Nimesutwa na mwanamke hadi nikawa mpole

Nimesutwa na mwanamke hadi nikawa mpole

pole kwa msuto achana na watu wanaolala wote wakiwa uchi hujui nn wanapeana akiwa kifuani yote anayaongea halaf kingine asilimia nyingi ya wanaume hamna kabaroho
 
Pole mkuu lakin ulikuwa upo sahihi sana hata mim nisinge weza kaa kimya
 
Kuna kila dalili huyo msela wako huyo demu wake ana mlamba nyuma.
 
Duuh pole! Wenzako hawapeleki maneno mkuu! Unaandaa fumanizi ili jamaa asibishe
 
Ulilofanya sawa. Kama ni urafiki kufa heri ufe kuliko kuwa na rafiki wa namna hiyo. Wewe limsaidia kumpa mawazo amchunguze mchumba wake yeye mwenyewe. Lakini badala ya kufanya hivyo akaenda kumwambia. Iko siku atakuja kwako akilia na kukuomba msamaha wakati yatakapomkuta ya kumkuta
 
hawa viumbe wapo vizuri kwenye kuchamba sijui na wanawake wa kizungu wapo hivyo..?!!
unaweza kata hata kupita kwenye mtaa fulani kisa machambo yao hatari sana!
 
Ishu kama hii ilishawah nitokea. Mshkaji kaenda kumwambia dem wake kila kitu. Dem kaja na madem wenzake daah! Nilikua mdogo kama mbegu ya mchicha. Mshkaji alinichunia kama mwaka ndio anakuja kugundua kweli dem wake mgawaji. Niliapa kutofungua mdomo wangu
 
Acha dharau mkuu alokwambia kuwa waislam hawajasoma ni nani hebu tuthibitishie hapa Leo tujue kuwa hao waislam hawajasoma
[emoji23] [emoji23] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
Yaan wewe hadi MMU bado unawaza mambo ya shekhe!!!!

Yaani umeniacha hoi
 
Wahenga unena.Ukitafuta kisicho kuhusu utakipata kinachokuudhi.Naona mkuu umeyapata yanakuudhi...
 
pole kwa msuto achana na watu wanaolala wote wakiwa uchi hujui nn wanapeana akiwa kifuani yote anayaongea halaf kingine asilimia nyingi ya wanaume hamna kabaroho
Daaah
Nilikumis hadi nikaumwa.
 
habari za jumapili !
usiombe haya yakukute hata ungekuwa mbabe kama scopion lazima uwe mdogo kama sisimizi!

Nina rafiki mmoja tumeshibana sana yaani ni zaidi ya rafiki au naweza kusema ameshakuwa ndugu yangu!

Ana mpenzi wake ameshamvalisha pete kitambo tu kinachosubiriwa ni ndoa tu!
kiukweli yule mwanamke hajatulia kabisa ni zaidi ya mara moja nishamkuta katika mazingira sio mazuri tena wanaume tofauti na mapozi ya kimapenzi!kuna rafiki yangu mwingine aliendaga nae hadi mbeya akakaa nae wiki mzima huko yeye alienda kikazi.
niliamua kukaa kimya maana kuingilia mapenzi ya watu mwisho utaonekana mchonganishi nikanyamaza ili jamaa mwenyewe siku aje ajionee!
lakini ikawa inaniuma sana naona rafiki yangu pale anapotezewa muda tu nikaamua kujifunga mabomu nikamueleza nje ndani zote za mchumba wake!jana nimefika ofisini asubuhi naambiwa natafutwa na mwanamke [emoji15] huku jamaa wananiaglngalia dizaini flani!
haijapita muda hamadi shemeji huyu hapa hajanawa hata uso wala kupiga mswaki kanisimamia mbele
"haya nieleze lini nilikuuzia maana unasema mimi nauza"jasho lilitoka nikaanza kusweti balaa ikabidi niwe mdogo nikajitetea tu kwamba nililewa ili niue soo maana watu wa ofisini wakaanza kujipitisha wajue kuna nini?!daahhh yaani hapa najuta kumwambia msela nimeona namsaidia kumbe sikio la kufa haliskii dawa sina hamu
Ila tu mwambie tu kiume jamaa yako aache ufala au labda kama ana ndoto za kuishi na malaya.
 
Pia mwanaume kuwa mmbea mmbea nayo haiji kabisa.

Kwanza hilo la umbea wala halina jinsia.

Watu wangekuwa wanajali na kufanya yao na kuachana na ya wengine basi migogoro na mitafaruku hapa duniani ingekuwa michache sana.
Huu sio umbea. Hata mimi nikigundua nyendo zisizofaa kwa shemeji yangu yoyote naenda kumwambia mwenyewe achukue tahadhari, potelea mbali.
 
Mazingira tunayoishi yameshatufanya tuwe na mentality mbovu,hamna utu wala kuaminiana,na hulazimu watu kupiga kimya huku wakimuona mwenzao anadumbukia shimoni.

Ulikuwa na nia njema lakini imekuponza,na hili nimeliona sana,hata ndugu wanaweza kujua kuwa dada yao ana tatizo lakini wakakaa kimya,wakasema watajuana wenyewe mbele ya safari.

Swali? Je tunajenga au tunabomoa
 
Back
Top Bottom