Nimepoteza ufunguo wa gari

Nimepoteza ufunguo wa gari

Ukishapata ufumbuzi wa ufunguo, ili tatizo lisitokee tena hakikisha unakuwa na keyFinde - ambapo waweza locate ufunguo wako kwa kutumia app ya simu au alarm.
Wakuu asanteni nimeupata ufunguo wa gari. Ulikuwa ndani ya begi ambalo huwa silitumii kabisa.
Sasa ni wakati muafaka wa kumiliki Keyfinder, ingia aliexpress au amazon
upload_2018-6-5_8-55-27.png
 
Ngoja nikachongeshe now...nahisi dalili kama hizi
 
Jitahidi ufungue mlango kisha fungua kitasa cha mlango Wa Driver kachonge funguo .
 
Home mitaa gani? Kama funguo imepotea jipange ununue ignition switch mpya ufunguliwe mlango ibadirishwe tu, kama gari ipo nyumbani mbona poa tu.
Sio lazima anunue ignition switch mpya. Akiweza kufungua mlango wanatoa hio ignition wanaitumia kuchonga meno kwenye funguo mpya.
 
Wakuu asanteni nimeupata ufunguo wa gari. Ulikuwa ndani ya begi ambalo huwa silitumii kabisa.
Asanteni kwa walio nitia moyo na walio nishauri. Nimejifunza mengi kupitia uzi huu.
Haya nenda kachonge funguo ya akiba.
 
Sio lazima anunue ignition switch mpya. Akiweza kufungua mlango wanatoa hio ignition wanaitumia kuchonga meno kwenye funguo mpya.

Ndicho jamaa alichofanya kwangu, nilimfata Ubungo, haikuchukua hata dakika kumi kazi ikawa imesha, akala 20,000/= fasta.
 
Ndicho jamaa alichofanya kwangu, nilimfata Ubungo, haikuchukua hata dakika kumi kazi ikawa imesha, akala 20,000/= fasta.
Ndo raha ya technolojia ya zamani, hizi gari mpya funguo ya ignition haichongeki inabidi ubadili ignition system nzima pamoja na ile computer yake au upate sehemu wanayoweza kuprogram ufunguo mpya ambayo sidhani kama itapungua laki.
 
Wakuu nimepoteza ufunguo wa gari. Toyota.

Nifanyeje?
Sina spare.
Tafuta fundi Aje afungue switch uende nayo mawasiliano kama uko Dar pemben ya barabara iingiayo sokoni kutoka Barabara ya Mandela watakuchongea ufunguo mujarabu.Mimi polis walinipotezea ufunguo wangu nikafanya hvo.
 
magari ya model za kizamani ndio yanatumia funguo magari ya ya kisasa kama hilo gari lako hewa yanatumia touch kama smartphone
Dah..mkuu..sijawahi kuona kufuli kwenye gari...zaidi ya kuona kwenye vyoo vya baa nyingi...hata hivyo magari ya huku kwetu yako wazi tuu...unaingia unasukumwa kwa nyuma...linawaka unasepa.....🙂
 
duh pole mkuu!, mwite fundi akufuate ulipo akuchongee...

nakumbuka kuna siku nilipoteza ufunguo wa pikipiki ya mtu aisee, yaani funguo ilidondoka bila mm kujua maana haikuzima, hadi nafika home yaani niizime nakuta ufunguo hakuna loh! sio kuchanganyikiwa kule....nilipanic sana, nikawaza chombo ya mtu nafanyaje...lakini baada ya kutulia kdogo tatizo likatatuliwa kwa mafundi tena kwa gharama ndogo sana wala sikuamini. nikajua nitamnunulia pikipiki mpya mwenye chombo kumbe mambo ni madogo sana yaani. usipanic sana, kwa gharama ndogo unatatua tatizo lako mkuu
 
Back
Top Bottom