Nimepewa namba ya simu na Demu

Bolfo Mkuu punguza hasira, msamehe mwenzio.

Jamani naomba tuwe wastaarabu jamani, hata kama unamjibu mtu jaribu ku-revise unavyomjibu mwenzako ili asikwazike. Pia Tuwe tunavumiliana hata mtu akikujibu vibaya mwambie awe anatumia lugha nzuri au vipi mpotezee.
Tuwe na amani jamani

naam mkuu, point tupu. Mfano tosha wa great thinker
 
Huyu boflo hadi leo yupo kwenye ignore list yangu. Nafikiria kumtoa maana kaonyesha kabadilika kidogo
 
NgumiJiwe lugha uliyotumia ilikuwa ya kumkandia mwenzio badala ya kumshauri, ina maudhi fulani. Pengine ungetumia lugha kama yangu angekuelewa.

no any offence was intended,sema jamaa aliichukulia too personal
 
Ok... Huyu demu ni jiran..na haya maeneo ninayokaa ni upanga huku majirani hawasalimiani.... Sasa huyu demu alikuwa chuo miaka 3 toka amerudi ana kama mwezi 1... Ndio maana
nikashangaa kusalimiwa na kupewa namba


Boflo umeama lini ILala, MBONA KIMYA KIMYA
 
Leo nimekutana na bibi akanikaribisha kwake jamani hv hii haifanani na kupewa namba eee!
 
Kupewa simu na huyo demu kunaweza kuwa na maana nyingi. Si mlikuwa mnaelewana kabla? Kwa kuwa mtaani kwenu majirani hawasemeshani, pengine kakupa ili apate angalau mtu wa kuzungumza naye.

Ninachokushauri usije kunasa katika upuuzi wa kufikiria kuwa kwa kuwa kakupa simu ndio anakutongoza. Na wala tena isiwe sababu ya kumkera mtoto wa watu kwa kupiga simu saa zote. Mheshimu kama jirani, kama dada, kama rafiki. Kukiwa na jengine lolote, wacha wakati uamue.
 
Ngumijiwe kumuita mwenzio shoga ni shogoe ndo nini maana yake.?
Papizo nae anacheeeeka mazuri hayo.
 
Wana Jf kuna jirani yangu hapa
Mtaa wa maweni ni bomba sana,
midume karibu yote ina mmezea mate,na ni msomi ametoka chuo karibuni,
Asubuhi leo wakati naenda grocery nikakutana nae akanisalimia halafu
akaniambia chukua namba yangu, mpaka sasa hivi nina maswali kibao
Siamini kupewa namba na ninaomba
ushauri wenu hivi kupewa namba ya simu ni ishara ya nini?

Mpende jirani yako kama.....Sasa we boflo unataka hata mkipatikana na shida ucku msipigiane cim ndo maana amekupa hiyo namba siyo kwamba anataka mnanihino!
 
Hakuna ajabu wewe ndo unataka kufanya mambo ya ajabu jirani yako huyo inaweza kutokea shida ukampigia
 
Ok... Huyu demu ni jiran..na haya maeneo ninayokaa ni upanga huku majirani hawasalimiani.... Sasa huyu demu alikuwa chuo miaka 3 toka amerudi ana kama mwezi 1... Ndio maana
nikashangaa kusalimiwa na kupewa namba

Bado maelezo yako yana walakini mkuu,from nowhere mtu akusalimie tu na kukupa namba?inatia ukakasi kidogo kuelewa unless kuna supported maelezo,kuwa wazi kama kweli uko serious na discussion.
 
Hahahahahahahah
kuna raha dunia hii
Hiyo ni number tu

Angekukonyeza je ungechukua kweli hiyo number?
au ungebaki hapo unatetemeka ...
 
Kwa kuwa ni jirani yako, amekupatia hiyo namba kwa ajili ya ulinzi shirikishi, ili kama kuna tatizo kama vile ukiona kibaka/wezi wanachungulia dirishani usiku umjulishe, au kama kwa bahati mbaya nyumba yake ikishika moto naye yupo kazini umlishe. Sasa wewe kwa kuwa ni kizazi chanyoka unaanza kuwaza UFENENGE. Acha hayo mawazo machafu, huyo ni jirani mwema.
 
Back
Top Bottom