Kaizer
Platinum Member
- Sep 16, 2008
- 25,320
- 17,822
sinafungu, ni kwa nini u rule out kuwa wewe siye mkosaji kwa yale ambayo yametokea na kusababisha mshindwe kuonana kama matakwa yenu?
Kitendo cha wewe kutumia upenyu ulikuwa nao kulala na mkewe inatoa picha hata katika shughuli na hali ya kawaida wewe si wa kuaminika. Pengine anakukwepa kwa tabia zako fulani ambazo kwake hazimfurahishi, na pengine haya yote unayosema umemsaidia si wewe peke yako; kuna wengine wamefanya zaidi yako.
Inasikitisha sana kuwa siku zinavyozidi kwenda mbele jamii inakuwa ikichekelea yale ambayo huonekana ni kinyume na maadili ya kawaida ya kila siku. Umeona haitoshi wewe kutembea na mkewe ila pia ulitangaze kwa watu wengine.
Nakusihi angalia sana nyenendo zako, unaweza kuona kana kwamba yale unayofanya unakomesha kumbe unajikomesha mwenyewe. What goes around comes back around.
Miss you mama watoto wangu..hii comment nimeiapprove sisemi kitu tena