Nimempa kibuti rasmi

Dabil

JF-Expert Member
Sep 30, 2021
5,885
13,263
Wakuu salama !

Ipo hivi, nilikuwa na huyu manzi wangu ambaye tulikuwa tumepanga baada ya miezi kadhaa tuanze process za kutambulishana kwa wazazi lakini safari yetu imefika ukomo gafla ,nimependa tu kuwashirikisha kilichotokea na nimefanya maamuzi yangu ambayo naona ni sahihi.

Kwa vile tumekaa pamoja kwa kama mwaka mmoja na kila mtu ana mishe zake ila mda mwingi alikuwa anakuja kwangu na kukaa pamoja. Sasa ishu imekuja huwa yuko busy mda wote na simu kitu ambacho niliona amebadilika na pia alianza madharau kiasi kwamba wakati mwingine nimeona akae kwao maana ananiletea tu stress .

Mwezi uliyopita nilifungua laptop yangu ili niingie Facebook nikakuta amesign out ila hakuclear history kwahiyo nikiclick login moja kwa moja naingia kwenye account yake , nikaanza kusoma inbox kadhaa zote siyo mbaya ila nikawa na wasiwasi na jamaa mmoja ,maana inbox zimefuta lakini jamaa akituma msg ni Kama imeanzia katikati kumbe anazifuta ,nilikuta msg " we ni mtam tukutane tena weekend unipe tena basi".haalafu hamna jibu Wala salamu, nikaona hapa huyu manzi wangu anafuta msg.

Na Mimi ikawa ndo mchezo wangu jioni nikiingia kwenye laptop Kama msg haijafunguliwa nasoma halafu nafuta ili asione msg imesomwa. Basi nikajua hapa ndo kiburi inapoanzia.

Baada ya siku mbili nikamwambia umesahau kulog out kwenye computer halafu flani ni Nani mbona msg zake sizielewi ? Akasema simfahamu, nikamwambia Kama humu mfahamu anajuaje utam wako ? Akaniambia "aaah si unajua wanaume wanavyoshoboka simfahamu kabisa ndo maana sikumjibu .

Basi akaanza kurudisha mapenzi ya kinafki na kung'angania kurudi kulala kwangu.Tukakaa Kama week hivi ubusy ukaendelea tena mda wote Yuko busy kuchat hamna attention kwangu. Nikaamua nitafute mtego ili kuwe na kibuti ambacho hata yeye ataona sijamsingizia.

Nikaunda account fb kwa jina la jamaa na kujifanya Kama jamaa ,halafu nikamwadd kwa kutaanguliza Salam na kumwelezea kwamba ile account nimesahau password tuchat kwenye hii mpya . Wala hakujibu,gafla nikaddiwa kwa account nyingine yenye mrembo picha na jina tofuati ,akaniambia mi ndo flani ile account jamaa yangu anaweza kusoma msg tuwe huru huku.

Kwa siku mbili nikiwa nimerudi kwenye mishe basi nikiingia chumbani yeye anabaki sebuleni kwamba anaangalia movie kumbe anachat na Mimi, kifupi jamaa anamgonga sana, nimemwomba hadi picha za utupu katuma akidhani ni jamaa. Nimempanga tukutane chimbo kesho anipe utamu.Bila shaka nitatangulia lodge nione huyu mbuzi akijitokeza nampa kibuti bila kumsemesha.

MREJESHO .

Nilisubiri aende kwao ili nimwambie huko huko,nimefanya hivo makusudi ili ishu nzima isijekujulikana na watu waliotuzunguka . Nimemwuliza amekana kila kitu ,hata picha alizokuwa anatuma amezikana siyo yeye wakati kapiga bila hata filters .


Kwanza kukana tu niliona tunashindana bure wakati mi nimeshafanya maamuzi yangu,nikamwambia rasmi tusijuane na usikanyage kwangu,baada ya siku mbili akanitafuta na kukiri kwamba hakutegemea angefanya kitu kama na alikana kwasababu aliogopa akikiri nitamwacha .Nimemweleza msimamo na nimemwambia tushamalizana usinitafute.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom