Nimesutwa na mwanamke hadi nikawa mpole

Nimesutwa na mwanamke hadi nikawa mpole

flintsky

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
654
Reaction score
747
Habari za Jumapili,

Usiombe haya yakukute hata ungekuwa mbabe kama Scopion lazima uwe mdogo kama sisimizi.

Nina rafiki mmoja tumeshibana sana yaani ni zaidi ya rafiki au naweza kusema ameshakuwa ndugu yangu.

Ana mpenzi wake ameshamvalisha pete kitambo tu kinachosubiriwa ni ndoa tu, kiukweli yule mwanamke hajatulia kabisa ni zaidi ya mara moja nishamkuta katika mazingira sio mazuri tena wanaume tofauti na mapozi ya kimapenzi! Kuna rafiki yangu mwingine aliendaga nae hadi Mbeya akakaa nae wiki mzima huko yeye alienda kikazi.

Niliamua kukaa kimya maana kuingilia mapenzi ya watu mwisho utaonekana mchonganishi nikanyamaza ili jamaa mwenyewe siku aje ajionee lakini ikawa inaniuma sana naona rafiki yangu pale anapotezewa muda tu.

Nikaamua kujifunga mabomu nikamueleza nje ndani zote za mchumba wake! Jana nimefika ofisini asubuhi naambiwa natafutwa na mwanamke [emoji15] huku jamaa wananiangalia dizaini flani! Haijapita muda hamadi shemeji huyu hapa hajanawa hata uso wala kupiga mswaki kanisimamia mbele.

"Haya nieleze lini nilikuuzia maana unasema mimi nauza" jasho lilitoka nikaanza kusweti balaa ikabidi niwe mdogo nikajitetea tu kwamba nililewa ili niue soo, maana watu wa ofisini wakaanza kujipitisha wajue kuna nini? Daah! Yaani hapa najuta kumwambia msela nimeona namsaidia kumbe sikio la kufa haliskii dawa, sina hamu.
 
Hahahaaa...mimi naona ulistahili kupata hayo yaliyokutokea.

Safari ijayo, ili kuepukana na fedheha kama hiyo iliyokutokea, fanya yako na jali yako.

Ya wengine waachie wenyewe maana mwisho wa usabasi na kilomolomo nao huwa ni aibu.
 
Hahahaaa...mimi naona ulistahili kupata hayo yaliyokutokea.

Safari ijayo, ili kuepukana na fedheha kama hiyo iliyokutokea, fanya yako na jali yako.

Ya wengine waachie wenyewe maana mwisho wa usabasi na kilomolomo nao huwa ni aibu.
mi nilimshauri afanye uchunguzi ila yeye kaenda kumwambia!na mimi nilifanya kumsaidia jamaa sio kwa nia mbaya!ila poa ndio nimekoma
 
mwanaume kumweleza kitu alafu anatoka anaenda kumsimulia mke wake au mchumba,demu simfagilii hata kidogo ....angetuliza akili zake achuje yale uliomwambia na sio kukimbilia kumwambie huyo mchumbake.

Pia mwanaume kuwa mmbea mmbea nayo haiji kabisa.

Kwanza hilo la umbea wala halina jinsia.

Watu wangekuwa wanajali na kufanya yao na kuachana na ya wengine basi migogoro na mitafaruku hapa duniani ingekuwa michache sana.
 
mwanaume kumweleza kitu alafu anatoka anaenda kumsimulia mke wake au mchumba,demu simfagilii hata kidogo ....angetuliza akili zake achuje yale uliomwambia na sio kukimbilia kumwambie huyo mchumbake.
jamaa imebaki ananikwepa tu yaani kweli imaniuma kama mwanamke kweli anaweza kuvunja urafiki wetu wa siku nyingi
 
habari za jumapili !
usiombe haya yakukute hata ungekuwa mbabe kama scopion lazima uwe mdogo kama sisimizi!

Nina rafiki mmoja tumeshibana sana yaani ni zaidi ya rafiki au naweza kusema ameshakuwa ndugu yangu!

Ana mpenzi wake ameshamvalisha pete kitambo tu kinachosubiriwa ni ndoa tu!
kiukweli yule mwanamke hajatulia kabisa ni zaidi ya mara moja nishamkuta katika mazingira sio mazuri tena wanaume tofauti na mapozi ya kimapenzi!kuna rafiki yangu mwingine aliendaga nae hadi mbeya akakaa nae wiki mzima huko yeye alienda kikazi.
niliamua kukaa kimya maana kuingilia mapenzi ya watu mwisho utaonekana mchonganishi nikanyamaza ili jamaa mwenyewe siku aje ajionee!
lakini ikawa inaniuma sana naona rafiki yangu pale anapotezewa muda tu nikaamua kujifunga mabomu nikamueleza nje ndani zote za mchumba wake!jana nimefika ofisini asubuhi naambiwa natafutwa na mwanamke [emoji15] huku jamaa wananiaglngalia dizaini flani!
haijapita muda hamadi shemeji huyu hapa hajanawa hata uso wala kupiga mswaki kanisimamia mbele
"haya nieleze lini nilikuuzia maana unasema mimi nauza"jasho lilitoka nikaanza kusweti balaa ikabidi niwe mdogo nikajitetea tu kwamba nililewa ili niue soo maana watu wa ofisini wakaanza kujipitisha wajue kuna nini?!daahhh yaani hapa najuta kumwambia msela nimeona namsaidia kumbe sikio la kufa haliskii dawa sina hamu
Tunaomba na kapicha tafadhari
 
Wanakuaga kama mabaunsa! Unataka kutia kitumbua mchanga...
 
Ku
mi nilimshauri afanye uchunguzi ila yeye kaenda kumwambia!na mimi nilifanya kumsaidia jamaa sio kwa nia mbaya!ila poa ndio nimekoma
kuna siku atakukumbuka na atayakumbuka yote uliyomueleza.
 
Huna kosa ...kama mshikaji hajali muombe tu na wewe papuchi umle
 
Mianaume mingine baada ifanye utafit inaishia kumwambia mwanamke any but ethically you have done goodwill brother be confidently
 
Usithubutu kupeleka maneno kwa wapendano..hata kwa kutania.. utaumbuka.. wanaambiana kila kitu...
 
Back
Top Bottom