nimepata mtoto wa kiume

nimepata mtoto wa kiume

AshaDii duh yaani hayo uliyoyasema ni maneno ya busara ever. Nakushukuru sana kwa kumpa mafunzo mema Mc Tilly Chizenga
Mc Tilly Chizenga hongera sana kwa kuongeza uzao katika dunia hii. Nawaombe sana wewe na mama na mtoto afya njema haswa mtoto na mama kwa wakati huu.
Uwe mfano bora kwa mwanao mlee katika uchaji wa Mungu akue katika malezi bora na wewe ukiwa kioo kwake aone mazuri yako.
Zingatia sana ushauri wa AshaDii na naamini kwa kuwa ni wa pili malezi unayajua au kama unajifunza wasiliana nasi tutakupa tips ulizokosa
 
Last edited by a moderator:
Mkuu
congratulations-on-baby-boy-birth-greeting-card.gif
 
Hongera sana mzee mzima wa kusherehesha, Mungu amjaalie afya njema huyo mwanao pamoja na mamaye!!
 
Hongera sana Mc Tilly, may Lord bless that cute boy of your to grow to be an important person in the country n the world.

asante dear Kaunga,pekundu panahusika sana hapo!nitapazingatia kila sekunde ya malezi yangu
 
hongera sana mkuu.
kumbe kimya chako kilikuwa na mshindo atii.
nijalie hali ya mama na mtt kwanza
 
AshaDii duh yaani hayo uliyoyasema ni maneno ya busara ever. Nakushukuru sana kwa kumpa mafunzo mema Mc Tilly Chizenga
Mc Tilly Chizenga hongera sana kwa kuongeza uzao katika dunia hii. Nawaombe sana wewe na mama na mtoto afya njema haswa mtoto na mama kwa wakati huu.
Uwe mfano bora kwa mwanao mlee katika uchaji wa Mungu akue katika malezi bora na wewe ukiwa kioo kwake aone mazuri yako.
Zingatia sana ushauri wa AshaDii na naamini kwa kuwa ni wa pili malezi unayajua au kama unajifunza wasiliana nasi tutakupa tips ulizokosa

asante kaka,nakuheshimu sana kiongozi!nitazingatia yote usemayo,ubarikiwe
 
hongera sana mkuu.
kumbe kimya chako kilikuwa na mshindo atii.
nijalie hali ya mama na mtt kwanza

yah mwalimu wa walimu,ilikuwa kila nikiingia ktk net mama ananitizama kwa jicho la njoo kwangu,basi naacha net nampetipeti!lol!
 
yah mwalimu wa walimu,ilikuwa kila nikiingia ktk net mama ananitizama kwa jicho la njoo kwangu,basi naacha net nampetipeti!lol!

good job.
sasa na kwa kipindi hiki ndo uache kabisa ili zile zamu za kumbembeleza mtoto usiku mshee wote.
usimwache akakesha alone lol!
 
good job.
sasa na kwa kipindi hiki ndo uache kabisa ili zile zamu za kumbembeleza mtoto usiku mshee wote.
usimwache akakesha alone lol!

mwalimu.mafunzo yako ni kama amri kwangu!nitakachofanya nitakuwa natenga kamuda kadogo kupitia hapa kuelimika kidogo na kisha kugonga likes za kutosha kisha huyo nasepa!mpaka mke wangu anipe cheti cha kuwa mume na baba bora!
 
Hongera baba napenda sana wababa wanaofurahia watoto na kuwakubali. Kama hambanwi na mila sana waweza mtahiri mapema kabla hata ya kufika miezi mitatu anapona haraka bila kujitonesha kidonda na mama anakuwepo kumuangalia kwa karibu as anakuwa maternity. Msaidie mvulana huyo aje kuwa baba mzuri na kuwaheshim wanawake kama mama yake na aje kuwa na mkewe kama wewe. Usisahau kumpeleka kwenye masinagogi( dini yako) hataiacha hata atakapokuwa mzee all the best

maneno yako yana thamani kubwa mno kwangu!nakosa namna bora ya kukushukuru!ASANTE MNOO
 
Hongera saaana Chizenga, wewe pamoja na mkeo.

Mwenyezi Mungu awajalie neema na upendo wa dhati ndani na kati ya familia yenu... Na zaidi ya yoote awashindishe mitihani yoote ambayo kila wanandoa upitia ikiwa kama namna moja wapo wa kuifanya iwe imara zaidi.

Tips;


  1. Watoto wa kiume hodari kweli kwa kulia (walio wengi) na kunyonya... Mkeo needs your support sasa hivi more that ever. Inategemea mnaishi vipi na kama mnawasaidizi, ila hizo responsibilities mlizo nazo kwa sasa ni 24/7 walau hadi Jr afike miaka miwili.
  2. Baba haina maana ya wewe kuitwa mume wake ama baba wa hao watoto... TOkana na trend ya kaka/baba zetu kutegea majukumu yao naomba jitahidi usiwepo kwenye hilo kundi.
  3. Mtoto mchanga ako so delicate.... Najua hilo wajua ila nakukumbusha inabidi kum handle with care... kama mwatumia saana AC punguzeni isiwe kali saana, kama sehem za baridi mm kave vizuri na kutosahau kofia na soksi always... Soksi husaidia kulinda dhidi ya pneumonia, kofia ulinda utosi wake ambao bado ni mchanga.
  4. Sijui kama unatabia ya kutoka nje ya ndoa yako ama lah... Ila kama wewe ni mmoja wao TAFADHALI oga uchafu wako na kuuacha huko huko kabla hujarudi nyumbani kwako. Usithubutu kumgusa mtoto ukiwa katika hali hiyo.
  5. Epuka malezi ya ulimbukeni... Hata kama una uwezo, watoto walee katika mazingira ya wao ku appreciate na kuweza ishi mahala na sehemu yoyote. Mtoto usimjengee kuona kuwa kuongea kiingereza ndio kuonekana wa maana kuliko lugha yake, mfanya athamini roots zake hasa kwa kujua hata kabila lako, la mkeo, Kiswahili na Kiingereza.. kwanza inamfanya awe na command nyingi ya lugha.
Epukeni kutumia watoto kama chambo hasa katika maugomvi yenu... Epukana kuambia tabia mbaya za wakubwa kama shangazi, babu, mjomba, binamu kwa mtoto, Ukimjengea mwanao kuwa na dharau kwa wakubwa hata kama kweli hao wakubwa wana mapungufu hayo inamjenga mtoto kuwa na dharau sana kwa jamii which in most cases hupelekea kutokuwepo na adabu. Naamini unataka wanao wakikua kila mtu aseme mtoto wa @Mc Tilly Chizenga
hakuna kama yulee..


Kila la kheri mkuu.... Happy holidays.​

ASANTE SANA ASHADII,nathamini sana muda wako uliotumia kuandika mengi yote mazuri kwangu!namna bora ya kukushukuru ni kuyatekeleza uliyoniambia,nami nitafanya hivyo!

no 4,hakika ningelikuwa na tabia hiyo au kuwahi kufanya hivyo japo kwa usiku mmoja maneno hayo yangenichoma sana!namshukuru Mungu sikuwahi kabla ya ndoa,wakati wote wa ndoa na ninaamini itakuwa hivyo mpaka sekunde ya mwisho nitakayopumua hapa duniani!
 
Hongera sana mkuu, ukikaa ukitafakari kwa makini, yale yote ambayo ulitamani wewe ufanyiwe wewe, sasa ndio wakati wake wa kuyalipa kwa mwanao. yale yote pia ambayo wazazi walikuzuia kuyafaanya utotoni mwako jaribu pia kuyafikiria, yale unayoona yalifaa uyafanye lakini ukanyimwa hio fursa, ni wakati pia wa kumaptia mwanao hayo.

Upendo wa kweli kwa mtoto ni pamoja na kumuonya na ikibidi kiboko kwa wakati wake azawadiwe, asikudanganye mtu kiboko kimetusaidia sana wengi wetu kuwa watu wema.

Pia Mkuu, akikua usimzoeshe kufanyiwa kazi na house girl, mfunze kutandika kitanda chake mwenyewe, chombo chake cha kulia ajue kukiosha, usafi na nguo zake afue mara moja moja mkuu pia kazi nyingine za nyumbani afanye. itamsaidia sana na atakuwa mkubwa akiwa responsible.

Maneno machache ya hekima yasema hivi
Mithali 22:6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
Mithali 13:24 Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.
Mithali 22:15Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.
Mithali 23:13 Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
Waefeso 6:4 Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.

kwa mamlaka niliyojipa mimi mwenyewe,ninakupasisha wewe Tized kuwa mtu mwenye busara na hekima.Alilolipasisha Mc Tilly Chizenga, BUJIBUJI asilipinge!neno hili limekuwa kweli.
 
niwashukuru wote kwa pamoja kwa kunipongeza na kunipa maneno ya busara na hekima!nitayatekeleza yote mazuri niliyoyapata hapa na nitakayoendelea kuyapata hapa
 
nashangazwa na upendo ulioko moyoni hutoka wapi?kwenye vyumba maalum au kwenye chemchem isiyo kwisha?namna nilivyokuwa nawapenda wazazi wangu,ndugu zangu na nilipompata mke wangu nikampenda mpaka nikadhani kamaliza upendo wote uliopo moyoni mwangu,nikapata mtoto wa kwanza,nampenda kuliko maelezo hata yeye mwenyewe ana miaka 3 lakini anajua,na sasa nashangaa nausikia moto wa upendo unanichoma kwa mwanangu mpendwa mpya!dah!upendo ni nini?unatoka wapi?una bonge la reserve enhe?
 
hureeeeeee!!!wow wow!!!!!tik tik tik!!!!mmmh na mi naye nashangilia utafikiri wa kwangu!!!anyway mtoto wa mwenzio ni wako pia hureeeeeeeeeee!!!
 
Back
Top Bottom