshati na Madini awe Engineer aliyebobea kwenye UMEME, a doctor or Professor in that field. Ngeleja alikuwa MWANASHERIA wa Vodacom kabla hajaingia kwenye siasa!!!What do you expect from him???

Januri Makamba ni mhitumi wa shahada ya KUSULUHISHA MIGOGORO YA WAKIMBIZI. Halafu watu wanategemea atoe ufumbuzi wa tatizo la umeme. Never,he won't. He is as bogus as anybody in CCM.
 
Well said. Inaonekana huyu jamaa kapelekwa pale kwa kazi moja tuu, kulinda maslahi ya RA kwenye umeme na madini. Toka achaguliwe yeye na DOWANS! DOWANS mpaka amejisahau anaongea kama vile ndio serikali.

Tumemshtukia.

Mbona hajaongelea uwiano wa ukusanyaji kodi migodini kwenye Corporate tax na PAYE tax.January hana uwezo wa kuongelea vitu technical ambavyo ni beneficial kwa nchi.Ni bingwa wa kuongelea vitu vya kitapeli/ kisanii zaidi kama DOWANS.


Makamba hajui kwamba kuna watanganyika wamehamishwa maeneo ya machimbo na hadi leo hawajalipwa?

Je hajui kwamba kuna ajenda imelala ya wawekezaji huko Mara kutiririsha maji yenye sumu mto mara NA WATANGANYIKA HAWAJAFIDIWA????

hUYU mAKAMBA KWANZA NCHI HAIJUI hajui matatizo yanayowakabili watanganyika leo nakuja na hoja nyepesi ya DOWANS, hoja mabayo majibu yake yako kwenye riport ya Mwakyembe.Huyu anatusanii anakula posho bure tu

Amekuja na mradi wa posho za vikao vya kamati yake.Watanganyika kama hamjui huyu kabuni mradi, ina maana kila wakati wankutana na wanlipana posho.Nina uhakika hadi mwisho wa mwaka kamati ya NISHATI NA MADINI itakuwa imetumia peasa nyingi za walipa kodi kutokana na vikao kwa kisingizio cha DHARURA PROJECT
Mdogo wangu MNYIKA zinduka bomu hilo litawalipukia la posho


 
Whatever it is kaka!
Kuna wadau wameuliza vitu vya msingi sana,kwa mfano nani anapaswa atangaze dharura?katiba na sheria zinasemaje?kama kamati how comes wanakuja na solution za dharura wakati anayepaswa kutoa tamko la dharura hajasema?

Lakini tujiulize kwa hizo hizo solution za "dharura" ni kweli Tanesco wameshindwa kabisa kuziona hizo mpaka hiyo kamati ikae na kuwaonyesha?kuna Electrical engineers waliobobea pale Tanesco wameshindwa kabisa kuyaona hayo?inatia shaka kidogo kujumlisha nayooote haya yaliyotokea toka RICHMOND to DOWANS (na mgogoro unaoendelea kuhusu hilo deni mpaka sasa),lakini pia huyo February Makamba kuingia kwake kwenye kamati hiyo na ukaribu wake na wale wanatuhumiwa kwenye DOWANS kwa yeyote yule lazima impe mashaka..labda kama wewe mwenzetu unaishi nje ya TANZANIA.


Sidhani kama TANESCO wana uhuru wa kuamua chochote kuhusu mustakabali wa shirika kimkakati wala kibiashara. Maamuzi yote yako kwa vigogo walioko CCM-CC. Hakuna shirika la umeme la taifa hapo; wao wameamua ni sehemu ya ulaji na ufujaji tu - hata serikali nayo haioni taabu kutolipa deni la TANESCO labda kama kuna maslahi binafsi (Net Group Solution). Kuna wanaopendekeza TANESCO ivunjwe na kuundwa upya. Jawabu ni kuivunja CCM kwanza (na kuiunda upya kwa wanaotaka idumu) ndipo tuweze kushughulikia sekta ya umeme inavyostahili. Wao wanasema "kujivua gamba" lakini sina imani kama wanaweza kuendesha "mapinduzi ya kweli" kuondoa tabaka la mafia linalokinyonga chama na uchumi wa taifa taratiib na kwa uhakika zaidi.
 
Mara nyingi huwa najiuliza hivi kweli sisi Watanzania tuna akili ama tunatumia zaidi hisia kama wanyama. Ikiwa leo tumeshindwa kuendesha shirika la reli mbovu toka mjarumani yenye gharama ndogo kabisa ktk kufanyia ukarabati tutaweza kweli kuendesha reli ya kasi inayotumia umeme?..Na kama tunashindwa kuzalisha umeme wetu wenye uwezo wa mega 3,000 tukizalisha asilimia 15 tu kwa sababu tumeshindwa kukarabati hizo dams (cheapest of them all) Je, tutaweza kukarabati haya malengo mengine ambayo tunayapanga!

Kwa fikra hizi za kina Makamba ndio maana JK kasema Nyerere kaiacha nchi maskini kwa maana kwamba utajiri wa nchi ni fedha zilizoko benki sio rasilimali na maliaasili zake... Ama kweli naogopa kusomea uchumi chuo kikuuu UDSM.

Haya ebu turudi nyuma kuifikiria hiyo Dowans, ni kiwango gani cha umeme wa dharura tunaouhitaji leo, sii chgini ya mega 200 hao Dowans wanaweza kuzalisha mega 35 hadi 100 kama wataongezea mitambo mingine... sasa kuna ulazima gani wa kuwasha hii mitambo yenye utata mkubwa ya ufisadi halitukijua fika kwamba shida ya umeme haitakwisha na mgao lazima uendelee..

Jamani, jamani tukumbuke kwamba Dowans ni kampuni hewa ambayo wameiunda haoa hao viongozi baada ya kula fedha za wafadhili wakijua wamepiga bao..Hawana pa kuipeleka na ndio maana bado imefungwa wakitafuta njia.. Sasa mimi nasema hivi kama wao ni waungwana na maadam mitambo imeshaletwa nchini na hawawezi kuitupa baharini waiwashe pasipo kumlipa mtu kwani hakuna wa kumlipa. generator hiyo tumepewa buree msaada baada ya baadhi viongozi wetu kwenda Houston na kulia na manispaa ya jiji hilo..

Nawaomba sana wakazi wa Marekani na hasa Houston, fuatilieni kwa ukaribu hizi generator zimenunuliwa wapi na kwa kiasi gani hata mtaupata ukweli wanaojaribu kuuficha...Bomba la gas kwenda Mwanza nilisema nani atapewa?...Haya nambieni leo hii ni nani CEO wa shirika linalopewa jukumu la mradi huo..

Niliwahi kusema Bush baba kanunua Kigamboni na anataka kuwekeza watu wakabisha sana, wakaja na gear za udini na chuki kwa sababu ambazo mimi sizielewi, sasa nadhani mnayakubali maneno yangu. Hivyo tafuteni kwa undani hilo shirika linalotaka kuwekeza Kigamboni mji mpya na tafuteni wenye hisa kubwa kisha turudi hapa tuzungumze zaidi...Na bado, Kiwila pia kuna mpya ambayo kauziwa mhndi ambaye katafuta mwekezaji kuficha uchafu uliotokea.. Haya yote hamyaoni na kuyachoka jamani?
 
Naungana na wewe Niweze. naamini kuna mapendekezo mengi ambao wataalamu binafsi(enegy consultants wa nje na wa ndani) walishafanya utafiti na kupendekeza short, medium amd long plan solution kwa tatizo letu hili la umeme. Tatizo liliopo ni utekelezaji na uvivu wa kuamua wa serikali yetu iliyopo madarakani.
Mara zote vipaumbele vyetu ni vya zima moto na kwa maslahi ya Ki CCM zaidi na hasa matumbo yya wakubwa wenye ulafi usiokuwa ma maana.
Mikataba mingi iliingiwa ili kujustfy tatizo na kutoa mianya ya kupata ulaji. hapo ndipo kwenye Tatizo? Taifa Makini haliwezi kuniambia kuwa Kamati ya siku 12 ya January[ sipendi kumwita makamba kwani napata kichefuchefu kwa jina hilo) tena isiyokuwa na wataalamu kwamba imekuja na mapendekezo ya solution ya umeme Tanzania.
Kweli kwenye vipofu hata mwenye makengeza anakuwa mtawala!!!!

Sasa tupo kwenye lindi lililotakana na kudharau Taaluma kwa muda mrefu na Tuna mgao ! zaidi tunaongozwa na serikali ile ile isioona. Nafikiri dawa sio kususia mtindo walioutumia kupata ulaji ili nasi tupone kidogo! Bora Nusu Shari kuliko Shari kamili! . Twende nao kama wanavyotaka ili Umeme kidogo urudi kwenye mtandao.hii itasaidia uchumi usiporomoke zaidi na kunusuru asilimia karibu 4 ya watanzania ambao kipato chao kwa namna moja ama nyingine kinategemea kuwepo kwa umeme.

Tusipokubali hilo basi tusisubiri watu hawa wakae mpaka miaka mitano iishe maana hali itakuwa mbaya zaidi. Tuwangoe sasa na tuweke watu makini watakaoeshimu utaalamu.
Ahsante
 
Back
Top Bottom