Hongereni kwa majukumu ya leo waja jamvi.
Nikiri wazi kuwa kwa kipindi kirefu nimekuwa ndg msomaji tu hapa jukwaani. Na leo nimeona nishare nanyi jambo...
Nilikutana na huyu binti mida ya usiku, akili za usiku(ulevi) zikanifanya nisimame kumsaidia(kutupa ndoano). Hakusita kutaka msaada wa lifti mpaka eneo analoelekea. Tukiwa njiani ndipo stori za hapa na pale zikaendelea ikiwa ni pamoja na kujuana kwa kifupi.
Nilijikuta nafika mpaka mahali anapoishi. Kabla ya kuachana nikajaribu kuona kama ninaweza kuambulia kitu (niwazi kwamba mimi ni mstaarabu kwa kiasi flani. Nilikuwa radhi kumuacha aende zake) ila baada ya kuona kama kuna muelekeo nikakaza kamba na baada ya muda kweli nikapitishwa.
Nikaulizwa "kwahiyo unatakaje?"
Nikajibu "tutafute gesti" (mwanzo alisema anaishi na dada yake hapo gheto)
Nikaulizwa tena "wapi?"
Nikajibu "popote pa karibu"
Ndipo alipoomba dk kadhaa aende ndani kuchange then tutaenda machinjioni. Moyoni nilijiambia kuwa ndo style ya kuachwa kwenye mataa na mtoto wa mjini ila nikaamua hebu nimruhusu then nione. Kweli akaenda ndani na kama baada ya dk 5 akatoka. Kurudi kwenye gari akaniambia dada yake bado hajarudi. Hivyo kama vipi tuzame gheto. Akili za usiku zilizochanganyika na mhemko zikanipanda na kujikuta nimezama ndani.
Yalitokea yakutokea na baada ya shughuli nikaamriwa kumlipa, sikuona hiyana. Nikatoa elfu 10. Nikajibiwa haitoshi kwani gesti lazima ningelipia. Nikaongeza 10 nyingine. Nilijikuta nimeomba no ya simu then nikaondoka.
Kesho yake mchana nilimtafuta tena huyu binti, lengo likiwa ni kumsabahi (lakini pia kujaribu no ya simu kama ni fake au lah) bahati nzuri ilipatikana na tukaahidiana kuonana. Jioni ya siku hiyo tulionana, ndipo nilipoona kitu cha tofauti. Nakiri kwa dhati ya moyo huyu binti wa kichaga alikuwa kaumbika vema. Mcheshi na muwazi sana. Kwa muda mfupi nikajikuta namfahamu na kumzoea sana.
Ukurasa rasmi wa kufahamiana na kuanza mapenzi rasmi ukafunguliwa. Alikuwa wazi kwangu kuwa yeye ni Bar maid wa bar maarufu sana mitaa ya kinondoni.
Ndugu zangu binti huyu alinionyesha mapenzi ambayo sikutegemea hata kidogo, nilipikiwa chakula kitamu kila akiwa off (kwa hakika sijawahi kupikiwa chakula kuzuri namna hiyo before), huyu binti hajawahi kuniomba hela yoyote (nimekuwa nikichangia chakula na mambo mengine kama mwanaume ila sio kulazimishwa), amekuwa mtu wa karibu tofauti na nilivyotarajia, ni mjuzi na mtaalamu wa mapenzi (hapa mnaelewa), bila kusahau kupelekewa maji bafuni
Baada ya muda mrefu kuwa tunakutania kwake mara zote (sio kweli kwamba alikuwa anaishi na dadayake) siku moja akataka kufika kwangu. Nikamdanganya kuwa nimeoa. Dah, aisee palitokea ugomvi mkubwa siku hiyo. Mtoto alilia sana usiku kucha, nilimuonea huruma sana. Ila sikuwa na jinsi coz sikuwa nawazo wala kudhani kuwa ningeweza kuwa nae kama mke na mume (bado niko single af)
Baada ya tukio lile tulikubaliana tuachane kwa maana ya mapenzi ila tuwe marafiki. Ukweli toka tulipoachana nahuyu binti nimejikuta nampenda ghafla, amezidi kuwa mwema kwangu kiasi cha hata kunisaidia hela pale ninapomdanganya kuwa nina shida ili kumpima, zaidi nakumbuka ucheshi wake, mapishi yake na kila kitu.
Wana MMU nakiri huyu binti ameniteka sehemu ya akili yangu. Na ikimbukwe amekuwa muwazi sana kwangu, kiasi cha kuniachia simu yake mara zote nilipohitaji kukagua (ili kumtafutia kisingizio) nimekuwa nikitembelea bar yao mara kwa mara kwa kushtukiza ila mara zote sijawahi kuhisi tabia yoyote mbaya kutoka kwake.
Huyu binti mara zote amekuwa mshauri mzuri kwangu japo shule sio sana ila atleast anajua dunia inanyoenda. Kwa mda mfupi nimejikuta nimefanya mengi kwa ushauri wake. Ni yeye aliyeshinikiza kupima afya. (Sikuwahi kabisa kupima HIV kipindi cha nyuma) hivyo kupelekea kumuamini zaidi na kuenjoy sex.
Nakiri binti huyu anavigezo vyote vya kuwa mke kwa upande wangu. Ila mazingira niliyokutana nae pamoja na mazingira ya kazi yake vinanikosesha amani kabisa.
Nimeshawahi kuwa na mahusiano mengi kabla yake, ila naweza sema hiyu ni wapili kwa kuuteka moyo wangu ukiacha mke hewa wa kichuochuo.
Kwa wanaume kama umewahi kukutana nahali hii ulihandle vipi?
Msaada wa maombi ndio unahitajika zaidi
Nisameheni kwa muandiko mbaya. Bado Lerner hapa JF.
Usiku mwema wapendwa!