Kana-Ka-Nsungu
JF-Expert Member
- Oct 4, 2007
- 2,257
- 353
Niko kwenye kijimgahawa napata supu, meza ya pembeni kuna mama wa makamo yupo na mbaba mwingine nao wamekaa wanakunywa soda. Yule mama machozi yanamtiririka ikabidi nitege sikio japo niambulie mawili matatu ya kunijuza chanzo cha kilio chake.
Kwa niliyoyaskia niliweza kugundua kuwa mama ana kijana wake ambaye according to yeye amebambikwa kesi ya kumbaka mwanafunzi mwenzie, mama anadai huyo msichana alikuwa ni girl friend wa kijana wake na baba wa msichana amem frame up kumkomesha tu. Baba wa msichana ameshafungua kesi na anadai apewe laki tatu ili afute kesi. Yule mbaba aliyekaa nae pale nagundua kuwa ni mganga wa kienyeji na kwa kujiamini kabisa anamuambia mama "Usiwe na wasiwasi dada, nitafutie tu elfu arobaini tupoteze faili"
Toka siku hiyo najiuliza hivi inawezekanaje kwa hawa jamaa kupoteza mafaili? Hebu nijuzeni inakuwaje watu mlio na experience na haya mambo.
Kwa niliyoyaskia niliweza kugundua kuwa mama ana kijana wake ambaye according to yeye amebambikwa kesi ya kumbaka mwanafunzi mwenzie, mama anadai huyo msichana alikuwa ni girl friend wa kijana wake na baba wa msichana amem frame up kumkomesha tu. Baba wa msichana ameshafungua kesi na anadai apewe laki tatu ili afute kesi. Yule mbaba aliyekaa nae pale nagundua kuwa ni mganga wa kienyeji na kwa kujiamini kabisa anamuambia mama "Usiwe na wasiwasi dada, nitafutie tu elfu arobaini tupoteze faili"
Toka siku hiyo najiuliza hivi inawezekanaje kwa hawa jamaa kupoteza mafaili? Hebu nijuzeni inakuwaje watu mlio na experience na haya mambo.