Nimezipenda solution za January Makamba kiukweli

Nimezipenda solution za January Makamba kiukweli

Acha kukurupuka. Kamati imetoa mapendekezo kibao. Na kama umesoma hiyo article kuna mapendekezo ya sasa, kati, na muda mrefu. ie long term plan. Article ya Tanzania Daima imeweka only one pendekezo which is a short term. Subiri hapa hapa, in one day or two, InshaAllah---u will read the whole kamati report then utoe dukuduku lako. And I guarantee you, those are solutions to fix umeme.

Muulizeni Mnyika, yeye alikuwemo kwenye hivyo vikao.

Whatever it is kaka!
Kuna wadau wameuliza vitu vya msingi sana,kwa mfano nani anapaswa atangaze dharura?katiba na sheria zinasemaje?kama kamati how comes wanakuja na solution za dharura wakati anayepaswa kutoa tamko la dharura hajasema?

Lakini tujiulize kwa hizo hizo solution za "dharura" ni kweli Tanesco wameshindwa kabisa kuziona hizo mpaka hiyo kamati ikae na kuwaonyesha?kuna Electrical engineers waliobobea pale Tanesco wameshindwa kabisa kuyaona hayo?inatia shaka kidogo kujumlisha nayooote haya yaliyotokea toka RICHMOND to DOWANS (na mgogoro unaoendelea kuhusu hilo deni mpaka sasa),lakini pia huyo February Makamba kuingia kwake kwenye kamati hiyo na ukaribu wake na wale wanatuhumiwa kwenye DOWANS kwa yeyote yule lazima impe mashaka..labda kama wewe mwenzetu unaishi nje ya TANZANIA.

 
And u listen to Mbowe, Regia Mtema, Slaa, Sugu, Lema??

Mnyika ni member wa kamati na kamati haiwezi kutoa recommendations without a consensus. Haya ni matakwa ya Kamati sio January Makamba. Maybe ya can't hear me because you are unwilling to listen and your idolatry to Chadema is probably plugging your masikio.

kwenye hiyo kamati majority ni ccm hata mnyika akipinga haitasaidia,besides,mnyika alishatoa msimamo wake kuhusu dowans,hajawahi kusema tanesco wakodishe mitambo ya dowans na huo ndio msimamo wa chadema xcept zitto ambaye ana damu ya akina makamba
 
Kimsingi sikubaliani na dharura hakuna umeme ulijulikana utakosekana dharura ni jambo la ghafla hili linaumri wa mtoto wa std one siyo wala siioni hiyo dharura .
Pili utawashaje mitambo ya dowans wkt shauri liko mahakamani huko ni kuingilia uhuru wa mahakama kwa lengo la kutaka tz iamrishwe kulipa deni haiitaji Phd kubaini hila za makamba ktk hili kwa nini analazimisha kuwashwa kwa mitambo yenye kesi????????;(
 
namkubali january makamba, I wish yeye ndiyo angekuwa waziri na ngeleja angebaki mbunge.
 
The thing is, our MPs have something of interest in the so called "dowans". dharura maanake nini? kwanini sasa ivi? Have you solved the existing problems of contract breach between dowans and the government? sasa mnawasha ili iweje?
 
Tatizo, hakuna watanzania wazalendo, wanaotupenda kwa ukweli. Nani hajui kuwa mwenyekiti wa hiyo kamati anainterest na iyo so called dowans? The days are numbered, iko siku.
 
Kwanini huko nyuma makampuni ya madini hayajawahi kukatiwa umeme wakati wa Tanzania wamekuwa wakipata adha hii miaka nenda rudi?
umeona eeehh mzeee mkulima, hata mimi najiuliza sijapata jibu.Nini kinaendelea nchi hii na hawa jamaa wa madini na report iliyotoka juzi kwenye ukaguzi zinaonyesha wanalipa na hela haifiki inapotakiwa, nazidi kuchanganyikiwa tu.
 
Ningeiheshimu hiyo kamati kama ingeiamuru serikali kuwawajibisha watendaji wazembe mara moja ikiwa ni pamoja na hao waliotufikisha kwenye dowans, acheni blabla hatujalala mtauwawa bure
 
Kwa nini wataalamu wetu wa masual ya nishati wako kimya na kuwaachia wanasiasa kuchukua nafasi zao? Watushauri ni njia ipi mbadala wa Dowans inafaa kwa muda huu. Nahisi kamati hailijui hili labda. Mimi nimepata hii information hapa CumminsPower.com Website Search
 
Cummins in Africa
When a severe drought reduced Kenya's hydroelectric power to a
trickle, the versatility of Cummins Power Generation was admirably
demonstrated when 39 Rental Power units were relocated from
Ghana to Kenya-on the other side of Africa-in just 12 weeks.
 
Cummins in Africa


When a severe drought reduced Kenya’s hydroelectric power to a
trickle, the versatility of Cummins Power Generation was admirably
demonstrated when 39 Rental Power units were relocated from

Ghana to Kenya—on the other side of Africa—in just 12 weeks.
 
ongeeni na mtoe bla bla zote kama watakuwa wamevunja kanuni za nchi kwa kuingilia madaraka ya tanesco au wizara watanzania hatutaki kujua tunachohitaji umeme. kama makampuni ya madini yatapunguziwa umeme ili sisi tuweze kuishi kama zamani kwetu ni neema hatutaki kujua kama makamba na kamati yake wameingilia madaraka ya raisi au ya waziri mkuuu tunachohitaji ni umeme procedure baadae period.
 
Inaonyesha kweli nyie wachache humu JF na nchini kwetu hamjui "uchumi" wala kitu kinaitwa "solution" kamati wanakaa siku 12 kuzungumzia jinsi ya kupunguza megawatts za migodini na kuongeza uzalishaji IPTL kama solutions kwa depth ya tatizo la umeme nchini Tanzania. Kwani Tanesco hawajagundua migodi haiitaji hizo megawatts au kuongeza fedha za mafuta? Kazi ya mkurugenzi wa Tanesco ni nini? au Hii kazi kapewa January pia. Mpaka sasa tunaona wananchi wanaoipenda Tanzania wanapinga Dawans ndani ya Tanesco, they don't want to hear this word anymore.
TATIZO LA WANASIASA WETU NI KUJIFANYA WANAJUA KILA KITU KULIKO WENYE TAALUMA YAO!



Taaluma Bongo?.....acha kutuyeyusha wewe. Hao unaowaita wataalam walikuwepo wapi miaka hii sita iliyopita?
 
Kiutawala (Administrative) kuwauzia wateja watatu 50 MW ni biashara nzuri sana kuliko kuziuza hizo MW kwa wateja 10,000. Solutions siyo kuziondoa hizo 50 MW toka migodini na kuzisambaza kwa wateja 10,000 bali kutumia rasilimali zilizopo kuongeza uzalishaji. Kwa uelewa wangu mdogo Wilaya zenye matumizi madogo ya umeme zingeondolewa kwa muda kwenye Grid ya Taifa na badala yake wawe na Genereta za kuhudumia Wilaya zao. Umeme ulioko kwenye Grid ya Taifa kwa kipindi hiki wote uelekezwe kwenye majiji na wilaya ambazo ni kitovu cha uchumi wa nchi kama DSM, Arusha, Mwanza, Morogoro, Mbeya, Tanga ili kunusuru viwanda vyetu. Maeneo ya burudani kama Bagamoyo yanaweza kujiendesha kwa Genereta bila kuathiri mapato yao
 
ongeeni na mtoe bla bla zote kama watakuwa wamevunja kanuni za nchi kwa kuingilia madaraka ya tanesco au wizara watanzania hatutaki kujua tunachohitaji umeme. kama makampuni ya madini yatapunguziwa umeme ili sisi tuweze kuishi kama zamani kwetu ni neema hatutaki kujua kama makamba na kamati yake wameingilia madaraka ya raisi au ya waziri mkuuu tunachohitaji ni umeme procedure baadae period.

Hutojali gharama za kuupata umeme huo? Hujui kuwa inawezekana kabisa kuwa tatizo limepikwa ili maslahi ya watu yatimie? Cummins Power Rentals(http://www.cumminspower.com/www/literature/brochures/F-1600CPRGlobalBrochure-en.pdf) wanaweza kuleta hata 2000MW ndani ya wiki 12(mgao umeanza toka Desemba ambazo ndio hizo wiki 12) kwa bei nafuu zaidi. Watawala hawaangalii kwingine zaidi ya Dowans?
 
Dowans deal is DOA ( Dead on Arrival). Kwa hiyo solution ya dowans naomba isizungumziwe sababu inaprove upumbavu na ujinga wetu sote watanzania kwa pamoja. Wao dowans walipoiba deal ya Richmond walileta mitambo TZ ndani ya 6 months, lakini viongozi wetu wa siasa wakiongozwa na JK wanasema mitambo inachukua muda mrefu kupatikana... REALLY????

Yaani matapeli wameweza kuleta mitambo lakini since 2006, JK na Serikali pamoja na lawama zote na ikijulikna demand kwa mwaka inakuwa almost 100MW, wameweza kuongeza less than 20MW per yr kwenye grid?? Nyingine ni story za kuyumba kwa uchumi duniani, wakati in Reality kuyumba kwa uchumi duniani ndio plus kwa wanunuzi wa Generators sababu makampuni yakuuza yana generators zilizokuwa ordered ambazo wanunuzi hawana hela.

Solution tunasema kila siku hapa since 2007, SERIKALI iende GE/Wartsila watoe order ya generators za 200MW ASAP na 100MW gas generators kwa 2012, 2013, 2014, hiyo ndio solution, lakini tupo hapa na mark my words leo March 2011, mpaka march 2012 kutakuwa hakuna NET MW hata moja itakayoongezwa kwenye grid na huku matumizi ya umeme yanakuwa 100MW ++ per yr.
 
Back
Top Bottom