Ligaba
JF-Expert Member
- Oct 12, 2018
- 1,045
- 2,821
Wakuu Leo kwa upole nawasalimu wote kwa unyenyekevu wa kipekee uliojawa hofu na huzuni kubwa.
Utakapo jadili au kuchangia naomba uzingatie hili bila kuongeza sababu yoyote ya zaidi kuhusu mwenendo wangu wa maisha. Mimi ni mfanyakazi serikali na sana nimebase kwenye biashara zaidi ya kazi na zaidi sijihusishi na mambo yoyote ya uvunjaji wa sheria kwa maana ni RAIA mwema na niko highly respected katika mtaa wangu kutokana ni jitihada zangu za kimaendeleo kiasi cha kuwa role model wa vijana wengi mtaani. Niko ofisi zangu tatu ambazo zimekuwa zikiletea maendeleo kiasi cha watu kushangaa.
Kilichonistua Leo saa 4 usiku nikiwa nataka kufunga biashara yangu nimefuatwa na watu wawili waliokuja ofisini kwangu wakiwa katika gari aina ya Harrrier old model na kunifahamisha wao ni maofisa wa polisi kitengo cha upelelezi kutoka central polisi na mmoja amenionyesha kitambulisho lakini nikiwa na bumbuwazi hata sijakumbuka hata kunote jina.
Wamenifahamisha kwamba Nina kesi ilioko huko central na natakiwa kuondoka na wao usiku huu. Bahati nzuri dukani kwangu kuna ukuta wa nondo mtu hawezi ingia ndani. Nilipotaka wanijulishe Nina kesi gani? Hawakutaka na walitaka kutumia ubabe ila ilibidi niite jamaa zangu wanisaidie kujua tatizo. Baada ya kufika rafiki zangu wa jirani, jamaa wakashuka kidogo na wameniuliza maswali yafuatayo:-
1. Unaitwa Fulani (wakitumia professional yangu je ni kweli nina taaluma hiyo? Jibu ndio
2. Nina kitambulisho cha kazi au cha Uraia? Jibu ndio.
3. Kwa nini tulipoacha namba ofisini kwako takribani miezi miwili nyuma hukutaka kutupigia? Jibu, sikupewa taarifa na hamjaacha taarifa kwamba nyie ni polisi nilijua za watu tu kawaida na huwa simtafuti mtu bila shida.
Mwisho wameniachia ila wamenitaka kesho saa 4 nilipoti polisi central kwa mahojiano. Na wamenisihi kama nitakuwa na kitambulisho cha kazi nisiende na mdhamini ila kama sina lazima niende na mtu wa kunidhamini. Sikuwahi tegemea hata siku moja nitatakiwa kuripoti wanakoripoti watu wenye makosa makubwa hata Mara moja. Na mpaka muda huu usingizi sina siku hizi hawachelewi kukupa kesi ya uhujumu uchumi. Binafsi sijioni kuwa ni mtu wa hatari kwa kiwango hicho.
Naombeni msaada wa mtu mwenye uelewa wa matukio kama haya. Nina work ID je niende pekee yangu au nichukue backup? Msaada wenu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Utakapo jadili au kuchangia naomba uzingatie hili bila kuongeza sababu yoyote ya zaidi kuhusu mwenendo wangu wa maisha. Mimi ni mfanyakazi serikali na sana nimebase kwenye biashara zaidi ya kazi na zaidi sijihusishi na mambo yoyote ya uvunjaji wa sheria kwa maana ni RAIA mwema na niko highly respected katika mtaa wangu kutokana ni jitihada zangu za kimaendeleo kiasi cha kuwa role model wa vijana wengi mtaani. Niko ofisi zangu tatu ambazo zimekuwa zikiletea maendeleo kiasi cha watu kushangaa.
Kilichonistua Leo saa 4 usiku nikiwa nataka kufunga biashara yangu nimefuatwa na watu wawili waliokuja ofisini kwangu wakiwa katika gari aina ya Harrrier old model na kunifahamisha wao ni maofisa wa polisi kitengo cha upelelezi kutoka central polisi na mmoja amenionyesha kitambulisho lakini nikiwa na bumbuwazi hata sijakumbuka hata kunote jina.
Wamenifahamisha kwamba Nina kesi ilioko huko central na natakiwa kuondoka na wao usiku huu. Bahati nzuri dukani kwangu kuna ukuta wa nondo mtu hawezi ingia ndani. Nilipotaka wanijulishe Nina kesi gani? Hawakutaka na walitaka kutumia ubabe ila ilibidi niite jamaa zangu wanisaidie kujua tatizo. Baada ya kufika rafiki zangu wa jirani, jamaa wakashuka kidogo na wameniuliza maswali yafuatayo:-
1. Unaitwa Fulani (wakitumia professional yangu je ni kweli nina taaluma hiyo? Jibu ndio
2. Nina kitambulisho cha kazi au cha Uraia? Jibu ndio.
3. Kwa nini tulipoacha namba ofisini kwako takribani miezi miwili nyuma hukutaka kutupigia? Jibu, sikupewa taarifa na hamjaacha taarifa kwamba nyie ni polisi nilijua za watu tu kawaida na huwa simtafuti mtu bila shida.
Mwisho wameniachia ila wamenitaka kesho saa 4 nilipoti polisi central kwa mahojiano. Na wamenisihi kama nitakuwa na kitambulisho cha kazi nisiende na mdhamini ila kama sina lazima niende na mtu wa kunidhamini. Sikuwahi tegemea hata siku moja nitatakiwa kuripoti wanakoripoti watu wenye makosa makubwa hata Mara moja. Na mpaka muda huu usingizi sina siku hizi hawachelewi kukupa kesi ya uhujumu uchumi. Binafsi sijioni kuwa ni mtu wa hatari kwa kiwango hicho.
Naombeni msaada wa mtu mwenye uelewa wa matukio kama haya. Nina work ID je niende pekee yangu au nichukue backup? Msaada wenu.
Sent using Jamii Forums mobile app