george aloyce
JF-Expert Member
- Aug 22, 2017
- 1,302
- 1,971
Nilimuoa mke wangu miaka 25 iliyopita akiwa na watoto wawili wa kiume aliowapata kwenye ndoa yake ya awali.
Niliwapenda sana wale watoto na kuwachukulia kama watoto wangu kabisa na hakuna aliyejua kuwa si wanangu kwani tuliishi pamoja kwa upendo kama familia moja.
Tuliishi kwa amani kwenye nyumba za kupanga wakati huo nikiwa nafanya kazi na nilihakikisha watoto wangu wanapata huduma zote muhimu ikiwamo kuwasomesha shule bora kabisa.
Baba yao mzazi hakuwahi kutoa msaada wa aina yoyote wala kuhudumia watoto wake wala kuonekana.
Watoto walikuwa na akili sana darasani na baada ya masomo wote walipata ajira mmoja ameajiriwa kama daktari na mwingine ni mwanasheria.
Kinachoniumiza ni kwamba baada ya kufanya hayo yote mke wangu na wanangu wa kufikia wameungana na baba yao mzazi na sasa wanaishi pamoja kama familia .
Kwa sasa sina pa kuishi nakaa leo kwa ndugu huyu, kesho ndugu yule. Mbaya zaidi wameniblock na hata nikipiga kwa kutumia simu zingine wakijua ni mimi wanakata simu na kuiblock hiyo namba ngeni niliyotumia.
Ndugu zangu wa mtandaoni naomba ushauri wenu, nifanye nini?
Niliwapenda sana wale watoto na kuwachukulia kama watoto wangu kabisa na hakuna aliyejua kuwa si wanangu kwani tuliishi pamoja kwa upendo kama familia moja.
Tuliishi kwa amani kwenye nyumba za kupanga wakati huo nikiwa nafanya kazi na nilihakikisha watoto wangu wanapata huduma zote muhimu ikiwamo kuwasomesha shule bora kabisa.
Baba yao mzazi hakuwahi kutoa msaada wa aina yoyote wala kuhudumia watoto wake wala kuonekana.
Watoto walikuwa na akili sana darasani na baada ya masomo wote walipata ajira mmoja ameajiriwa kama daktari na mwingine ni mwanasheria.
Kinachoniumiza ni kwamba baada ya kufanya hayo yote mke wangu na wanangu wa kufikia wameungana na baba yao mzazi na sasa wanaishi pamoja kama familia .
Kwa sasa sina pa kuishi nakaa leo kwa ndugu huyu, kesho ndugu yule. Mbaya zaidi wameniblock na hata nikipiga kwa kutumia simu zingine wakijua ni mimi wanakata simu na kuiblock hiyo namba ngeni niliyotumia.
Ndugu zangu wa mtandaoni naomba ushauri wenu, nifanye nini?