Nimemshika mchumba wangu na message ya kimapenzi

Nimemshika mchumba wangu na message ya kimapenzi

lutumbu

Member
Joined
Jan 18, 2013
Posts
9
Reaction score
1
Niko katika mahusiano ya kimapenzi kwa muda sasa mpaka kumchumbia huyu niliye naye na kuishi naye.Juzi kuna message ya kimapenzi imeingia kwenye simu yake.Cha kushangaza amekuwa mkali baada ya mimi kuishika simu yake kwa kigezo kwamba hamjui huyo mtumaji ila atamfuatilia then anijulishe. Kumwambia afanye hilo zoezi hapo tukiwa pamoja akakataa.Nishaurini bandugu hiyo ni halali kweli mimi kusubiria mpaka amfuatilie mhusika ndio aniambie?asamteni kwa ushauri.
 
Duuh kwanini hakupi namba ya huyo mhusika ucheki kama hawajuani, nafikiri ni muhimu kuweka msimamo wako
 
Lol...acha kupekenyua simu ya mpenzi wako. Wanasema eti ukifanya hivyo utajipa jakamoyo.

Kwa hiyo unachotakiwa kufanya ni kuficha kichwa chako mchangani na kujifanya kama hujui vile.
 
chukua hiyo namba na ufuatilie kama wanajuana au la. yeye kua mkali wewe kushika simu yake ujue kuna tatizo mahali. otherwise na yeye angekua anamshangaa mtumaji wa hiyo msg na angekushirikisha katika kumjua ni nani. Jiandae kwa usiyotegemea.
 
Lol...acha kupekenyua simu ya mpenzi wako. Wanasema eti ukifanya hivyo utajipa jakamoyo. Kwa hiyo unachotakiwa kufanya ni kuficha kichwa chako mchangani na kujifanya kama hujui vile.

Akifanya hivyo si ndo ataendelea kujiumiza maana kitu anakijua A to Z halafu ajifanye kama hakijui???????
 
Akifanya hivyo si ndo ataendelea kujiumiza maana kitu anakijua A to Z halafu ajifanye kama hakijui???????

Kuna sarcasm kwenye hicho nilichoandika na hiyo sarcasm inalenga katika kuonyesha stupidity na foolishness ambayo watu wa humu huionyesha.
 
Kosa ulilofanya ni wewe kupekua simu ya mwenzako,
Japo binadamu tumeumbiwa wivu ila ni vizuri kama na wewe ungeweza kuushinda wivu ulionao.
Chakufanya ni kumsubiri na kuangalia ni jibu gani atakalokupa ili na wewe uweze kulipima kwenye mizani yako.
 
Duh, binadamu ni wa ajabu sana! Mtu unaishi nae lakini bado anakucheat..!!! Mkuu huyo atakua BF wake wa zamani tu.
 
Kwakweli Mungu anijalie moyo wa subira kama nyie wenzangu! Yaani nimeona text halafu yeye anakuwa mkali! Kudadadeki! Sina muda wa kuomba ushauri mimi. Ngoja nizeeke zeeke kwanza labda hii midadi itaisha!
 
ulichokua unakitafuta kwnye cmu yake umekipata,pole!kwa nini akatae kufanya hilo zoezi mbele yako?something is wrong somewhere.
 
kuwa mvumilivu subiri jibu lake mpe nafasi ya kujieleza.lakini pia usimchunguze kwa staili iyo ya message utapata stress bure,pia onyesha kumjali hata kama wahisi kuna mwingine pia ongezaa upendo kwake na kumheshimu pia.
 
ukimchunguza bata hutamla
Jichunguze pia na wewe kama unamtimiziya vyote vya kiroho na kimwili
 
Duuuh kwa kuwa ulikuwa unatafuta kujua kitu basi bila shaka umejua!
 
Talking through experience acha kabisa hiyo maneno mkuu utakuja kufa kwa presha bure

Kibaruani kwetu tunatanianaga sana wakati mwingine kwa simu au sms. Nilimtumia dada sms ya matani kama ilivyo kawaida kumbe mchumba wake akapekua na kuikuta na nyingine demu ananiomba nimpeleke lunch

Niliponea chupu chupu kupigwa ngumi wakati hakuna kabisa mahusiano achiliambali kutamaniana
Lakini baada ya kuja kubaini ukweli aibu ilioje
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom