Nimepoteza ufunguo wa gari

Nimepoteza ufunguo wa gari

Sasa unautafutia humu.
Au labda kama huenda kuna mtu kauona. Weka namba ya simu basi....
 
Dah...kumbe magari nayo hutumia funguo! Nilikuwa sijui kabisa....
Sio yote ndugu
Mie kagari kangu ni old model
Haitumii ufunguo inawashwa kwa kusukumwa nyuma,
Milango inafungwa kwa komeo,
Ndani hakuna viti huwa tumeweka stuli
Ndizo twakalia.
Pia haina break kusimama mpaka tuta mbele.
 
Unakuta utahangaika kote uko alafu funguo upo sehemu pakijinga kabisa isipokua unautafuta bila mafanikio
 
Inategemea na gari/model/mwaka.
Kama ni model ya zamani zaidi unaweza ukachongewa kama ni model mpya funguo zina chip ndani funguo hizi za kuchonga kawaida hazistart gari, funguo inabidi ifanyiwe programming na nadhani kwa kuwa ushapoteza inakuwa kasheshe, waone Manji Keys kisutu mtaa wa Zanaki.
Manji Key Master
Mkuuu umemaliza kazi, akifuata ushauri huu atapata suluhisho. Gari za kisasa ufunguo wa kuchonga kwa Mangi hauwashi gari bali utaweza kufungua mlango tu.
 
Wakuu asanteni nimeupata ufunguo wa gari. Ulikuwa ndani ya begi ambalo huwa silitumii kabisa.
Asanteni kwa walio nitia moyo na walio nishauri. Nimejifunza mengi kupitia uzi huu.
 
Mkuuu umemaliza kazi, akifuata ushauri huu atapata suluhisho. Gari za kisasa ufunguo wa kuchonga kwa Mangi hauwashi gari bali utaweza kufungua mlango tu.
Wakuu asanteni nimeupata ufunguo wa gari. Ulikuwa ndani ya begi ambalo huwa silitumii kabisa.
 
Heh. Kama huna usingizi kunywa kahawa kidogo ufungue kichwa. Maana kwa ushauri huu nina wasiwasi
Wakuu asanteni nimeupata ufunguo wa gari. Ulikuwa ndani ya begi ambalo huwa silitumii kabisa.
 
Kuchongesha funguo spare bila remote ni 15,000/= tu.

Sijui huwa mnajiamini kitu gani?
Wakuu asanteni nimeupata ufunguo wa gari. Ulikuwa ndani ya begi ambalo huwa silitumii kabisa.
 
Wakuu asanteni nimeupata ufunguo wa gari. Ulikuwa ndani ya begi ambalo huwa silitumii kabisa.
Sasa huku uliuwekeje?
Ulijifichia mwenyewe?
Jenga tabia ya kuweka funguo sehemu moja/maalumu.
 
Back
Top Bottom