Nimesitisha rasmi kuchangia harusi

Safi sana mkuu, watu hawachangii wagonjwa wanaoumwa wanahitaji dawa au vipimo hata 50k haifiki lkn wanachangia harusi.

Nina ndugu na wadogo zangu huko kijijini wanasoma kayumba kwa taabu halafu nijifanye mjini doninwa kuchangia harusi??

Mimi nilishakataa kata na wife wangu nae kaniunga mkono, tunachangia vitu vya lazima kama shule, safari ya lazima, vifo, magonjwa n.k
 
Harusi nitachangia, sito changia endapo sitokuwa na pesa. Pesa ni matokeo tu.
 
Wewe ulichangiwa kwenye harusi YAKO. Je waliokuchangia wangekuwa na fikra zako ungeweza kufanya sherehe bila msaada wowote?
 
Safi sana mkuu, watu hawachangii wagonjwa wanaoumwa wanahitaji dawa au vipimo hata 50k haifiki lkn wanachangia harusi.

Nina ndugu na wadogo zangu huko kijijini wanasoma kayumba kwa taabu halafu nijifanye mjini doninwa kuchangia harusi??

Mimi nilishakataa kata na wife wangu nae kaniunga mkono, tunachangia vitu vya lazima kama shule, safari ya lazima, vifo, magonjwa n.k
Vipi wewe wakati unaoa si ulichangiwa iweje wewe leo ukatae kuwachangia wenzio waliokuchangia? Ulitakiwa ukatae kuchangiwa then
 
Maharusi wanatangaza ndoa wakati hawana hata single cent wao akili yao wanawaza michango tu..
 
Kila mwanaume anapaswa kujipanga harusi yake iweje kwa kile alicho nacho. Kutangaza ukitegemea michango ni lawama. Watu tuna matatizo yetu na familia zetu, tufanye ya maana.
 
ukiendekeza haya mambo ni kero, juzi kuna mama kaja ana sare ya dera na mchango wa kitchen party alishaolewa miaka karibia nane sasa, walifunga ndoa bila sherehe eti leo ndiyo wanafanya harusi,
nimeona ni ujinga kuchangia vitu kama hivi.
ha hahahaha anataka avae shela
 
kinachoniudhi mimi ni watu kupanga m=bajeti kubwa kupitia mifuko ya watu ...... hivi mkienda kanisani au msikititini au serikalini mkafunga ndoa .. jioni mkakaa mahali mkala chakula kwa pamoja kila mtua akenda kwake hiyo itakuwa siyo ndoa au? tatizo tuanakazana harusi huku misingi ya ndoa hatujui ni ujinga aisee
 
Mimi sikumbuki mara ya mwisho nilichangia lini harusi. Nilishafanya maamuzi miaka mingi sana. Ndugu na marafiki wameshalijua hili hivyo hata mialiko sipati, na sioni shida maana sio lazima niende.
Nilifanya harusi ya binti yangu na sikuchangisha maana nilijikuna ninapofikia. siwezi kufanya kitu cha kifahari halafu the next day watu hamna hata chakula ndani, ni ujinga na ushamba pia.
ukioa au kuolewa jipange wewe na familia yako ambayo ni wazazi wako na ndugu zako wa kuzaliwa nao, mnaweza, lakini sio kuchangisha mpaka harusi inapita una maadui tayari wale ambao uliwalazimisha wakuchangie wakashindwa.
hii kitu iko Tanzania tu. tuchangie wagonjwa, bora hata na wanaosoma na misiba lakini harusi hapana. si lazima ufanye harusi ya mamilioni. muhimu ni ndoa ambayo haihitaji gharama kubwa.
Umefanya maamuzi mazuri, fanya vitu vya maendeleo achana na michango ya harusi haina tija
 
Siku hizi sio harusi tu. Michango ipo kwenye Ubatizo, Kipaimara, sijui mtoto "kafaulu" kutoka chekechea kuingia standard one na mambo luluki yasiyo na tija. Kina mama wengi ndio wanaotuingiza kwenye hii mitego.

Changia pale inapobidi na sema NO bila haya pale unapoona hii haijakaa sawa. Mtu atanuna siku 2 ila maisha yataendelea tu

Kuna watu wamezaliwa kupenda shughuli, kila utumbo lazima achange na ahudhurie, mara nyingi wamama. wanaume mnatakiwa kidogo muwe wakali huko nyumbani kwa wake zenu waachane na hivi vitu ambavyo havina maendeleo. Ukiongelea harusi inaambatana na send off, reception, kitchen party, kuna bag party pia siku hizi, ujinga mtupu. Bado mke hajashika mimba akafanyiwa baby shower au uswahilini wanaita beseni... ni michango tu, hamjashona sare, tena kwenye shughuli zote hizo... excuse me... hamnipati.. pesa yangu ina mambo lukuki ya maana sio upuuzi wa harusi na michango ya kishenzi isiyokwisha.
 
Temea mate mbali mjumbe usijilaani bure maana tutakula matunda ya vinywa vyetu.
Kwani kuolewa ni harusi mkuu?

Zamani si unaenda tu kwa baba na ng'ombe, unanichukua.

Sisi ukoo wetu tuna utamaduni wa get together. So mwanaume watamuona tu bila gharama za ziada.
 
Hii michango ya harusi,kitchen party,sendoff etc..inarudsha nyuma maendeleo..mtu usipokuwa makini hauendelei.
 
Wairi wa Habari na Utamamaduni Ndg.Nape angepiga tu marufuku michango ya harusi.Tungeokoa pesa nyingi.
 
Habari wadau

Katikati na mwishoni mwa miaka ya tisini tulikua tukichangia harusi 5000 unapata single card na 10,000 unapewa bibi na bwana
Mwanzoni mwa miaka ya 2000 hadi Katikati mwa 2000 tulikua tukichangia harusi 20,000 single na double 30-40 k

Michango ya harusi ikaenda inapanda hivyo hivyo, hadi 2010 ilikua 50-70 single na double ni kuanzia 100 k

Hivi navyoandika 2016 harusi ya jamaa yangu iliyoisha nimechangia 200k, hivyo tunaweza kusema sasa harusi nyingi Michango ni kuanzia 150-200 k na kuendelea
Kwa Hali hii naweza kusema Bila kupepesa macho Michango ya harusi za kileo imechangia kunirudisha nyuma maendeleo yangu binafsi kwa kiasi kikubwa

Mwezi Feb nilichangia harusi 4, each 100,000=
Mwezi huu wa Tatu nimechangia 2 tayari zote zinafanyika wiki hii, moja Thursday na nyingine siku ya pasaka wanabariki ndoa, zile ndoa nyingi zinazofungwa kwa pamoja

Kama mjuavyo koo zetu za wachaga ni kubwa mno, kama ukoo wetu roughly tunaweza kufikia watu 400 tuliopo dar, sasa kwa hali hii unaweza kukuta kila miezi 3 Kuna harusi kwenye ukoo huu, bado harusi za kazini, mtaani na alumni society, nimejaribu kupiga hesabu ya harusi nilizoandika kwenye diary tangu 2006 hadi sasa, jumla kuu niliyopata ningekua na nyumba zingine mbili ambazo ningekua nachukua kodi mbali na hii ninayoishi na familia yangu au ningekua hata na dala dala mbili zinazoleta hesabu

Au, ningeamua kufungua akaunti ya ada za watoto basi watoto wangu wangesoma miaka mingi sana Bila mm kuwazia ada, tofauti na sasa ikifika January ya kila mwaka kichwa kinauma

Naweka azimio, baada ya pasaka sichangii tena harusi, Bahati nzuri watu wangu wa karibu wote yaani tumbo letu tumeshamaliza suala hili , watoto wangu bado ni wadogo wapo primary school, hadi waje wafikie hatua ya harusi sio leo sichangii harusi iwe ndani au nje ya ukoo, sitawatamkia maneno haya bali nitakua nawazungusha tu hadi harusi inapita

Mungu nisaidie niweze kutimiza azimio hili kikamilifu, isiwe kama mara ya mwisho nilipoazimia nikashindwa

Amen
Uamuzi mzuri
mimi nilishaacha kuchangia harusi muda tu
 
Kwani kuolewa ni harusi mkuu?

Zamani si unaenda tu kwa baba na ng'ombe, unanichukua.

Sisi ukoo wetu tuna utamaduni wa get together. So mwanaume watamuona tu bila gharama za ziada.
Tamaduni hubadilika dada yangu utapata anayeamini katika sherehe maana hata za Tamaduni huwa na sherehe ndogo ambayo ndugu pia uchangia.
 
Back
Top Bottom