Nimeota tena kuna mtu atakufa

Nimeota tena kuna mtu atakufa

Status
Not open for further replies.

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,973
Reaction score
831,535
f90a39315cbe412e8b6c642045c42d96.jpg
Mtu anaweza kudhani ni story ya kutunga la la hasha, sina faida kwenye hilo, hiki ni kitu kinatokea kwa mara ya tatu Leo... Mida ileile
Baada ya kuota tena Leo, nimesita mno kuweka hili bandiko lakini kuna sauti inanisisitiza niandike..
Nimeota sijaoteshwa kuwa kuna mtu atakufa..... Lakini kila nikimwangalia namuona mwisho shingoni... Sura inanipotea na nikikazana kunyanyua macho yanapata kiza kisha nashtuka
Ndoto zipo za aina nyingi
Kuna ndoto kinyume
Kuna ndoto za wazi
Kuna ndoto taarifa
Kuna ndoto maono
ed9ff9e1119cf829af794f20d510623e.jpg

Ndoto zenye tabia ya kujirudia rudia hizo ni ndoto taarifa ama maono... Watabiri wengi huzitumia sana hizi ndoto
Ndoto yangu pamoja na kujirudia lakini yaweza kuwa ndoto kinyume! Kwamba ukiota mtu atakufa basi itakuja kinyume chake kwamba kuna mtu atazaliwa
Lakini vilevile si lazima kiwe kifo cha roho kuachana na mwili, inawezekana ikawa mtu kuondolewa kwenye nafasi fulani kimadaraka ama mtu fulani kupata cheo kikubwa bila kutarajia (kumbuka vifo vingi sio jambo la kupanga)
Lakini pia inaweza kuwa na tafsiri ya mtu fulani kunusurika kifo au jambo lingine lolote baya... Ndoto nyingi hazina tafsiri moja, unachoangalia ni ile tafsiri inayoweza kuleta uhalisia zaidi kulingana na mazingira husika ya wakati huo
Ndoto ndoto hizi ukiwa muotaji sana halafu vitu unavyoota vikawa na uhalisia fulani kuna siku unaweza ukamwambia mtu WEWE UTAKUFA na akafa kweli
Kila ulalapo Mwombe sana Mungu kwa imani yako! Fanya dua, sali omba ndoto zako zitoke kwake na sio kuzimu.....
c5dd6dcdb5def787d112b832c64a6c5d.jpg
 
Nakushauri umfuate Mungu katika roho na kweli.
Omba na Mungu atakurehemu.
 
Niliota nakojoa ktk maji kumbe ninakojoa kitandani siendi tena mtoni kuoga.
Shikamooo Ndoto
 
Hope unajua kuomba na kuziuia kitu kusitokee, ndoto huwa inakuja mapema ili uweze izuia au uitamie itokee kwa njia ya maombi,

Ndoto ni ulimwengu wa roho kwanza...
 
Hata me ndoto zanagu zinakuaga na ukweli Kwa asilimia 50 nikiota kitu hasbuhi nitaona kitu icho sehemu yyt naomba kujua maana yake nini mtalamu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom