Nimezama kwa Bar Maid

Nimezama kwa Bar Maid

Kwa namna ulivyoelezea simulizi lako ni wazi upo njia panda na kibaya zaidi hatua ya mwanzo ya mahusiano yenu ilikuwa umeanzia mguu wa kushoto...

Mahusiano mengi yanayoanza kwa kudinyana baada tu ya tongozo la kwanza huishia hewani tu maana chanzo chake huwa ni mihemuko kuliko fukuto la penzi moyoni...
 
Kaka..nenda mkapime kwanza..kama fresh basi weka ndani kihalali maana naona umekufa umeoza ndugu yangu
 
concern yangu isije kuwa ameona kuna future anakufanyia maigizo? tozo aliyo ku charge siku ya kwanza inatia mashaka.inawezekana ni tabia yake ila wewe ni mteja wake watofauti ndo maana ameamua kukufanyia maigizo.cha muhimu kama umempenda mchunguze bro vuta jiko.yawezekana huyo ndo bahati yako.yawezekana kama ungemkuta kanisani huyo huyo saivi tungekuwa tunaongea mengine tukijianda kula ndafu
 
Yaan huyo ni mke kabisaaa, church sikuizi ni usanii tu mke ni ww unaemuona haijarishi wapi umemuona, km unaona aibu na kazi yake mfungulie biashara
 
concern yangu isije kuwa ameona kuna future anakufanyia maigizo? tozo aliyo ku charge siku ya kwanza inatia mashaka.inawezekana ni tabia yake ila wewe ni mteja wake watofauti ndo maana ameamua kukufanyia maigizo.cha muhimu kama umempenda mchunguze bro vuta jiko.yawezekana huyo ndo bahati yako.yawezekana kama ungemkuta kanisani huyo huyo saivi tungekuwa tunaongea mengine tukijianda kula ndafu
Mtazamo wangu na wako unaendanda mkuu. Thanks much
 
Muwe wapenzi for atleast 4 years.

Mpe mtaji afanye biashra nyingine, aachane na hiyo kazi ya sasa.

Naamini wapenzi wanakutana popote pale.

Mke wangu tulikutana kwenye bus la Kilimanjaro, alikuwa anagawa maji, i will never regret.
tunaomba usimulie kidogo
 
Mkuu unasema hujaona tabia mbaya wakati kakuuzia k !

Jaribu kuwa na uhusiano naye wa muda mrefu huku ukimchunguza zaidi kabla ya kuamua kumuidhinisha (kuoa) kabisa.
 
Story yako nimesoma btn lines kuna sehemu kama ulikuwa unatupiga fix hivi maana ukiwa muongo unatakiwa uwe na kumbukumbu. Kuna sehemu ulisema hajawahi kukuomba hela wakati siku ya kwanza kumnjunja alikulipisha hela sasa sijui ulikuwa umesahau au ndio umekuwa kipofu kwenye hilo penzi jipya
 
Usijali ndugu kama umempenda kutoka moyoni mfungulie biashara au kazi yoyote anayoweza kufanya tofauti na hiyo.
 
Umesema ana akili ya maisha. Kwanini usimuachishe kazi na kumpa mtaji wa biashara kama utaweza!?

Pale mwishoni mkuu nimeeleza kuwa mazingira niliyokutana nae pamoja na mazingira ya kazi ndio vyanipa wasiwasi mkuu. Ushauri wako nimeuelewa sana mkuu. Thanks
 
Tafuta rafiki yako yeyote, then umwambie aende hapo bar akamtongoze na ahakikishe kumuahidi dau kubwa kama 40,000 au 50000 baadaa ya kulala nae...na akomae kumsubiri hadi watakapomaliza kazi huku pale pale anampa care za kila aina including kununua msosi na vinywaji... wakienda kula tunda you know what to do..ila pia usishangae bbest yako akipendwa zaidi..ukubaliane tu na matokeo ya utafiti ila utupe mrejesho...
 
Endelea kupambana na hali yako mkuu,, kwa Hilo wacha nisiwe na swaga kabisa
 
Tafuta rafiki yako yeyote, then umwambie aende hapo bar akamtongoze na ahakikishe kumuahidi dau kubwa kama 40,000 au 50000 baadaa ya kulala nae...na akomae kumsubiri hadi watakapomaliza kazi huku pale pale anampa care za kila aina including kununua msosi na vinywaji... wakienda kula tunda you know what to do..ila pia usishangae bbest yako akipendwa zaidi..ukubaliane tu na matokeo ya utafiti ila utupe mrejesho...
Ukimchunguza sana bata huwezi kumla mkuu
 
Ujue hata nyoka siyo nyoka kama hajakung'ata. Bar ni bar tu na barmaid ni barmaid tu. Nakutakia jioni njema.
 
mkuu we jilipue tuu....ila kumbuka utamu wa nje na wa ndani ni tofauti....uwe na akili nyingi kuhakikisha furaha yako haibughudhiwi.....mwanamke atabaki kuwa mwanamke milele.....kila la kheri kamanda...
 
Back
Top Bottom