Nimewakumbuka Marehemu Mama na Pacha wangu Japo sikuwahi kuwaona kwa Sura

Nimewakumbuka Marehemu Mama na Pacha wangu Japo sikuwahi kuwaona kwa Sura

Nusratt

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2024
Posts
1,707
Reaction score
4,192
Muda huu nimejikuta ghafla namkumbuka marehemu mama yangu, Mama mapacha Nusratt na Nasra.

Tulizaliwa mapacha na mimi nikiwa Dotto.
Kwa bahati mbaya nasikia mama alipata ajali akiwa na Kulwa (Nasra) wakati wakitoka hospitali ambako Kulwa alikuwa anaugua mafua na homa.

Mama na pacha wangu walisukumwa na gari dogo, Nasra alifia palepale eneo la ajali na mama alifia hospitali masaa machache baada ya kufikishwa hospitali.
Naambiwa nilikuwa na miezi 5 tu.

Baada ya maziko, baba yangu alinipeleka kwa bibi mzaa mama na hakuwahi kurudi tena mpaka leo hii.

Nimekua mkubwa sasa bila kuijua sura halisi ya mama yangu, pacha wangu Nasra wala sura ya baba yangu, zaidi ya kuwaona kwenye picha.

Huenda Nasra asingeugua siku ile, basi tungekuwa tuko familia kamili yaani sisi watoto, baba na mama yetu.

Niliendelea kukua nikijua bibi yangu ndie mama yangu mzazi mpaka pale siku moja aliponiambia ukweli kuhusu mimi, pacha wangu na wazazi wangu.

Nililia sana japo haikubadilisha uhalisia.
Bibi alinilea na kunisomesha kwa juhudi zote.
Aliuza mazao ili niende shule na hatimaye chuo.

Nilifanikiwa kiasi kupata elimu na kujiajiri.
Ila kabla bibi yangu hajafaidi matunda yangu vizuri, Mungu nae akamchukua bibi yangu.

Nimejikuta nakumbuka nilikotoka, nilipokuwa na hapa nilipo.

Mungu aendelee kumrehemu mama yangu, bibi yangu na pacha wangu. Hao ndio ndugu zangu kwani sikuwahi kumjua ndugu yangu yeyote yule.

Baba yangu alinitelekeza hivyo wala sitaki kujua kuhusu yeye.

Nimejikuta nawakumbuka sana.

View: https://youtu.be/cVb7QxyiuR4?si=eoSwWTiW4vt4z_K3
 
Kwa kiasi kikubwa inauma sana , ila lililo budi kutokea acha liwe, muhimu sala dua na maombi ni kwa hao walio tangulia ,kulwa ,mama na bibi wajaliwe kupumzika kwa amani.

Wewe shukuru kwa yote yalio tokea , usiache kumtafuta baba na tanguliza kumsamehe, pambana na maisha , nami nakuombea kufanikiwa.
Pole mno
 
Muda huu nimejikuta ghafla namkumbuka marehemu mama yangu, Mama mapacha Nusratt na Nasra.

Tulizaliwa mapacha na mimi nikiwa Dotto.
Kwa bahati mbaya nasikia mama alipata ajali akiwa na Kulwa (Nasra) wakati wakitoka hospitali ambako Kulwa alikuwa anaugua mafua na homa.

Mama na pacha wangu walisukumwa na gari dogo, Nasra alifia palepale eneo la ajali na mama alifia hospitali masaa machache baada ya kufikishwa hospitali.
Naambiwa nilikuwa na miezi 5 tu.


Baada ya maziko, baba yangu alinipeleka kwa bibi mzaa mama na hakuwahi kurudi tena mpaka leo hii.

Nimekua mkubwa sasa bila kuijua sura halisi ya mama yangu, pacha wangu Nasra wala sura ya baba yangu, zaidi ya kuwaona kwenye picha.

Huenda Nasra asingeugua siku ile, basi tungekuwa tuko familia kamili yaani sisi watoto, baba na mama yetu.

Niliendelea kukua nikijua bibi yangu ndie mama yangu mzazi mpaka pale siku moja aliponiambia ukweli kuhusu mimi, pacha wangu na wazazi wangu.

Nililia sana japo haikubadilisha uhalisia.
Bibi alinilea na kunisomesha kwa juhudi zote.
Aliuza mazao ili niende shule na hatimaye chuo.

Nilifanikiwa kiasi kupata elimu na kujiajiri.
Ila kabla bibi yangu hajafaidi matunda yangu vizuri, Mungu nae akamchukua bibi yangu.

Nimejikuta nakumbuka nilikotoka, nilipokuwa na hapa nilipo.

Mungu aendelee kumrehemu mama yangu, bibi yangu na pacha wangu. Hao ndio ndugu zangu kwani sikuwahi kumjua ndugu yangu yeyote yule.

Baba yangu alinitelekeza hivyo wala sitaki kujua kuhusu yeye.

Nimejikuta nawakumbuka sana.
Pole sana mamie, waendelee kupumzika kwa amani 🙏🏽

Wababa wanaotelekeza watoto wao ni 🚮🚮🚮🚮
 
Muda huu nimejikuta ghafla namkumbuka marehemu mama yangu, Mama mapacha Nusratt na Nasra.

Tulizaliwa mapacha na mimi nikiwa Dotto.
Kwa bahati mbaya nasikia mama alipata ajali akiwa na Kulwa (Nasra) wakati wakitoka hospitali ambako Kulwa alikuwa anaugua mafua na homa.

Mama na pacha wangu walisukumwa na gari dogo, Nasra alifia palepale eneo la ajali na mama alifia hospitali masaa machache baada ya kufikishwa hospitali.
Naambiwa nilikuwa na miezi 5 tu.


Baada ya maziko, baba yangu alinipeleka kwa bibi mzaa mama na hakuwahi kurudi tena mpaka leo hii.

Nimekua mkubwa sasa bila kuijua sura halisi ya mama yangu, pacha wangu Nasra wala sura ya baba yangu, zaidi ya kuwaona kwenye picha.

Huenda Nasra asingeugua siku ile, basi tungekuwa tuko familia kamili yaani sisi watoto, baba na mama yetu.

Niliendelea kukua nikijua bibi yangu ndie mama yangu mzazi mpaka pale siku moja aliponiambia ukweli kuhusu mimi, pacha wangu na wazazi wangu.

Nililia sana japo haikubadilisha uhalisia.
Bibi alinilea na kunisomesha kwa juhudi zote.
Aliuza mazao ili niende shule na hatimaye chuo.

Nilifanikiwa kiasi kupata elimu na kujiajiri.
Ila kabla bibi yangu hajafaidi matunda yangu vizuri, Mungu nae akamchukua bibi yangu.

Nimejikuta nakumbuka nilikotoka, nilipokuwa na hapa nilipo.

Mungu aendelee kumrehemu mama yangu, bibi yangu na pacha wangu. Hao ndio ndugu zangu kwani sikuwahi kumjua ndugu yangu yeyote yule.

Baba yangu alinitelekeza hivyo wala sitaki kujua kuhusu yeye.

Nimejikuta nawakumbuka sana.
Piga moyo konde
 
Kwa kiasi kikubwa inauma sana , ila lililo budi kutokea acha liwe, muhimu sala dua na maombi ni kwa hao walio tangulia ,kulwa ,mama na bibi wajaliwe kupumzika kwa amani.

Wewe shukuru kwa yote yalio tokea , usiache kumtafuta baba na tanguliza kumsamehe, pambana na maisha , nami nakuombea kufanikiwa.
Pole mno
Sijui kama nitaweza kumsamehe hata kama nikimpata.
Alifanya nikulie kwenye maisha ambayo hayakuwa ndoto yangu.
 
Back
Top Bottom