Huyu jamaa amefanyiwa uhamisho wa Ndani ya Halmashauri, kutoka Shule Moja kwenda nyingine Ndani ya Halmashauri. Ninachojua huo uhamisho utagharamiwa na DED mwenyewe kupitia OC za Idara ya Elimu(P/S) anayofanyia kazi mdau.
Nimewahi kuzunguka huko nilipokuwa nafanya biashara ya kununua Korosho, kwahiyo probably jamaa atakuwa amehamishwa kupelekwa maeneo ya Kitaya au Kilimahewa. Ingawa Nina Uhakika itakuwa Kitaya ndiyo ilikumbwa na machafuko ya kushambuliwa na Magaidi. Ingawa Ulinzi umeimarishwa saivi kuanzia Kitaya-Kilimahewa-Mnongodi-hadi Kitama I &II.
Kila la kheri Mkuu, Pesa yako ya Uhamisho utalipwa ingawa kwa kuchelewa kutegemeana na OC inavyokuja.
Mwanaume hachagui kazi, tuendelee kupambana.