Nimezipenda solution za January Makamba kiukweli

Nimezipenda solution za January Makamba kiukweli

Hivi nyie mnaoilidiscuss neno DHARURA mna maana gani?.....mnataka kuniambia hamuoni DHARURA yoyote katika nchi hii?....ni sawa kabisa kwenu kuona mgao wa umeme unaendelea?......kwa hiyo nyie DHARURA ni mpaka mkwere aseme?.......:A S 13:
 
ongeeni na mtoe bla bla zote kama watakuwa wamevunja kanuni za nchi kwa kuingilia madaraka ya tanesco au wizara watanzania hatutaki kujua tunachohitaji umeme. kama makampuni ya madini yatapunguziwa umeme ili sisi tuweze kuishi kama zamani kwetu ni neema hatutaki kujua kama makamba na kamati yake wameingilia madaraka ya raisi au ya waziri mkuuu tunachohitaji ni umeme procedure baadae period.

Hizo red hapo ndicho kikubwa ambacho mafisadi waliopo katika issue hii wnakitaka.
Wanataka watanzania wapate umeme kwa kutumia mitambo ile ya kifisadi ili muone umuhimu wa mikataba ile na mfunge midomo yenu ili wao waendelee kula kiulaiini.
Naona wamefanikiwa kwako. inasikitisha mno.
 
Hizo red hapo ndicho kikubwa ambacho mafisadi waliopo katika issue hii wnakitaka.
Wanataka watanzania wapate umeme kwa kutumia mitambo ile ya kifisadi ili muone umuhimu wa mikataba ile na mfunge midomo yenu ili wao waendelee kula kiulaiini.
Naona wamefanikiwa kwako. inasikitisha mno.

Ni kweli kabisa....gridi ina upungufu wa 200MW+ hiyo Dowans itatoa less than 100MW bado gap lipo.....kwa nini hatutafuti makampuni makubwa kama General Electric,Cummins etc badal ya makampuni haya yasiyoeleweka?
 
Hivi nyie mnaoilidiscuss neno DHARURA mna maana gani?.....mnataka kuniambia hamuoni DHARURA yoyote katika nchi hii?....ni sawa kabisa kwenu kuona mgao wa umeme unaendelea?......kwa hiyo nyie DHARURA ni mpaka mkwere aseme?.......:A S 13:

Dharura uionayo ni ya kujitakia kama sio kupikwa........
 
Kwa mara ya kwanza katika historia ya bunge letu, kamati hii ya Makamba ni ya utendaji. Wanatoa amri na kuingilia utendaji wa TANESCO na wizara halafu wanaonekana eti wako pragmatic. Mimi nakwambia mitambo ya Dowans ikishawashwa hutamsikia tena Makamba maana atakuwa amemaliza kazi aliyotumwa.

Nami pia ningependa nifahamishwe ni Kamati ipi ya Bunge kati ya hii ya Makamba( Nishati na madini) na ile ya Zitto( Mashirika ya Umma) ambayo TANESCO inatakiwa kufanya nayo kazi kwa karibu na kupokea maagizo/ maelekezo/ushauri wa moja kwa moja? Kwa nini TANESCO imekuwa shamba la bibi kwa wanasiasa wetu? Wabunge wetu humu JF nisaidia kujua majukumu, mipaka ya kazi za kamati hizi.
 
Ni kweli kabisa....gridi ina upungufu wa 200MW+ hiyo Dowans itatoa less than 100MW bado gap lipo.....kwa nini hatutafuti makampuni makubwa kama General Electric,Cummins etc badal ya makampuni haya yasiyoeleweka?

Hawa wana kitu kinaitwa ZERO TOLERENCE AS FAR AS CORRUPTION IS CONCERNED. Hata kuchangia harambee za vyama vya siasa hawaruhusiwi
 
Hawa wana kitu kinaitwa ZERO TOLERENCE AS FAR AS CORRUPTION IS CONCERNED. Hata kuchangia harambee za vyama vya siasa hawaruhusiwi

When a severe drought reduced Kenya's hydroelectric power to a
trickle, the versatility of Cummins Power Generation was admirably
demonstrated when 39 Rental Power units were relocated from
Ghana to Kenya-on the other side of Africa-in just 12 weeks.
 
namkubali january makamba, I wish yeye ndiyo angekuwa waziri na ngeleja angebaki mbunge.

Ndiko anakoelekea, ni suala la muda tu. Baba yake atakapong'atuka Ukatibu Mkuu wa CCM mwakani, January atakuwa waziri.
 
Kamati ya Bunge ikiongozwa na January Makamba haikukaa chini ikafikiria yenyewe tuache sias za chuki jamani. Kamati ilikutana na wataalamu mbalimbali kama Energy and Electric Power Engineers, wanasheria, development planners, economist na wao wenyewe kama wanasias. Katika swala la umeme ni sayansi pekee inayoweza kutukwamua na siyo siasa, wanasias kazi yao ni kushawishi.

Makamba alitamka bungeni kuwa kamati yake itafanya liwezekanalo ili kupata permanent solution ya umeme hapa nchini. Sasa kama nyie mnaona haiwezekani andikeni mapendekezo yenu ya kisayansi na siyo ya kisiasa yaani yanayowezekana yakifanyiwa kazi alafu myapeleke kwa kamati husika wao kazi yao ni kucompile na kuyawasilisha kwa speaker kama walivyofanya sasa. Kamati ya bunge inapoundwa lazima ihusishe makundi yote bungeni, nashangaa kama kamati hii ilikua inaongozwa na mtu wa CHADEMA ikaja na mapendekezo kama hayo sijui mngekosoa au vipi? Kwenye kamati ile kuna watu wenye vision kama January na Mnyika hivyo hawakukurupuka. Kumbuka Zittoalipendekeza mitambo ya dowans inunuliwe ikiambatana na mapendekezo kibao lakini badala ya kuwaza kisayansi siasa ikatawala matokeo yake tunapiga blabla.

Ushauri wangu kwa kamati ni kuwa isisikilize wanasiasa isikilize wataalamu maana hapa tulipo na matatizo tuliyo nayo sasa ni kutokana na kutosikiliza wataalamu na kusikiliza wanasiasa wantaka nini science needs only political will in solving national problem. Bush alikataa kusikiliza wataalamu wa vita kuhusu irak na Afghanistan na wachum akasikiliza kina rumsfeld wenye makampuni ya ujenzi na vyakula sasa kibao kimeigeukia marekani walioiponza wanauza vyakula na ujenzi tena wanaikopesha nchi ilihali waliyoiharibu ni Marekani.

Nasihi kamati zote za bunge zifanye kazi kwa kushirikisha wataalamu na kutojali itikadi za kisiasa au maslahi ya chama fulani. We need tangible solutions to our problems.
 
Kwa wasiojua ni kwamba TANESCO ina makubaliano na baadhi ya migodi kwamba wakikata umeme inabidi Tanesco iilipe migodi hiyo kiasi fulani kufidia hasara ya uzalishaji.Kiasi hicho inasemekana kinatakiwa kwenda kusaidia jamii.Sijui kama hii kamati inafahamu hili.
 
kwa wasiojua ni kwamba tanesco ina makubaliano na baadhi ya migodi kwamba wakikata umeme inabidi tanesco iilipe migodi hiyo kiasi fulani kufidia hasara ya uzalishaji.kiasi hicho inasemekana kinatakiwa kwenda kusaidia jamii.sijui kama hii kamati inafahamu hili.

:a s 13:
 
ongeeni na mtoe bla bla zote kama watakuwa wamevunja kanuni za nchi kwa kuingilia madaraka ya tanesco au wizara watanzania hatutaki kujua tunachohitaji umeme. kama makampuni ya madini yatapunguziwa umeme ili sisi tuweze kuishi kama zamani kwetu ni neema hatutaki kujua kama makamba na kamati yake wameingilia madaraka ya raisi au ya waziri mkuuu tunachohitaji ni umeme procedure baadae period.

Howard si vyema ku-generalize issue. Ni kweli kwamba watanzania tunahitaji umeme iwe tumeshaunganishwa Tanesco au tunataraji kuunganishwa, lakini kusema kwamba hatujali huo umeme unakujaje hilo si kweli. Sio mara zote kwamba the end justifies the means.
Ndani ya Tanesco kuna wazalendo wenye majibu ya matatizo ya umeme Tanzania tatizo hawapewi microphone na wanachoandika kutokana na tafiti mbalimbali kimejaa vumbi ndani ya makabati.

Kama mnakumbuka waziri Ngeleja alikuja bungeni na proposals (short, medium and long term). Sasa watuambie proposal za Makamba zimetokana na wataalam gani na zile za Ngeleja zilitokana na wataalam gani.
Tanesco limekuwa shamba la bibi kila mtu achuma anavyotaka.

January alipata kusema "tutaishauri serikali lakini ikikataa tutaishinikiza", yaweza kuwa ni kauli ya kizalendo lakini kwa kung'ang'ania Dowans kwa nini nisiamini M/Kiti wa kamati kabeba masilahi ya kundi la wabaka uchumi??

Hizi zote mie naziona ni sarakasi za kisiasa, sioni dhamira ya kweli ndani ya chama tawala na serikali kushughulikia tatizo la umeme. Tumekuwa taifa dhaifu lenye watu na viongozi dhaifu, ni waoga wa worst cases ndo maana tunatishwa tusipowasha mitambo ya dowans TRA watapoteza 840b lakini hawajawahi kusema TRA inapoteza bilioni ngapi kwa misamaha, rushwa, wizi n.k
Tunatishwa mahospitali yatakosa dawa wakati hatujui ni lini walisema yana dawa, na kama hali ni mbaya mbona wabunge wanapewa milioni 90 za kununua gari, mbona jet yetu inaruka kila leo mara uswisi, mauritania, congo, sasa iko paris.

Kama hali ni mbaya tuiche iwe mbaya to the very last point ili kila mwananchi ajue nani katufikisha hapa, maralia haitibiwi kwa panado hata siku moja. Proposal za kamati ni panado tu, huwezi mkajifungia ndani siku 12 mkaja na majibu ya umeme 2030 bila hata ya utafiti.

Dowans wakifanikiwa ama kuwasha mitambo yao ama kuiuza kwa serikali itakuwa ni ushindi kwa wabaka uchumi na fedheha kwa wazalendo. Binafsi niko tayari kusubiri majibu sahihi kuliko kupata raha ya kitambo huku utu wa mtanzania ukiendelea kufedeheshwa.

Cha msingi nunua tochi/taa za kichina ili kupunguza hatari ya mishumaa nyumbani kwako!
 
Hizo red hapo ndicho kikubwa ambacho mafisadi waliopo katika issue hii wnakitaka.
Wanataka watanzania wapate umeme kwa kutumia mitambo ile ya kifisadi ili muone umuhimu wa mikataba ile na mfunge midomo yenu ili wao waendelee kula kiulaiini.
Naona wamefanikiwa kwako. inasikitisha mno.

Tulishapoteza kujiamini Ndibalema,
Vita yetu na mafisadi inakuwa ngumu kwa sababu leo mtanzania hayuko tayari kuvumilia njaa.
Ndio maana wengine wanasema "watanzania wanachotaka ni umeme" ikimaanisha hawajali nani anauleta kwa gharama ipi.
 
cha ajabu zaid waziri mhusika kakaa kimyaa.... huyu january sijui february ametumwa..na baada ya mitambo kuwashwa tu hatasikika tenaa

ole wao tanesco wawashe mitambo bili kupitia mahakamani......maana shauri bado liko kule ....
 
Mhh nimeona post ya mtu mmoja hapa jf, labda nichangie kwa kucopy aliyoandika:

Kumezuka mchezo wa watu kumkweza Bwana January Makamba ati ni shupavu katika maamuzi yake ya Dowans ya kutuchinjilia mbali na gogoro linaloendelea! Naomba wanaomsifu wajibu yafuatayo

  1. Katika kutibu tatizo sugu la umeme kwa hatua za dharura zinazohitaji kuwashwa generator za Dowans, Je tunajua implications zake kwa kampuni inayoidai Tanesco? ilhali mgogoro ukiwa bado kwenye vyombo vya sheria?
  2. Je huyo Bw. Adawi anayesemwa yuko tayari kusamehe deni la Tanesco la zaidi ya Tshs 90 bio. amesema hayo wapi hayo kimaandishi? Wanasheria wapi walikuwepo kuweka sawa makubaliano hayo kisheria?
  3. Na hata kama kuna makubaliano ya umeme huo wa dharura nani anajua thamani ya mradi huo wa dharura? Ni vipi kama tukiuziwa 100MW kwa gharama itakayo-factor in deni lake na thamani halisi au zaidi ya umeme huo unaouzwa na faida lukuki? Hivi kwa nini huo mkataba wa dharura usiwe wazi tukauona? Bunge mbona haliusishwi ila kamati zake?
  4. Na mwisho huyu Makamba ana upeo gani wa mambo ya sheria kujifanya kijogoo namna hiyo kwa mambo anayochukulia kirejareja namna hiyo? amepewa ngapi mpaka sasa?
 
Tunaweza kuvumilia wiki mbili tu bado mvua zianze kunyesha mabwawa yatajaa, huu udharura una lake jambo nao hatuutaki, leo asubuhi mvua imebeep Dar Nadhani maeneo mengine itakuwa imepiga
 
Tunaweza kuvumilia wiki mbili tu bado mvua zianze kunyesha mabwawa yatajaa, huu udharura una lake jambo nao hatuutaki, leo asubuhi mvua imebeep Dar Nadhani maeneo mengine itakuwa imepiga

Hoja nzuri sana hii....unajua wakisaini na Dowans hiyo temporary contract na mvua zikanyesha basi tunalipa capacity charges mpaka mkataba uishe...tumelala gizani miezi mitatu sasa wiki mbili sio shida sana
 
Back
Top Bottom