Nimeokota kitambulisho cha NIDA

Nimeokota kitambulisho cha NIDA

Kitendo cha kukipeleka kitambulisho chake kinatosha kabisa kuonyesha hujui chochote wala hujahusika hakuna muhalifu atakae mdhuru mtu na akapeleke kitambulisho chake polisi au kwenye ofisi yake
Kwa akili mbovu za Hawa polisi wetu unaweza sumbuliwa Bure.
 
Peleka polisi man. Niliokota wallet ina IDs kibao za mtu mmoja, nikaona ya ofisini kwake DIT. Hapo nimeokota Chang'ombe kule.

Kwakua nilikua na trip ya posta iyo siku, nikajifanya mwema nikaenda nacho DIT walinzi nikawavuka bila kuwaambia ila nilivoenda mapokezi nikawaambia. Nikawekwa sehemu akaja HR nikawa naongea nae.

Aisee kumbe jamaa alivamiwa jana yake alivokua anarudi kutoka kazini. Kaibiwa ibiwa ye yupo hospital.

Sema HR alikua muelewa, ila nikaacha taarifa zangu. Owner alikuja akanitafuta akiwa na polisi aone kama atanitambua ni moja ya watu niliomuattack, alivoniona tu akasema hapana uyu mrefu sana walikua wafupi. Nikasema dah. Wema huu.
Haaa haaa chupu chupu
 
Ndio nadhani wangeweka mfumo huo na kama mtu akibadili namba ya simu, kuwe na namna labda kuona namba za simu za muhusika kupitia namba ya NIDA kwenye mfumo wa NIDA.

Na zaidi kuwe na mfumo wa kuripoti kadi iliyopotea kwa mmiliki, ili ziweze kuonekana na wengine ambao wameokota. Yaani mtu akipoteza kadi atafute loss report itakayomuwezesha kuripoti tukio la kupotea kwenye mfumo wa NIDA.

Hii itasaidia watu kupata kadi zao kirahisi. Mfumo huu unaweza ukatumika hata kwenye sekta nyingine pia.
Kwenye vituo vya mwendokasi Kwa wakatisha tiketi Kuna vitambulisho kibao vilivyookotwa.
 
Peleka polisi man. Niliokota wallet ina IDs kibao za mtu mmoja, nikaona ya ofisini kwake DIT. Hapo nimeokota Chang'ombe kule.

Kwakua nilikua na trip ya posta iyo siku, nikajifanya mwema nikaenda nacho DIT walinzi nikawavuka bila kuwaambia ila nilivoenda mapokezi nikawaambia. Nikawekwa sehemu akaja HR nikawa naongea nae.

Aisee kumbe jamaa alivamiwa jana yake alivokua anarudi kutoka kazini. Kaibiwa ibiwa ye yupo hospital.

Sema HR alikua muelewa, ila nikaacha taarifa zangu. Owner alikuja akanitafuta akiwa na polisi aone kama atanitambua ni moja ya watu niliomuattack, alivoniona tu akasema hapana uyu mrefu sana walikua wafupi. Nikasema dah. Wema huu.
Ungezaliwa kama SENGA mkuu sijui ingekuaje
 
Kiongozi habari yako. Kitambulisho hicho ni chakwangu. Nakili nilidondosha mitaa hiyo nilipita wanapouza kuku wa kuchona. Nahisi nilidondosha maeneo hayo ya Ihumwa. Ni kitambulisho tu Sina kingine. Nakipataje. Kwa Sasa nipo Dodoma
 
Kiongozi habari yako. Kitambulisho hicho ni chakwangu. Nakili nilidondosha mitaa hiyo nilipita wanapouza kuku wa kuchona. Nahisi nilidondosha maeneo hayo ya Ihumwa. Ni kitambulisho tu Sina kingine. Nakipataje. Kwa Sasa nipo Dodoma
Unaweza kunitumia hata kwenye basi nikakilipia Haina shida.
 
Kuna jamaa aliwahi okota simu ya mtu ikamponza, akataka irudisha kwa nia nzuri lakini ikamponza. Kitambulisho nachoweza kuokota na nikatoa taarifa ni cha ndugu yangu. Vingine napotezea hapo hapo, sitaki usumbufu na vyombo vya dola.
Uko sahihi Mkuu na hivi Polisi yetu inatumia nguvu nyingi bila maarifa, utajuta kuzaliwa. Ndo maana hata Mtu akikuta Mtu kajinyonga anaogopa kutoa taarifa Polisi kwani Intelijensia yao ni duni mno na jamii inaogopa usumbufu na kubambikiwa. Jeshi la Polisi ni chanzo kikubwa sana cha uonevu, kubambikia watu kesi, uporaji nk. nlk
 
Kiongozi naomba tuwasiliane kwa namba hiyo kwa ajili ya kukipata kitambulisho au tuwasiliane humu nilipo unitumie kwenye basi. Majina ni hayohayo yaliyopo kwenye kitambulisho na namba ya simu hiyo hapo. Asante
 
nilishawai kuokota kitamburisho cha Nida nikakisoma jina na picha simjui nikakitupa hapohapo.hii Dunia ya sasa ni ya kishenzi.
 
Katoe kwanza taarifa kituo cha polisi
Unapeleka unaambiwa tulia nje huyu jamaa alikabwa na kuibiwa pikpik NDIO MAANA wengi tunavipita vina madhara yake
 
Back
Top Bottom